On beahalf of Muhimbili University Fellowship of Evangelical Students(MUFES) I Welcome You to the extended fellowship in Muhimbili Main Campus this Friday 30th November, 2012 from 6:00pm,Minister-Apostle Onesmo Ndegi



Rais Kikwete aongoza Harambee ya Chuo Kuu cha St.John Dodoma.



Mkurugenzi mkuu wa PPF Bwana William Eriyo akikabidhi hundi ya shilingi milioni kumi kama mchango wa shirika lake kwa ajili ujenzi  ya Hosteli ya wanafunzi wenye ulemavu wa viungo na wasichana katika Chuo Kikuu cha St.John kilichopo mjini Dodoma, wakati wa harambee iliyofanyika katika ukumbi wa Diamond jubilee jijini Dar ea Salaam jana.

Katika Harambe hiyo jumla ya shilingi milioni 584/m zilikusanya ikiwa ni ahadi na fedha taslimu.Wapili kushoto ni Askofu mkuu wa Kanisa la Anglikana Dr.Valentino Mokiwa na kulia ni Mkuu wa chuo hicho askofu mkuu mstaafu Dr.Donald Mtetemela.

Uganda yalegeza na kuondoa adhabu ya Kifo kwa Mashoga.

Bunge la Uganda limeshindwa kupitisha sheria ya kuua watu wanaojihusisha na mapenzi ya jinsia moja (ushoga) kama ilivyoahidiwa na spika wa Bunge la nchi hiyo Rebecca Kadaga na badala yake bunge hilo limejikita katika kufanyia marekebisho muswada huo kwakutafuta tiba mbadala kabla ya kuisha kwa mwaka, ikiwa ni tofauti na spika huyo alipoongea na vyombo vya habari wiki mbili zilizopita alipoahidi kwamba sheria hiyo itapitishwa kabla ya kuisha kwa mwaka huu.

Lakini amerejea tena katika vyombo vya habari ijumaa iliyopita akisema kwamba hawatapitisha sheria hiyo kwasasa mpaka hapo baadaye akidai kwamba wametoa zawadi ya Christmas kwa mawaikili wa watu wanaojihusisha na vitendo vya kishoga akidai kwamba wamekuwa katika kampeni kwa muda mrefu ya kupinga sheria kali za serikali ya Uganda dhidi ya matendo ya ushoga.

Uganda ni kati ya nchi za kiafrika ambazo zina msimamo mkali juu ya watu wanaojihusisha na mapenzi ya jinsia moja, awali kwa upande wa bwana James Nsaba Buturo ambaye ni waziri mstaafu wa maadili wa serikali na kiongozi wa umoja wa maendeleo ya maadili nchini humo amesema hakuna maswali juu ya hilo anauhakika wa asilimia 99 kwamba muswada huo utapitishwa na kuwa sheria kamili.


Spika wa Bunge la Uganda Rebecca Kadaga


Source rumaafrica.blogspot.com

CPCT kuwasha moto Desemba

Baraza la Makanisa ya Kipentekost Tanzania (CPCT) nchini linatarajia kuwasha moto wa maombi ya kufunga mapema mwezi Desemba mosi hadi 23, 2012 ili Mungu akomeshe vurugu dhidi ya adui shetani ambaye hutumia watu kuharibu amani nchini.

Kauli hiyo ilitolewa na Mwenyekiti wa Baraza hilo,  Askofu David Batenzi wakati akiongea na chanzo kimoja cha habari kwenye semina ya viongozi wa ngazi ya maaskofu na makatibu wa makanisa ya kipentekosti Tanzania, iliyofanyika Dodoma, kwenye kanisa la  Phidelphia Gospel Assembly.

Askofu Batenzi, alisema imewalazimu kukimbilia magotini mwa Mungu kufanya maombi ya siku 23 ili kujiweka imara mbele za Bwana Yesu, ambaye wanaamini wakimlilia vita ya shetani dhidi ya kanisa itakoma kama ilivyokuwa nyakati za ukuta wa Yeriko.

Mtumishi huyo alisema, kutokana na ukosefu wa nidhamu alionao shetani na wafuasi wake, kikao kimeamua kwa pamoja Maaskofu wote kuwashirikisha waumini wote wa makanisa ya kipentekosti, ili maombi hayo yafanyike kwa ajili ya mahitaji watakayoyaomba.

Alisema kuwa katika siku hizo za maombi pamoja na kuombea amani na utulivu wa nchi, pia wataomba maombi ya kukomesha vurugu zinazofanywa dhidi ya wakristo, vinavyotendwa vya kuhatarisha amani.

Mbali na kuombea amani na ulinzi katika majengo ya ibada, pia wataomba kwa ajili ya viongozi wa serikali ili Mungu awape kusimamia haki ambayo hivi sasa imeingia dosari kutokana na baadhi ya waumini kuleta machafuko yasiyo na msingi ndani ya nchi hii ambayo Mungu amewabarikia watu wake.

Awali Askofu Batenzi aliongelea juu ya kusudi la semina hiyo, alisema ni kukumbushana kwa viongozi wa CPCT kuhusu changamoto wanazokutana nazo kwenye makanisa ya Kipentekosti, na jinsi watakavyokabiliana  pamoja na kuangalia maazimio kupitia katiba ya CPCT

Batenzi aliongeza kuwa, pamoja na hayo kikao hicho cha siku mbili ambacho kilikuwa na mada mbalimbali kutoka kwa watumishi wa Mungu, pia lengo lingine ilikuwa ni kunoana kiroho viongozi wenyewe kwa wenyewe na kuhimiza  waumini kuongeza kasi ya utendaji wa kiroho ambao utafanikisha kuwahubiria wanaovuruga amani.

Aidha alisema suala lingine lililoangaliwa kwa makini ni juu ya kuimarisha umoja wa makanisa, kuanzia watumishi hadi waumini na kupeana taarifa mbalimbali zitakazoweka wazi kama kuna tatizo lolote dhidi ya makanisa.

Hata hivyo,  Askofu huyo aliwakumbusha juu ya utekelezaji wa maazimio magumu, ambayo yamekuwa yakisuasua katika umoja wa Baraza la Maaskofu wa Kipentekosti Tanzania.

Mapema kabla ya kikao hicho ulifanyika uchaguzi wa baraza hilo mkoani Dodoma , ambapo Makamu Askofu wa TAG, Jimbo la Dodoma Mchungaji  Willbarforce  Mongi, alichaguliwa kuwa Mwenyekiti na nafasi ya makamu ilienda kwa Mchungaji Charles Kanyika.

Kwa upande wa Katibu wa Baraza hilo, Mkoa wa Dodoma alichanguliwa Mchungaji Baraka Kihoza ambapo wajumbe waliochaguliwa ni pamoja na Askofu Silvester Thadey, Askofu Julias Bundala na aliyekuwa Mwenyekiti wa kipindi cha nyuma Askofu Donard Mhango.

Men of Valor "When Men Praise" Conference.






Pastor Isaac Mallonga  Host and
R.I.O.T Visionary
Pastor Daniel Musokwa Tehillah Mbeya
Kenneth Oduor (Kenya)

When Men Praise
John Marco leading Worship




R.I.O.T   Dancers on stage

amazing dance
Leadership Interview
much focus




The Drive Season One ndani ya Kanisa la City Harvest Jijini Dar es Salaam.


Timu ya ‘THE City Shakers’ kutoka Kanisa la City Harvest la jijini Dar es Salaam, imeandaa tukio maalumu linalotengeneza picha halisi ya ‘safari’  ya maisha ya wanavyuo tangu wanapodahiliwa vyuoni hadi siku ya mahafali. Tukio hilo linajulikana kama  The Drive Season One, likibainisha changamoto zilizo mbele yao na mbinu za kuzishinda.

Akiongea na na chanzo cha blog hii, kuhusiana na Safari hiyo, Mwenyekiti wa timu ya maandalizi, Bw. Augustine Chavala, alisema kuwa wanavyuo wengi mara wanapodahiliwa chuo wanajikuta katika makundi  ambayo mwisho wa siku huzima ndoto za maisha yao.

“Wanavyuo wengi kabla ya kujiunga na vyuo vikuu huwa na njozi mbalimbali, lakini makundi wanayojiingiza kwayo hupotoa kabisa ufahamu wao na wakizinduka miaka mitatu imefika wanaondoka kama walivyoingia,” alisema na kuongeza:

“Makundi huharibu maisha ya wanafunzi wengi, huanza kwenda klabu, hufeli mitihani, wengine huishia kufukuzwa vyuo na kuambukizwa magonjwa yasiyotibika, tunatarajia kufanya safari hiyo kuwaasa na kuwapa mbinu za kujihami.”

Dhumuni lingine la safari hiyo, Mwenyekiti Chavala alibainisha kuwa ni kuonyesha upendo kwa wanavyuo hao na kuwadhihirishia kwamba ni wa muhimu sana mbele ya jamii inayowazunguka.

“Tunaomba wanafunzi wengi wajitokeze siku hiyo (Ijumaa ijayo tarehe 23) kuanzia saa tatu usiku, pale City Harvest, Mabibo Garage, karibu na Victoria Petrol Station,” alisema na kuongeza:

Usiku huo utapambwa na team nzima ya The City Shakers, World alive, ambapo wanavyuo watapata wasaa wa kucheza muziki kuona Sarakasi, maigizo, Vichekesho, filamu na vitu vingine vingi.

Fahari Ya Ujana


Makamba apotoa Biblia!

•    Ni kumlinganisha Kikwete  na  Yesu•    Wachungaji, maaskofu wamjia juu•    Alikuwa akijihami na kura za maruhani

Katibu Mkuu mstaafu wa chama cha Mapinduzi CCM, Luteni mstaafu Yusufu Makamba, siku chache zilizopita katika Mkutano Mkuu wa CCM uliofanyika mjini Dodoma alikaliliwa kutumia muda mwingi kutoa ufafanuzi wa vifungu vya Biblia kwa lengo la kumwombea kura Mwenyekiti wa CCM, Jakaya Kikwete huku akimfananisha mgombea huyo na Yesu Kristo, jambo ambalo limepingwa vikali na watumishi wa Mungu.

Katika mkutano Mkuu wa CCM, uliofanyika maeneo ya Kizota mjini Dodoma, Makamba alianza kwa kusema kuwa, ameshalemaa kwa kutumia vifungu vya Biblia, kila anapohutubia, licha ya kuzaliwa katika familia ya kiislamu, na kukulia katika uongozi wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT).    


Katibu Mkuu mstaafu wa CCM,  Yusufu Makamba
Makamba kabla ya kusema maneno hayo yaliyowaudhi baadhi ya wachungaji na maaskofu, alijihami kwa kuwaomba radhi masheikh, akidai kuwa lengo lake la kutumia Biblia jukwaani si kutangaza dini, bali anatumia vifungu vya Biblia kumwombea kura Kikwete ili aweze kuendelea kushika nafasi ya uenyekiti kwa kipindi kijacho.

Baadhi ya wale walioguswa na kauli nzito ya  Makamba, ya kumfananisha Rais Kikwete na Yesu ni; Askofu wa Kanisa la TAG, Zanzibar, Dickson Kaganga ambaye alikuwa na haya ya kusema:

“Luteni Makamba kwa kauli yake hiyo, mimi namuangalia kama mtu asiyejua maana ya Biblia na kuleta tafsiri mbaya katika ulimwengu wa kawaida,” alisema na kuongeza:

“Hata kama ni kumpigia kampeni, lakini mfano huo ni mkubwa sana hakutakiwa kuutumia katika mambo ya dunia.”

Naye Mtumishi mwingine wa Kanisa la EAGT, Geita, Mchungaji Obed Kyando, alisema, alichokifanya Makamba ni upuuzi ambao ni dhihaka na ni kufuru mbele za Mungu.

“Huwezi kumfananisha Yesu na Kikwete, ni kweli Mungu huchagua kiongozi au humtumia mtu yoyote, lakini hili ni kufuru,” alisema.

Mwenyekiti wa CPCT Dodoma, Wilberforce Mongi aliongea kwa njia ya simu kutoka mkoani humo, alisema Makamba si mtu anayejua Neno la Mungu, au mafundisho yake kwa usahihi, ingawa kwa maelezo yake anaeleza kuwahi kuwepo  KKKT.
“Mtu asiyemjua Kristo anaweza kusema lolote, najua hana analolijua kwa habari ya Yesu na Ukristo kwa ujumla,  hakuwa akieleza jambo la maana,” alisema.
Akizidi kuongea kwenye mkutano huo, Makamba alisema, anawakemea baadhi ya wanachama wa Chama Cha Mapinduzi ambao wamekuwa wakitumia muda mwingi kupanga mbinu ya kutaka kumpigia kura za maruhani Kikwete, jambo ambalo ni uendawazimu.

Makamba ambaye mara nyingi hurukia Biblia na kunukuu vifungu kadhaa wakati wa hotuba yake alinukuliwa akisema:
“Nasema wale wote ambao wanawaza kumpigia JK kura za maruhani washindwe kwa Jina la Yesu, mnampigia kura za maruhani ili iweje kuna watu hapa ambao kazi moja imewashinda, lakini wanataka Jakaya apunguziwe kazi ni kazi gani hiyo imemshinda……” alisema na kuongeza:

“Tena mtu huyo ambaye anasema tumpunguzie JK kazi hasemi tumpe nani, hapa kazi ni moja tu, kumtafuta Mwenyekiti na Mwenyekiti wetu ni Jakaya, hafanyi kazi kwa makusudi yake binafsi, bali anafanya kazi kwa makusudi ya Mungu.”

Alisema Jakaya anafananishwa na Yesu katika kitabu kitakatifu ndani ya Biblia, kwani Mungu wakati anataka kupeleka mkombozi duniani, alianza kuuliza amtume nani na Yesu akasema: “Niko hapa nitume mimi.”
Hata hivyo alisema, anawashangaa baadhi ya wanachama ndani ya CCM ambao kwa sasa wanafikiria juu ya Ikulu, na kuongeza kuwa; kura za urais zitapatikana kutoka ndani ya ukumbi wa mkutano mkuu, kama uliomalizika, jambo ambalo ni ukombozi kwa wana CCM na kwa taifa zima.

Alisema, wakati akifanya kazi alijikuta katika wakati mgumu kutokana na kuchukiwa na wanachama wengi kutokana na kufanya kazi katika mazingira ya kuwa muwazi na mkweli, hivyo kumtaka Jakaya Kikwete kuhakikisha anakuwa ngangari bila kuwa na hofu.
Makamba alisema katika kuongoza jahazi ndani ya CCM, Jakaya bado anafaa kushika nafasi hiyo ili kuongoza mashambulizi makubwa kwa wapinzani na wala hakuna sababu ya kuwepo kwa kura za maruhani.

Kura za Maruhani ni mfumo ulioanzishwa huko Zanzibar, na wanachama wa chama cha Wananchi CUF, waliokuwa wakishindana na wenzao wa CCM. Wakati mgombea waliyemtaka alipokosa nafasi ya kugombea kwa sababu fulani waliamua kuandika kura zao kuwa wamepigia maruhani. Hata hivyo maruhani ni mapepo au kwa lugha nyingine hujulikana kama mashetani.

Hata hivyo wachambuzi wa Biblia wanaelezea upotoaji wa kimaandiko alioutumia Makamba kwa kudhani kwamba aliyesema maneno hayo aliyotumia alikuwa ni Bwana Yesu, jambo ambalo ni potofu. Ukweli wenyewe ni kwamba, andiko hilo ambalo liko kwenye Isaya 6:8 likisomeka:

“Kisha nikasikia sauti ya Bwana, akisema, nimtume nani, naye ni nani atakayekwenda kwa ajili yetu? Ndipo nikasema, mimi hapa, nitume mimi.”

Kulingana na ushahidi wa kimaandiko, neno ‘Bwana’ katika mfumo huo linamaanisha  Yesu, hivyo isingewezekana ajiulize na kujituma mwenyewe. Hii inaonesha kuwa aliyekuwa akijibu ni Nabii Isaya na sio Yesu kama mpotoaji alivyosema.


Source :Jibu la Maisha

Dk. Malasusa awataka Viongozi wa dini kuwa mfano

Viongozi wa dini wametakiwa kuwa mfano katika maeneo wanayoyaongoza ili kuendelea kudumisha amani  kwa ajili ya ustawi wa nchi.
Rai hiyo ilitolewa  na Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Askofu Dk. Alex Malasusa, alipokuwa akihubiri katika  ibada ya kumweka wakfu, Askofu wa Dayosisi ya Dodoma, Amon Kinyunyu.

Dk. Malasusa alisema Serikali imetoa uhuru wa kuabudu hivyo viongozi wasiposimamia amani iliyopo watahatarisha uhuru uliopo wa kuabudu.

 “Kwa sasa hivi tunaona vurugu zinazosababisha kufyatuliwa kwa mabomu ya machozi, hatupendi kuona risasi za moto zinatumika kwa kuwa wakati huo itakuwa ni vigumu kupata muda wa kuabudu,” alisema.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dk. Rehema Nchimbi, ambaye aliiwakilisha serikali, alisema  viongozi wa dini wasibadilike, wahubiri amani na sio vurugu.

Dk. Rehema Nchimbi alisema serikali haina dini ila imetoa uhuru wa kila mwananchi kuabudu dini anayoitaka bila kuingiliwa uhuru wa mtu mwingine.

Aliwataka viongozi wa dini kumwogopa  Mungu aliyewaweka katika nafasi hizo na kuwasaidia katika kufanya mema.
Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Askofu Dk. Alex Malasusa      







Kwa upande wake, Askofu Kinyunyu aliwaomba waumuni wa Kanisa hilo kujikita katika kuendeleza mema yaliyoanzishwa na Askofu aliyemaliza muda wake, Festo Ngowo.

Alisema Askofu Ngowo alianzisha ujenzi wa ofisi za Dayosisi hiyo, ujenzi wa shule ya sekondari na miradi mingine mbalimbali ya Kanisa hilo.

Askofu Kinyunyu alichaguliwa kushika nafasi hiyo baada ya Askofu Ngowo kuugua kwa zaidi ya miaka miwili.

 Kwa mujibu wa taratibu za KKKT, inapotokea askofu akaugua zaidi ya muda huo, askofu mwingine huchaguliwa kuchukua nafasi hiyo.

Moto wa Mahakama ya Kadhi

Moto  wa kudai mahakama ya Kadhi inayogharamiwa na kusimamiwa na serikali umeibuka upya, lakini safari hii harakati zinafanyika msikitini na CD zimefyatuliwa na kuingizwa mitaani huku zikiwa na hotuba kali za wanazuoni na wanasiasa pia.

Miongoni mwa wanasiasa walioshiriki kwenye mkanda wa CD hiyo inayoitwa Waislamu Tujipange, ni Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi CUF Profesa Ibrahimu Haruna Lipumba, ambaye picha yake imewekwa kwenye jalada la juu ya CD hiyo.

Miongoni mwa hoja nzito za Prof. Lipumba, ni kuwa Mahakama ya kadhi isiyoendeshwa na kugharamiwa na serikali haiwezekani, kwa kuwa hicho ni chombo cha dola na hakiwezi kufanya hukumu kikiwa kinaendeshwa nje ya dola.

Akiwa ndani ya Msikiti wa Idrisa Kariakoo jijini Dar es Salaam siku chache zimepita, Profesa Lipumba alitolea mfano majimbo ya Kaskazini mwa Nigeria ambayo yalianza kuongozwa na sheria tangu yakiwa chini ya ukoloni wa Waingereza.
Profesa Ibrahimu Lipumba
Profesa Lipumba ambaye ni mchumi aliyewahi kuwa mshauri wa Rais kwa masuala ya uchumi, alionya kuwa ikiwa suala la mahakama hiyo litaachwa  mikononi mwa Waislamu wenyewe kama serikali inavyotaka linaweza kuangukia  mikononi mwa waislamu wenye siasa kali na siku moja wanaweza kudai hata dola ya kiislamu.

Kiongozi huyo wa kisiasa alieleza mshtuko wake aliposikia Rais Jakaya kikwete akisema kuwa Waislamu  wenyewe, jambo ambalo haliwezekani.

Katika mkanda huo Profesa Lipumba anaonekana akiwahamasisha Waislamu kujipanga ili kudai haki yao ya kutambuliwa kama rais wa daraja la  kwanza.

Mkanda huo umewashtua baadhi ya watu kutokana na ukweli kuwa, Profesa Lipumba ni kiongozi wa kisiasa anayepaswa kutetea watu wa dini zote, maneno “Waislam Tujipange” yanaweza kutafsiriwa kama kuelemea upande mmoja wa dini.

Alitumia nafasi hiyo kuzungumzia, historia ya Mahakama za Kadhi Tanzania, Kenya na Nigeria, huku akisisitiza kuwa, Waislamu wanapaswa kujipanga kutetea haki zao.

Katika CD, hiyo Sheikh Basaleh ambaye ndiye aliyemkaribisha Prof. Lipumba anasema kuwa, amemuita kiongozi  huyo kwa kuwa ni kiongozi na ni muislamu na hata  viongozi  wengine wa kisiasa wamekuwa wanaingia katika nyumba za ibada na kutoa hotuba.

“Nilipokuwa nikitangaza jana kuna mtu aliniuliza wewe Basaleh ulitutangazia kuwa atakuja Prof. Lipumba na utampa nafasi, yeye ni mwenyekiti wa CUF, je akija wa CCM utampa nafasi? nikasema yeye ametupa taarifa hata huyo wa CCM akitupa taarifa tutampa nafasi kwa kuwa kwanza huyo ndiye Rais wa nchi hii.  Karibu Profesa Lipumba…Rais mtarajiwa …karibu  uje uzungumze na  Waislamu katika nchi hii, lakini nakuomba uzungumzie hali ya kisiasa kuelekea uchaguzi wa 2015, karibu,” alisema Sheikh Basaleh.

Katika mkanda huo, Sheikh Said Ricco, anamalizia kwa kusema: “Mwaka 2010 kulifanyika juhudi kubwa sana kumsaidia bwana mkubwa vinginevyo asingekuwepo. Lakini mzee kapigwa wala hakumsaidia……Lipumba kasema nitakuja kuulizwa mimi wewe Lipumba nimekupa kisomo  umewasaidia nini Waislamu wenzio….hayo ni mashtaka sio mashtaka mbele za mwenyezi Mungu?”

Kisha anaendelea: “Atajibu hawa niliowaendea kwenye majukwaa ya kisiasa hawakunielewa nikawafuata hata misikini ndugu zangu hawa  walala hoi  hawakunielewa sasa tusichokielewa nini? Tutaenda kumjibu nini mwenyezi Mungu, kwa sababu kaja msikitini. Wewe unadhani ni mtu wa kutafuta kazi,  wanamtaka finland, china japani tena kwa pesa nyingi mno.

Ni kwa nini wewe unadhani anakuja msikitini anakuja kwa sababu anataka watanzania wenzie hasa sisi  tunaitwa walala hoi ambao ni Waislam. Ukiangalia huko mitaani wafagizi wote ni Waislamu , wakezetu ndio wanaotembea na mabeseni ya kuuza mihogo, jioni akirudi miguu  imepasuka akiingia kwenye neti ananasa.

Wanawake wa Kikristo hawafanyi hiyo biashara, sasa mimi nilichosimama hapa nakuombeni na sisi tuwe na majibu ya kumjibu Allah subiana uwataalah……….Imam ndani ya hotuba amezungumza wazi kwamba huu ni mwezi wa Rajab, mwezi Mtukufu mwezi ambao  hatutakiwi kudhulumu. Sasa je tuko tayari, tunamuahidi mwenyezi Mungu ndani ya mwezi wa Rajab, katika msikiti mkubwa wa Ali Jumaa, hatutabadilika tena kwenda kuwapigia kura wale; tuko tayari? mnaahidi mbele ya viongozi maana yeke hapa kuna Amir, sheikh Basaleh, maana yeye ndio kiongozi wetu. Je mnaahidi kuwa yeyote atakayebadilika mwenyezi Mungu amtie kansa ya damu?”

Tatizo lenu ni kupewa kapelo na fulana, kwanini mwanaume mwenzenu anakupa kapelo na fulana kwanini asikupe suruali………Ibrahimu yuko mbingu ya saba sasa wewe umkatae Ibrahimu wewe nani? ,” alimalizia sheikh huyo na kumkabidhi sheikh Basaleh ambaye alisema kazi ya mwaka 2015 imeshaanza na wasizubae wakapigwa bao la kisigino.

Kwa sasa Waislamu tayari wana mahakama ya Kadhi, na Kadhi Mkuu, lakini hagharamikiwi na serikali isipokuwa na waislamu wenyewe.

R.I.O.T. "Men of Valor(M.O.V)" - Men's conference. "When Men Praise”

Event Date:
Mon, 19/11/2012 - 5:30pm - Sun, 25/11/2012 - 8:30pm

Venue:National Museum Grouds, Opposite the IFM Institute, Dar Es Salaam

When Men Praise” : MEN OF VALOR (M.O.V) Conference.

Righteous Invasion of Truth (R.I.O.T) gladly brings ‘Men of Valor’, its first men’s conference in Dar es Salaam. M.O.V. is an interactive platform, reaching out to men across different ethnic groups, socio-economic and religious backgrounds to restore, transform, equip and edify the man holistically.

Men have a natural tendency of internalizing issues. When you ask a man what he is thinking when things are up to his neck, without a glance, he’ll instinctively say, “Nothing”. Men do cry, but their tears are only visible from the inside. That’s why God had to say, “It is not good for a man to be alone”. As much as studies show that women are twice as much susceptible to depression, surprisingly the male-to-female ratio for completed suicides is greater than 4:1

When in this state where the internalization of things has reached its limit, men tend to shift the blame for how they feel on the inside to outside things. We exhibit anger or irritability over everything. Men are more prone to using alcohol or drugs as an outlet. As if this isn’t enough, the male infant has a higher mortality rate than the female. Let alone the fact that the woman has a higher life expectancy rate.

To those that have overcome these obstacles, there is still no rest for them. The enemy has strategically planned to emasculate the ‘man’ figure from marriage, family and even the society at large. The ‘man’ as an authority figure is being undermined from his God-given position bestowed upon him from Genesis by God Himself.

How can men prevail this ongoing fierce battle? If only we could learn the greatest ‘Art of War’ –PRAISE! You might be the least in your father’s house or perhaps you are coming from the poorest family in your clan, but I clearly hear the Commander-in-Chief of the Army of The Lord saying this to you: “Jehovah is with you, Mighty Man of Valor”!

You can contact us by email  info@riotfoundation.org


Isaac Mallonga(Host)

The man behind R.I.O.T. and M.O.V. (Men of Valor), Isaac Mallonga, is passionate to live each day synchronized with the will of God. He is a graduate of East Africa School of Theology (EAST) in Nairobi, Kenya.
Born and raised in a Christian home, Isaac heard the call of God for a personal relationship with Him at a tender age. Isaac holds a degree in Bible Studies and Theology, two diplomas in IT and has work experience in the field. He is one of the lead pastors of Tehillah Friday in Dar es Salaam where he still ministers.
Although he doesn’t lead a regular Sunday morning congregation, Isaac is passionate about reaching out to the youth through unorthodox methods, beyond the four walls of a church building. He desires to coach men and women into the life God has intended them to live.
Bringing together other youth he has led a team of young leaders to preach the gospel through music and arts in high schools, colleges and also in small churches around Tanzania. Isaac is a musician and a worship leader and has served under several churches as a worship pastor. He has been in the youth ministry as a counselor and spiritual leader for over six years.
He has also spoken in several conferences including The Women of Virtue Annual Conferences (2010 and 2012), Tehillah Annual Conferences in Mbeya (2010 to 2012), and Occupy Till I Come Conference in Nairobi (June, 2012).


Kenneth Oduor (Kenya)



Kenneth Oduor is an Evangelist and a Pastor at Deliverance Church Umoja - part time. The Kenyan born has ministered in different countries around the East and Southern region, namely Kenya, Tanzania, Uganda, Zambia, Zimbabwe, Malawi and Botswana.
Minister Kenneth, who is currently based in Nairobi, has an education in Information Technology, Business Information Systems, Public Relations and Marketing. He has a working experience in machine operation, accounts and quality assurance. He is currently pursuing a Bachelor’s Degree in Biblical Studies.
Daniel Musokwa (Tanzania)


Daniel J. Musokwa was called into ministry while he was in Calgary Canada in March 2002. He returned to Tanzania in December 2004 to fulfil his calling into the Apostolic office. Prior to that Daniel was the Assistant Programme Coordinator for the Master of GIS degree programme and also an instructor for the Remote Sensing course at the Southern Alberta Institute of Technology (SAIT) in Calgary, Alberta, Canada.

Daniel and his wife, Irene have three daughters, Cherisse-Eleanor, Claire-Daisy and Chavelle-Dorothy. They live in Mbeya where Daniel ovesees the headquarters of New Testament Ministries.

Daniel and Irene look after the flock in Mbeya together where Irene is the Senior Pastor and the founder of Tehillah Ladies within the Tehillah network in Tanzania. Daniel also gives oversight to the Tehillah network in Tanzania. Soon he will be on the radio in major cities to propagate the message of God’s grace and love.



Carlos Kirimbai (Tanzania)

Usiku wa Tanzania Praise and Worship Team.

Ulikuwa ni usiku wa watofauti katika wa kusapoti maono Mungu aliyoyaweka kwa mtumishi wake Bwana Paul Mwangosi, Paul Mwangosi alipata maono ya umuhimu wa kumsifu na kumwabudu Mungu aliye hai mnamo mwaka 2008.Mwaka huo ikiwa mjini mwanza Mungu alisema naye  kuwa hajapata Heshima ya kutosha ile hali miungu isiyo hai ikiheshimiwa

Mnano mwaka 2011,Mungu aliachilia kibali cha kufanya mkesha kwa ajili ya kumsifu na kumwabudu.Mwaka huu ndipo Bwana Paul Mwangosi alipo washilikisha ndugu katika Kristo kuhusu maono haya ambao waliunda kamati ya kuandaa Mkesha wa Kumsifu na Kumwabudu Mungu aliye Hai.Kamati kwasasa ndio inayojulikana kama ya Tanzania Praise and Worship  Team,

Mkesha wa Kumsifu na Kumwabudu Mungu kwa mwaka jana katika Kanisa City Christian Centre Upanga (CCC).

Dhima ya ya Tanzania Praise and Worship  Team ni kutoa fursa kwa ajili ya watu wote kwa pamoja pasipo kujali tofauti za kidhehebu,kisiasa na kiuchumi Kumsifu na Kumwabudu Mungu kwa ajili ya Taifa la Tanzania.

Madhumuni ya Tanzania Praise and Worship  Team Kuandaa,kuhamasisha na Kuratibu Mkesha/Mikesha ya Kitaifa kwa kumsifu na Kumwabudu Mungu

Mkesha wa Kumsifu na Kumwabudu Mungu mwaka huu utafanyika tarehe 07/12/2012 katika Kanisa City Christian Centre Upanga (CCC)

Ilikufanikisha mkesha huu zinahitaika sh.Mill 18, Katika usiku wa Ibada ya jana zilipatatikana jumla ya sh.Millioni 4,642,000/ zilizopatikana tasirimu ni ash.mill 1,199,000/=


 Tanzania Praise and Worship Team madhabahuni wakihudumu katika usiku wa jana