Christina Shusho Kupepelusha bendera ya TanzaniaAfrica Gospel Music Awards



Kama ambavyo inafahamika, na Kama Ulikuwa Hufahamu basi Wacha Tukujuze kwa sasa, Mwanamuziki Bora Wa Kike Tanzania katika Anga za Kimataifa Christina Shusho ameingia Katika Mchakato wa Kushindania Tuzo Mbili mwaka huu 2012. Tuzo Ya Kwanza ni Mwanamuziki Bora Wa Kike Afrika na Tuzo Ya Pili ni Mwanamuziki Bora Kutoka Africa Mashariki.

Mashindano Hayo yanayoandaliwa kwa jina la Africa Gospel Music Awards Hufanyika kila Mwaka Mara moja katika Nchi ya Uingereza, Mwaka huu Mashindano hayo yatafanyika tarehe 7 Mwezi wa 7.
                        Christina Shusho akizungumza na Bloggers na Watumishi wa Mungu kuhusiana na tukio lililo mbele yake

Christina Shusho ni Mwanamuziki Pekee Wa Tanzania aliyeingia katika Tuzo hizo mwaka Jana na Mwaka huu. Timu Rasmi ya Kuhakikisha Christina Shusho anatwaa Taji Zote Mwaka huu inategemea kuzindua Kapeni Hiyo rasmi katika Viwanja Vya Dar Live Siku Ya Jumapili kuanzia saa 9 Alasili.

Ingawa Kura zimeanza kupigwa tangu tarehe 1 June, 2012 lakini Kampeni hizi Zinazinduliwa ili kutoa hamasa Kwa Watanzania ndani na Nje ya nchi kuweza Kushiriki Kumpigia Kura Mwanamuziki Huyu Wa Injili.
Papaa akimwambia jambo Christina Shusho kwa msisitizo



 Hata wewe Msomani Wangu Unaweza Kushiriki Kumpigia Kura Christina Shusho Mwaka huu Akatwa Tuzo hizi zitakazo Uweka Muziki Wa Injili Tanzania Katika Anga za Kimataifa.

Namna ya Kupiga Kura, Click Hapa.......http://africagospelawards.com/, then Uta click Nominees and Voting....http://africagospelawards.com/nominate.html

Chagua Jina Kutoka Category hii


ARTIST OF THE YEAR- EAST AFRICA
  1. Eko Dydda- Kenya
  2. Emmy Kosgei - Kenya
  3. Exodus- Uganda
  4. Christina Shusho- Tanzania
  5. Lam Lungwar- South Sudan
  6.  Sarah K-  Kenya
  7. Dawit Getachew-Ethiopia
  8. Kambua-Kenya
  9. Willie  Paul- Kenya
  10. Ann Marie Mutesi - Burundi

 FEMALE ARTIST OF THE YEAR
  1. Emmy Kosgei-Kenya
  2. Dena Mwana – Congo
  3. Ntokozo Mbambo- South Africa
  4. Rebecca- UK
  5. Gifty Osei- Ghana
  6. Kefee -Nigeria
  7. Onos Ariyo- Nigeria
  8. Diana Hamilton-UK
  9. Christina Shusho -Tanzania
  10. Lara George- Nigeria








Kutembea katika Roho ndani ya TAG Moshi na Apostle Onesmo Ndegi

Semina ya Neno la Mungu TAG Moshi ikiongozwa na Apostle Onesmo Ndegi wa Kanisa la Living Water Worship Centre, Katika Semina hiyo ya Siku 5 Apostle Onesmo Ndegi alikuwa akifundisha kuhusu kutembea katika Maisha ya Rohoni,Mwenyeji alikuwa ni Bishop Emmanueli Lazaro wa Kanisa la TAG Moshi. 
Siku zilikuwa za baraka sana kwa wale walioudhulio udhulia semina hiyo,maana walichokuwa wakifundishwa walikuwa wanakifanyia kazi na kuona matokeo yake.


Mwaka 2012 miezi michache iliyopita Living Water Centre waliandaa semina ya Neno la Mungu Mnenaji alikuwa ni Bishop Emmanueli Lazaro wa Kanisa la TAG Moshi,Semina hiyo ilikuwa ya Baraka sana kwa watu wengi walioudhulia semina hiyo.Baada ya hapo Bishop Emmanueli Lazaro alibarikiwa na Moyo wa Apostle Onesmo Ndegi jinsi kwa jinsi anavyo fundisha Neno la Mungu,Baada ya hapo Bishop Emmanueli Lazaro alimwandalia Apostle Ndegi semina Moshi kwa makusudi ya kusikiliza Neno kwa kijana wake.

Kama inavyofahamika  kuwa Apostle Onesmo Ndegi amepata Kibali ndani ya moyo wa Bishop Emmanuel Lazaro wa Kanisa la TAG Moshi, Lazaro ambaye ni Askofu wa Kwanza wa Kanisa la Tanzania Assemblies Of God.



Apostle Onesmo Ndegi akisistiza jambo wakati wa semina hiyo

Mnamo 26/06/2012 katika Kanisa la Living Water Center Kawe kutakuwa  Kongamano la Udhihilisho wa Utukufu wa Mungu  ambalo litajumuisha baadhi ya watumishi kutoka Tanzania na nje ya Tanzania Bishop Emmanueli Lazaro ni mmoja wa wanenaji katika Kongamano hilo.Watumishi Wengine watakao hudumu ni pamoja na Bishoop Dr Bernard Nwaka-Zambia,Apostle Dr Simpson Ngizela - South Africa na Bishop Emmanuel Tumwidike- Mbeya -Tanzania..


Baadhi ya waumini wa Kanisa la TAG Moshi kwa Bishop Emmanueli Lazaro wakifuatilia mafundisho kwa makini

Wanakwaya kanisani hapo wakimwabudu Mungu katika Semina hiyo
Kwa Sehemu ndani ya Kanisa umati wa waumini wa Moshi walioudhulia Semina hiyo ya Apostle Onesmo Ndegi katika kanisa la TAG
Maombezi na kufunguliwa pia ilikuwa ni sehemu ya Semina hiyo kama inavyoonekana






Baba na mwana Apostle Ndegi na Askofu Emmanueli Lazaro
Apostle Ndegi, wa pili kulia ni Mchungaji Alex wa Kanisa Living Water Center Moshi,wa tatu ni aliyewahi kujitambulisha kuwa ni kijana Bishop Lazaro,anaye fuatia ni Victor Ishengoma na mwisho ni Mr Rugambage ujumbe aliokuwa ameambatana na kutoka Living Water Centre Dar es salaam

Tamasha la John Shaban Magomeni TAG


Watu wajitokeza kuhudhilia walijitokeza kwa Wingi Katika Tamasha la Muziki wa Injili la KuSupport Mwanamuziki wa Muziki wa Injili John Shaban lililofanyika Jioni Ya Leo Katika Kanisa la TAG Magomeni.
Tamasha hilo lililosukumizwa pia na Wanamuziki Wakongwe kama Cosmas Chidumule, Makasy, John Komanya, Nelly, Stara Thomas, Upendo Kilahiro, Victor Aron na baadhi ya Kwaya Kutoka Jiji la Dar-es-Salaam.
Shughuli nzima ya hiyo ilikuwa ikiongozwa na. Mgeni Rasmi wa siku ya leo ni Mhe. Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dr. Fenella Mukangara.
 
Tamasha hilo lililokuwa maalum kwa ajili ya Kusifu na Kuabudu na Maombi kwa ajili ya Taifa Letu la Tanzania.

 
Mwanamziki wa Injili John Shabaani

Bishop John Komanya , Upendo Kilahiro na John Shabaani awakiimba

 John Shaban, Stella Joel na Mhe. Mgeni Rasmi Mhe. Waziri

 Mchungaji wa Kanisa la TAG Magomeni Pastor Kanemba akiwa na Mkewe siku ya Leo Kwenye Tamasha.
 Mwanamuziki wa Injili Stara Thomas alikuwepo kuhudumu Katika Tamasha hilo

Injili Nchini pia unajumuisha wazee wenye umri wao kama Cosmas Chidumule na Mzee Makasy
 
 
 Bishop John Komanya kushoto na Kulia ni Upendo Kilahiro ndani ya Tamasha 
 Watu Peopleeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee
 Nelly akiwa Jukwaani Kikazi zaidi siku ya Leo

Christian Bloggers wakiwa Kikazi zaidi siku ya hiyo,Kushoto ni Victor, Kati ni Papaa Ze Blogger na Kulia ni Tunu wakiwa Kikazi zaidi.

KAPOTIVE STAR SINGERS – BUKOBA





Kapotive Star Singers Kutoka Bukoba
KAPOTIVE Star Singers kutoka Bukoba Tanzania, ni kikundi kilichoanzishwa mwaka 2009, kikiwa na lengo la kueneza neno la Mungu kwa njia ya nyimbo za injili.

Kikundi hiki kinaundwa na waimbaji nane, wachezaji sita na wapiga vyombo wanne. Kikundi kinaongozwa na Mwl. Alexander Ndibalema – Mkurugenzi, Andrew Kagya – Mratibu, Theresia Kagya – Katibu, Claudius Mutabuzi – Mhasibu, Audax Mathias – Afisa masoko na Denis Deus – Afisa mahusiano. Na huduma zote za kitumishi wanafanyia wilayani  Bukoba mkoani  Kagera nchini Tanzania.
 
Tangu kuanzishwa kwake, kikundi kimeshatoa albums tano amabzo ni
Yesu ni Mwema
Zawadi ya Krismass
Naitamani Mbingu
Mama yetu
Asante Baba

Pastor Vijana Wanaohudumu Kazi Full Time

Baadhi ya Watumishi 10 Vijana Ambao wanamtumikia Mungu katika Kizazi Hiki.
 Watu Wanaokaribia Kustaafu wengi Walikuwa ndio Wanaokimbilia Kazi Ya Utumishi Wa Mungu.

Miaka Michache Iliyopita Kumekuwa na Wachungaji Wengi Sana Vijana Ambao Wameamua Kuwa Full Time Ministers Kwa Maana ya Kuchunga Makanisa na Wengine Kuwa na Huduma Kabisa ambazo zimekuwa zikiandaa Makongamano na Mikutano Ya Nje Kwa ajili ya Injili.

Watumishi hawa ni full time Worker kwenye Ufalme wa Kitumishi. Gonga hapa



 Pastor Justine Caleb ni Pastor wa Goshen Christian Miracle Centre ambao Kanisa liko Pale Ilala Boma.

 Pastor Isaac Mallonga, ambaye anahuduma yake Tehillah Ministry akiongoza Ibada za Kila Ijumaa pale Tehillah Mbezi Tangi Bovu pia huwa anahuduma za nje hasa kwa mashule ya secondari na Vyuo..
 
  Pastor Matthew. Pastor Matthew pichani akiwa ni Mke wake Rebecca Walianza Kazi Morogoro from Zero, na Kwa sasa Yuko Mkoani Mbeya akisimamia Radio Ya TAG na Pia Kufanya Huduma Vyuoni, Kwa Vijana na Kwenye Makanisa Mbalimbali, Pia ni Director Wa Friends On Friday Mbeya.

 Apostle Daniel Musokwa, Ni Miongoni mwa founder wa Tehillah Ministry. Daniel ni Senior wa Tehillah Mkoani Mbeya.

Pastor Daniel yuko Arusha anamtumikia Mungu Kama Youth Pastor. 

 Pastor Philip Kimaro Wa Calvary Arusha Pastor Philip Kimaro ni Mchungaji. Kati Ya Ma-Pastor ambao Wamesababisha Kanisa la Calvary kusifika kwa Praise and Worship hasa ile ya Kila Mwezi basi Pastor Philip ni nguzo mojawapo.

Ministry Of Jesus Christ" John Sembatwa.huduma ya Mafundisho Ya Neno la Mungu na Maombezi eneo la Kimara.
 Pastor Wanza Temu. Wakati Tehillah Dar inaanza hawa ndo walikuwa Waasisi, Mungu akamvuta huyu Jamaa kufanya kazi na Christ Embassy Tanzania. Wanza ni Pastor wa Christ Embassy hapa Tanzania eneo la Mbezi Makonde.
 Uliza Mwanza town utaambiwa Mwanza International Community Church utaambiwa. Alinza kama Muimbaji lakini aka-Catch fire, sasa hivi anaongoza Kanisa Mwanza Town. Pastor Zakayo Nzogere. Kanisa lake ni Mojawapo ya Makanisa ambayo vijana wengi sana pamoja na wanafunzi wanasali. Anapiga Neno si Mchezo, Prayers ndo usiseme, Kuimba mule mule, nakumbuka mwaka 2009 Uwanja wa Taifa akiwa Mc wa Campus Night alishika Kipaza kwenye wimbo wa "Storm Is Over Now". Kati Ya Message zako zooote nilizowahi Kuzisikia ambayo mpaka kesho sijaisahau "Strengthening Yourself In The Lord"-2010. Unaweza Mpata Facebook kama utakuwa unaenda Mwanza.
Huyu amevuka Border, Pastor Freddy Okello, Alipokuja Tanzania na Kusema Mungu amemwambia aje kutumika Tanzania niliona ni kati ya watu wa ajabu, from Uganda to Tanzania. Pastor Freddy ni Mchungaji wa Upper Room Ministry Kanisa Lake liko Opposite na Mlimani City Dar-es-Salaam. 

Ninaamini Kuna Wachungaji Vijana ambao hawajaolodheshwa hapa maana nafasi isingetosha wamejitoa kikamilifu kwa ajili ya Utumishi Wa Mungu. Mungu awabariki wao na Kazi yao Pia.







Source : http://samsasali.blogspot.com