Mzee wa Upako anenena

Mchungaji wa Kanisa la Maombezi la GRC na Ubungo, Dar es Salaam, Mchungaji Antony Lusekelo amewataka viongozi wa dini na Watanzania kwa jumla, kutambua kuwa Tanzania ni bora kuliko dini zao.

Mchungaji Lusekelo pia aliwataka viongozi wa dini kuendeleza vita dhidi ya rushwa huku akisema watoa rushwa na wapokeaji, wamejificha makanisani na kwenye misikiti.

Mchungaji Antony Lusekelo
Alitoa kauli hiyo jana jijini Dar es Salaam, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari  ambapo alisema viongozi wa dini lazima lazima washiriki katika mapambano ya rushwa bila woga.

Katika mazungumzo hayo, mchungaji huyo pia alisema  Serikali inapaswa kuwajibika kwa kutumia nguvu zake za kisheria katika kulinda amani, huku akinyoshea kidole tukio la hivi karibuni lililoashira kuvunja kwa amani, huku Serikali ikiwa haijachukua hatua.

Alisema hilo ni tatizo kubwa na kwamba  ni watu wengi wakiwamo viongozi wa dini kushindwa kusema ukweli kwa kuogopa maisha yao kuwa mafupi.

“Ni muhimu kila mwananchi kutambua kuwa  Tanzania ni bora kuliko Ukristo na Uislamu. Watu wengi wanaogopa kusema ukweli. Hata viongozi wa dini kwani watoa rushwa wamejificha misikitini na makanisani, tuendeleze mapambano dhidi ya rushwa ipo siku tutashinda,” alisema.

Kuhusu vurugu nchini, alisema chanzo ni viongozi wa dini  kuhubiri siasa za chuki misikitini  na makanisani.

“Vurugu siyo asili ya binadamu inatengenezwa, Serikali ina wajibu wa kutumia nguvu yake kisheria kuilinda amani na amani haishuki kutoka mbinguni au kwa maombi, inatengenezwa pia. Tatizo cheche za kidini zilipoanza hazikudhibitiwa. Serikali ilikuwepo, aidha kwa makusudi au bahati mbaya imelea cheche hizo,” alisema Lusekelo.

Lusekelo maarufu kama mzee wa Upako alisema  watu o wanataka nchi isikae kwa amani na kuandaa mazingira ya watu kukosea.

Paroko; Wanafunzi maisha si mteremko.

Wahitimu wa kidato cha Nne katika Sekondari ya Kata ya Kigonsera, na wale wa chuo cha Katekis, wilayani Mbinga mkoani Ruvuma, wametakiwa kuzingatia elimu kwa kuifanyia kazi na si vinginevyo kwa kuwa maisha siyo mteremko kama baadhi ya vijana wanavyodhani.

Wito huo ulitolewa na Paroko wa Kanisa Katoliki la Litembo wilayani humo, ambaye pia ni Mkurugenzi wa Miito (msimamia nidhamu kwa watawa), Joseph Ngai wakati wa ibada maalum ya wahitimu wa hao iliyofanyika katika Kanisa Kigonsera.

Paroko Ngai, alisema kuwa, baadhi ya vijana wa kitanzania wameyafanya maisha kuwa rahisi rahisi kwa kushindwa kufanya kazi, na badala yake wamekuwa wakijiingiza kwenye vitendo viovu ambavyo ni hatari mbele ya jamii.

“Vijana wangu mliohitimu leo, mmefundishwa maadili mema ya kielimu na kiroho, hivyo naamini mtakuwa mfano bora mbele ya jamii na Taifa zima, mkipata ajira msifikirie kupata maslahi tu; bila kuwajibika,”alisema Paroko huyo.

 Akigeukia upande wa kiroho kwa wahitimu hao, Paroko Ngai aliwataka kuhakikisha elimu ya Sekondari na ya kiroho waliyoipata wanamtangaza Kristo kokote waendako, ikiwa ni pamoja na kutoa elimu kwa watu wanaompinga Kristo.

 “Najua kazi ya kumtangaza kristo ni kazi ya kukatishwa tamaa na baadhi ya watu ambao hawana nia njema na utume huo, hivyo mnatakiwa kujipa moyo na kumuomba Mungu kwa kuwa hata waacha milele,”alisema mkuu huyo wa miito.   

Kwa namna nyingine Paroko huyo aliwahimiza wahitimu hao 16 kuwa na moyo wa shukrani kwa Mungu, kwa kuwa wao wamebahatika kupata elimu hiyo ambayo wengine hawakuweza kuipata.

‘Nilishuhudia wanafunzi 30 wakiuawa kinyama’

“Naweza kukumbuka vyema siku ya msiba wetu, ilikuwa ni usiku wa manane tulipovamiwa chuoni na kulazimishwa kutoka nje ya vyumba vyetu. Wauaji wakiwa na bunduki za kivita AK 47, sumu, mishale na visu vikali, walianza kuwahoji wanafunzi majina yao, wale waliokuwa na majina ya Kikristo walipigwa risasi na wengine kuchinjwa kwa kisu. Miili yao ilipangwa mistari nje ya majengo ya chuo. Wanafunzi waliokuwa na majina ya asili walitakiwa kutaja baadhi ya aya za kuran, walioweza walipona na walioshindwa waliuawa hapo hapo.”

Hiyo ni sehemu ya maelezo ya Bw. Elkanah Sardauna, mwanafunzi aliyenusurika kimiujiza kuuawa katika mauaji yanayofanana na mateso ya Mpinga Kristo, yaliyotokea mwezi uliopita katika Chuo Kikuu kimoja kilichopo Kaskazini mwa Nigeria na kuistaajabisha dunia.

Akielezea mkasa mzima kwa machozi huku akiwa amelazwa katika hospitali ya Mubi,  Sardauna alisema kuwa njia ya kuepuka kifo ilikuwa ni kuukana Ukristo na kutaja jina tu  kulitosha kuwafahamisha wauaji kuwa ni Mkristo, alienda mbali zaidi na kuwaambia wazi jina lake na kuwa yeye ni Mkristo.

Hata pale alipopigwa hadi kuanguka chini na kisha kuonywa kutotaja tena jina la Yesu aliendelea kusisitiza kuwa ni Mkristo. Na kwa kweli alikuwa tayari kwa lolote, lakini si kumkana Yesu.

Mwanafunzi huyo akiwa na maumivu makali alitanabaisha: “Walipotoka nje kila mtu alishikwa na bumbuwazi kwa kile kilichokuwa kikiendelea. Ilikuwa kama sinema na hakuna aliyejua nini kitatokea, ghafla ikatolewa amri ya kutoka nje na kila mtu kutaja jina lake, huku mauaji yakiendelea.”

Alieleza kwamba kila mmoja pasipo kujiandaa alianza kueleza anaitwa nani, na hapo sasa ikajulikana nani ni Muislamu na nani ni Mkristo, kwa waliokuwa na majina yasiyoeleweka (Kilugha) alitakiwa kutaja vifungu flani vya kuran.

Hata hivyo wanachuo wengi walishindwa mtihani wa kutaja aya hizo za Kuran na wakaangukia mikononi mwa mauti wakiaminika kuwa ni Wakristo waliojifanya Waislamu ili kukimbia kifo cha kuchinjwa.

“Walipofika kwangu waliniuliza jina langu, niliwaambia mimi ni Mkristo naitwa Elkanah, baada ya kusikia hivyo walinisukuma chini na kupaza sauti zao wakisema ‘Allahu Akbar.’ Nililia na kumwita Yesu pale pale chini. Walinitaka ninyamaze nisitaje jina hilo tena, lakini niliendelea na hapo wakanipiga risasi mkononi na kunichinja sehemu ya shingo yangu.

“Kabla ya kunikata sehemu ya shingo yangu walinitaka nilikane jina la Yesu na imani yangu ya Kristo, kwa kweli nilikataa. Walisema kuwa kila atakayekubali kufanya kile walichokuwa wakitaka basi uzima wake uko mikononi mwao. Kweli walikua na chuki kali dhidi ya Ukristo.”

Baada ya tukio hilo, Sardauna anaeleza kwamba walimtupa chini na wakadhani amekwisha fariki, wakamwacha na kuondoka zao.  

 “Ni Mungu tu aliyeniokoa kwani walipokuja kwenye bweni letu tukulikuwa wanafunzi wanne ambao tunalala chumba kimoja, sisi wote tulikuwa na majina ya kikristo, wanafunzi wenzangu watatu waliuawa mbele ya macho yangu,” alisema kwa majonzi.

Niliokotwa na kupelekwa hospitali na Mwandishi wa habari ambaye alibaini kuwa bado nilikuwa hai na nilihudumiwa na hapa naendelea na maisha. Nadhani Mungu ameuhifadhi hai uhai wangu kwa kusudi lake,” alisema kijana huyo.

Kiongozi mmoja wa kikristo nchini Nigeria, Mchungaji Gideon Para Mallam, ambaye pia ni Katibu wa Shirikisho la Kimataifa la wanafunzi wanaotoka katika makanisa ya kiinjilisti, ‘International Federation of Evangelical Students,’ aliliambia Shirika la Habari la Open Doors kuwa si tu kwamba vifo hivyo vinasikitisha, lakini pia wanaua taifa la kesho."

Afisa mmoja wa usalama aliliambia Shirika hilo la Habari kuwa, kundi la Boko Haram ni mchanganyiko wa watu wenye mafunzo ya kivita kutoka sehemu mbalimbali za dunia walihamia jimboni humo.  Mpaka sasa wanachama wa kundi hilo waliokamatwa kutokana na matukio hayo ya mauaji ni 154 na 30 kati yao waliuawa kabla ya tukio la kuwaua wanafunzi huko Mubi.

Alisema kwamba miongoni mwa silaha ambazo polisi walizikamata katika msako baada ya mauaji hayo zikiaminika kuwa zilitumika kuua wanafunzi hao ni pamoja na AK47, Sub Machine gan, sumu, mishale na visu.

Siku mbili tu kabla ya mauaji hayo, Chuo hicho kilikuwa na uchaguzi wa viongozi wa serikali ya wanafunzi na wengi wao waliuawa tena wakitajwa kuwa walikuwa Wakristo.

Shirika la Habari la ‘The Christian Association of Nigeria (CAN)  limebainisha kwamba wauaji hao ‘jihadists’ kabla ya kufanya tukio hilo walisambaza barua kwa waamini katika eneo hilo  wakiwataka kuikana imani ya Kikristo ndani ya wiki mbili au wasubiri maumivu, huku wakiwakataza kuonyesha onyo hilo kwa watu wa usalama kwa kuwa kufanya hivyo kungemaanisha kujihukumu kifo.

CAN ilisema wanaamini kuwa Boko Haram wanahusika moja kwa moja na tukio hilo ingawa Waislamu nchini humo wanakataa. Hata hivyo Shirika la Utangazaji la BBC lilieleza kwamba katika uchaguzi uliofanyika shuleni hapo walimchagua rais wa serikali ya wanafunzi ambaye ni Mkristo, ambaye ni miongoni mwa wanafunzi waliuawa.

Rais wa CAN, Mchungaji Ayo Oritsejafor, alisema kuwa amesikitishwa na mauaji ya wanafunzi wasiokuwa na hatia na kwamba wamelitaka Jeshi la Polisi kuhakikisha kuwa linawakamata wote waliohusika na kuwaachia wasiohusika.

"CAN tunaamini katika umoja na kwa namna hiyo tunawaomba wanawake na wanaume wenye mapenzi mema kujitokeza kuungana na serikali kutafuta wauaji,” alisema.

Hata hivyo Jeshi la Polisi lilikamata wanafunzi wengine waliosalimika ambao walieleza kwamba miongoni mwa wanafunzi hao wapo ambao ni sehemu ya mtandao wa Boko Haram. 

Naye Mchungaji wa Kanisa la Anglican, Gideon Adamu anaeleza kwamba inawezekana kuwa ni mambo ya kisiasa, huku akibainisha kwamba kaka yake naye aliwahi kupigwa risasi begani na mwisho wa siku alifariki.

Kiongozi mmoja wa kanisa dogo eneo hilo la Mubi, akiongea na Open Door, alisema kuwa licha ya mambo yote yaliyotokea, lakini kwa imani yao hawawezi kulipiza kisasi.

“Hatuwezi kuonyesha udhaifu wa kukimbia kutoka katika eneo hili, hapa ndipo Bwana alipotuita, tutakaa na kutimiza wito wetu kwa Mungu,”

Rais wa Nigeria, Goodluck Jonathan akiongea na ndugu wa wanafunzi waliofariki alisema kutokana na tukio hilo maswali yamekuwa mengi kuliko majibu, huku akiongeza kwamba Boko Haram wamekuwa wakitumia nguvu za majeshi yao.

Mchungaji Msigwa aendelea kuibana wizara Maliasili na Utalii

Waziri Kivuli wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Mchungaji Peter Msigwa, amesema wizi wa pembe za ndovu pamoja na kuuliwa kwa wanyama, ni matokeo ya idara hiyo kuendelea kuwalinda majangili badala ya kuwachukulia hatua.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Mchungaji Msigwa, alisema Rais Jakaya Kikwete, anatakiwa kuingilia kati na kuvunja mtandao wa ujangili ili kunusuru wanyamapori na maliasili nyingine za Taifa.

Mchungaji Msigwa ambaye pia ni Mbunge wa Iringa Mjini (Chadema), alisema mpaka sasa ni miezi mitatu tangu alipowasilisha taarifa za ujangili bungeni na kumtaka Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamis Kagasheki, achukue hatua dhidi ya majangili hao na matokeo yake amewajibisha watu watatu wa Idara ya Wanyamapori huku watuhumiwa wakubwa wakiachwa.
Waziri Kivuli wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Mchungaji Peter Msigwa


Alisema jambo hilo ni hatari na kusababisha idadi ya wanyama kupungua kila wakati.

Alisema wiki iliyopita, pembe za ndovu zenye uzito wa tani nne kutoka Tanzania na Kenya zenye thamani ya Sh. bilioni 2.5, ziliripotiwa kukamatwa na vyombo vya usalama vya mamlaka ya Jiji la Hong Kong.

Mchungaji Msigwa alisema tangu kutokea kwa tukio hilo mpaka sasa, waziri husika amekaa kimya pamoja na serikali yake juu ya suala hilo kana kwamba kilichotokea ni jambo la kawaida.

"Kama ilivyokuwa katika sakata la ununuzi wa rada, ni vema Watanzania wakazingatia kuwa hatua ya pembe za ndovu za Tanzania kukamatwa na vyombo vya usalama vya Hong Kong, ni kielelezo cha kuwa waziri na serikali wameshindwa hata kusimamia na kulinda maliasili zetu na kuviachia vyombo vya usalama vya nchi nyingine vikitufanyia kazi hiyo. Hii ni aibu kubwa kwa serikali na CCM," alisema.

Alisema pembe za ndovu zilizokamatwa ni matokeo ya kuendelea kuwalinda watuhumiwa wakuu wa ujangili.

Alikumbusha kwamba katika Mkutano wa Bunge uliopita, Kambi ya Upinzani bungeni pamoja na maoni ya Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira iliwataja vinara wa ujangili.

Alisema inashangaza kuona kwamba, hadi sasa watu hao hawajakamatwa hali inayochochea vitendo hivyo, wizi na ufujaji wa rasilimali nyingine za taifa.

"Kati ya wanaohutuhumiwa kuwa majangili, baadhi yao wameteuliwa katika Nec na pia ni washauri wa mwenyekiti wao. Hii ni hatari haina haja niwatajie majina wanajulikana na nyie fanyeni uchunguzi wenu mtawajua," alisema.

Alisema hatua za msingi zinatakiwa kuchukuliwa ili kutokomeza suala hilo katika kulinda utalii wa nchi pamoja na kuongeza uchumi wa nchi kupitia sekta hiyo.

Alidai Baloshingwa anafadhili pia majangili wanaoua wanyama katika mapori ya akiba ya Ugalla, Rungwe, Moyowosi na Maswa.

Alisema inashangaza kwamba wafadhili na majangili wanafahamika kwa majina, lakini hawachukuliwi hatua na pindi wanapokamatwa hufunguliwa kesi rahisi zenye dhamana hivyo huachiwa kwa dhamana.

"Usalama wa tembo uko hatarini kutokana na serikali kutochukua hatua dhidi ya ujangili wa tembo pamoja na taarifa hizi kuwepo serikalini na viongozi wa CCM kushiriki katika ujangili," alisema.

Tuhuma za Msigwa zinakuja wakati ambao Waziri Kagasheki amekuwa akisafisha Idara ya Wanyamapori ikiwemo kuwasimamisha vigogo wa idara hiyo.

Katika tukio la karibuni, Balozi Kagasheki amewatimua kazi vigogo watatu wa wizara hiyo akiwamo Mkurugenzi wa Wanyamapori, baada ya kubainika kuhusika katika kashfa ya utoroshaji wanyamapori hai kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) kwenda nje.

Vigogo hao wamefukuzwa kazi baada ya tume iliyoundwa kuchunguza kadhia hiyo kufanya uchunguzi na kumaliza kazi yake.

Katika kashfa hiyo, vigogo hao wanadaiwa kuhusika na usafirishaji wa wanyamapori hai 116 na ndege 16 Novemba 24 mwaka 2010,  kwenda nje ya nchi kupitia Kia.

Pia alisema biashara ya mkaa na hususani unaotokana na uvunaji wa misitu ya Pwani inafanywa kwa mtandao wa vigogo wa Idara ya Misitu ambao wameweka vijana kwenye kambi kwenye misitu hiyo.

"Na leo halitapita lori la mkaa kabisa kwa sababu vigogo walioandaa ziara hii wanajua kamati ya Bunge inakuja, wanazuia magari yao...hii ni biashara inayofanyika kwa mtandao kutoka wizarani, ukikamata lori simu zinapigwa na wanatoka ofisini kuja kuliruhusu liondoke," alisema.

Awali, akitoa taarifa ya hali ya misitu hiyo, Meneja Msaidizi wa TFS, Kanda ya Mashariki, Bernadetha Kadala, alisema hali ya misitu hiyo ni mbaya kwa kuwa imevamiwa na kuvunwa na wafanyabiashara haramu wa mkaa, kuni, mbao, kurunge na nguzo.

Alisema misitu hiyo pia imevamiwa na watu kwa ajili ya makazi na kilimo, na malisho ya mifugo.

"Maeneo mengi ndani ya misitu ya Ruvu yana uwazi kutokana na uharibifu huu," alisema.

Hata hivyo, alisema kumekuwa na doria za mara kwa mara ambazo zimewezesha kukamatwa kwa mbao, mkaa, kuni, nguzo, magogo, magari, pikipiki na baiskeli za wahalifu.

Alisema katika kipindi cha mwaka 2012/13, doria zilizofanyika zimekamata malori matano, mkaa magunia 810, mbao 445, nguzo 150 na magogo 190.

Kilichojili Mkesha maalumu wa Vijana @ St.Columbus


Pastor Deo Lubala
Pastor  Freddie Kyara
Word Alive Praise Team wakihudumu usiku wa jana St Columbus







  Jessica Honore na Team nzima  ya Word Alive Praise Team
Rose Mushi akifuatilia kwa makini

Rose Mushi akifundisha


twende kazi....

Night of worship@CCC Upanga.


Night of Worship ni Event iliyokuwa ya namna yake katika Usiku wa jana ndani ya Kanisa la City Christian Center  (CCC) Upanga. Tamasha hilo lilikutanisha vikundi mbalimbali na watu kutoka maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es salaam katika kulitukuza na kuliinua Jina la Yesu.

The Nextleve Praise and Worship Team ,CCC Worship Team ,VCC, Glorious Celebration, John Lisu,Pastor Safari na John Kagaruki na wengine wengi walikuwepo kuhudumu usiku huo.

Glorious Celebration walikuwa wanafanya Live Recording ya Album yao chini ya Kampuni ya Hackneel Video Production katika usiku wa jana ambapo ilikuwa ya baraka sana.

Bupeh ni mwimbaji wa Gopsel Hip Hop kutokea Nchini Kenya aliyekuwepo kuhudumu usiku wa jana alikuwa akifanya Gopsel Hip Hop iliyotokea kuwa baraka kwa idadi kubwa ya watu,pia akatoa ushuhuda wa maisha yake ambao uliweza kugusa maisha ya wengi.

Watu walipata kumpokea Yesu kama Bwana na Mwokozi wa Maisha yao. Night of worship ni Ibada itakayo kuwa katika mwendelezo wa Ijumaa usiku ya Kila mwezi ndani ya Kanisa la CCC Upanga.
VCC Praise and Worship Team kwa stage.
John Lisu

Backup Team ya John Lisu
Sarah katikati na wezenzake wakisupport John Lisu Team
Ilikuwa fullshangwe mpaka asubuhi Watu walipata mda wa kutosha kusifu na kuabudu
Glorious Celebration wakirecord Live ndani ya CCC Upanda usiku wa jana.
Paul na wenzake wa Glorious Celebration wakikamua vocal kwa stage.
Flora Mbasha na Mmewe pia walikuwepo kuwakilisha usiku wa jana.

Paul kwa stage na Umenifanya Ibada


Bupe kutoka Kenya kwa stage akifanya Gospel Hip Hop
Abella na Paula ni wadau walikuwepo katika Event hiyo usiku wa jana.
Bupe na Catheline wakifanya collabo ya Gospel Hip Hop
Video Production Crew wakifanya Live recording ya Glorious Celebration usiku wa jana
Chini ya Hackneel Video Production. 
Audio Production Crew wakiwa kazini kurecord Album ya Glorious Celebration usiku wa jana

Viongozi wa Kikundi cha Jumuiya ya Uamsho wafikishwa mahakamani.

Gari la Polisi ambalo liliwachukuwa Viongozi wa Jumuiya ya Uamsho ambao walishitakiwa kwa makosa ya kufanya fujo na uchochezi likiwa linasindikizwa na magari ya Polisi kuja Mahakama ya Wilaya ya Mwanakwerekwe.
Kikosi cha kutuliza ghasia wakiwa wanaimarisha usalama katika eneo la Mahakama ya Wilaya Mwanakwerekwe ambapo Viongozi wa Jumuiya ya UAMSHO walipelekwa kwenda kusomewa mashitaka yao.


Kiongozi wa Jumuiya ya Uamsho Shekh Farid Hadi Ahmed akishuka kwenye gari la Polisi kuelekea Mahakama ya Mwanakwerekwe kwenda kusomewa mashtaka yao yanayomkabili ikiwemo kusababisha fujo na uchochezi.

Askari wa kikosi cha kutuliza ghasiawakiangalia usalama mahakani hapo.

Baadhi ya Wananchi walioenda Mahakamani hapo kwenda kushuhudia kesi inayowakabili Viongozi wa Jumuiya ya Uamsho ambao walikosa dhamana na kurudishwa Rumande.

Kilichojili katika Semina ya Binti na Ufahamu Bora.

Binti na Ufahamu Bora ni semina ya Mabinti inayofanyika kila mwaka katika Kanisa la Living Water Center Kawe,Semina hiyo iliyokuwa ya siku tatu kwa kuongozwa na Mama Lilian Ndegi,Pastor Naomi mhamba na Mwl Rose Mushi, Katika siku ya hitimisho la Semina hiyo siku ya Jumapili Ibada nzima mwanzo hadi mwisho Mabinti ndio walio hudumu.


Semina hiyo ilifunguliwa na Mtumishi wa Mungu Apostle Onesmo Ndegi wa Kanisa la Living Water Center akiwa kama mgeni rasmi,Akizungumza na Mabinti hao aliwaasa katika suala zima la kukimbilia kuwaza kuolewa baadala yake aliwaambia wawaze kuwa na ushirika na Mungu megine yatafuata kwa wakati wake.

Mwl Lilian Ndegi na Pastor Naomi ni wanenaji waliokuwa wazungumza katika semina hiyo ambao ndio wabeba maono ya Semina hiyo kuwa inafanyika kila mwaka Katika kuwaleta mabinti karibu na Mungu ilikuweza kuwaepusha na changamoto za ujana na Dunia kwa ujumla.

Mwl.Rose Mushi pia ni mzungumzaji aliyekwepo  kuzungumza na mabinti katika namna Binti anapaswa kuwa vipi na Jamii anayomzunguka itamtambuaje kwa jinsi alivyo,akaongeza kwa kuzungumzia kanuni za binti anapaswa kuwaje.

Mabinti walipata kujifunza vitu vingi ikiwemo kujitambua na maswala ya mahusiano na changamoto za kimaisha,Semina hiyo ilihitimishwa siku ya Jana Jumapili ikiambatana na Ngoma,Fashion Show amabyo ilidhaminiwa na Mstafa Hassanali,Magizo Dance na kupata muda wa Kusifu na Kuabudu ikiongozwa na Mwl.Rose Mushi.


Pasotr Naomi Mhamba akizungumza na Mabinti

Meza kuu  Katibu wa Living Water Center Ministry Peace Matovu,Mama Apostle Ndegi na Rose Mushi wakifuatilia kwa makini semina.

Mabinti walojitokeza kuuzulia semina hiyo wakifuatilia kwa amakini.

Praise and Worship Team ya mabinti wakihudumu katika Ibada
Edna Luvanda Kiongozi wa Mabinti Kanisani hapo ndio alikuwa MC siku ya hitimishi la semina hiyo.
Apostle Ndegi ndiye alikuwa Mgeni rasmi katika Semina hiyo.
Wanenaji wa semina hiyo wakifuatilia jambo kwa makini kwa mtumishi wa Mungu Apostle  Ndegi
Semina hiyo ilipambwa na michezo mbalimbali kama ngoma,maigizo,dance na Fashion show kama inavyoonekana.


Baadhi ya Mabinti walioshiriki Fashion Show katika Stage,Nguo walizovaa walidhaminiwa na mbunifu maarufu wa mitindo Nchini Mustafa Hassanali.











Magreth Kasanga Mwenyekiti wa mabinti ndiye aliyesimama madhabahuni katika kuhudumu upande wa Neno


Baadhi ya Viongozi wa Mabinti Edina Luvanda,Happiness Kassanga,Happiness Silayo, Grace Mbwiga Mkrugenzi wa Living Water Center katika Pozi.


Mwl. Rose Mushi ndiye aliye kuwa mzungumzaji wa mwisho kwa kutoa mafundisho yenye challange kwa mabinti wenzake kama kawaida yake!