TAMASHA kubwa la kwanza la kusifu na kuabudu kwa mwaka 2014 Lafana .

TAMASHA kubwa la kwanza la kusifu na kuabudu kwa mwaka 2014 Lafana .Tamasha hilo ambalo hufanyika kila jumapili ya mwisho mwezi lilifanyika jumapili iliyopita (26.01.2014) pale Dar es Salaam Pentecoste Church ( DPC) .
Lilijumuisha wasanii kadhaa wa nyimbo za injili akiwemo John Lisu na kwaya ya rivers of life ya DPC .

 Pata habari zaidi kwa njia ya picha .


Mc Boniface & Joyce M wa DPC : 
Picha kwa hisani ya  DPC na Worshipers family Tanzania




Sehemu ya kwaya ya Rivers of life wakiwa jukwaani .
Picha kwa hisani ya  DPC na Worshipers family Tanzania


Picha kwa hisani ya  DPC na Worshipers family Tanzania



  Picha kwa hisani ya  DPC na Worshipers family Tanzania



Picha kwa hisani ya  DPC na Worshipers family Tanzania


Imetayarishwa na Erasmus Augustine.

Askofu Polycarp Kardinali Pengo anahitaji maombi yako.

Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo
Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo (70) ni mgonjwa, imetangazwa.

Taarifa ya kuugua kwa Kardinali Pengo, kiongozi wa kiroho anayeaminika kwa kukosoa uovu unaofanywa kwenye jamii, imetangazwa na Askofu Msaidizi wa kanisa hilo jimboni humo, Mhashamu Titus Mdoe.

Mdoe, alitoa taarifa hiyo wakati wa misa takatifu iliyofanyika jana kwenye kigango cha Nzasa, parokia ya Temboni jimboni humo.

Misa hiyo ilikuwa mahususi kwa ajili ya ukaguzi wa maendeleo ya ujenzi na huduma za kiroho kwa kigango hicho kinachotarajiwa kupandishwa hadi ili kiwe parokia.

Mhashamu Mdoe hakutaja ugonjwa unamsumbua Kardinali Pengo, lakini aliwataka Wakatoliki na watu wenye mapenzi mema, kuendelea kumuombea ili apate nafuu.

Alisema ugonjwa wa Kardinali Pengo unaweza kuchangiwa pia na hali ya kuelekea katika uzee, ingawa sababu hiyo haijafikia kuwa chanzo kikuu cha kumfanya augue.Katika hatua nyingine, Askofu Mdoe alisema utumishi wa umma ulio bora unapaswa kuelekezwa katika kutatua umasikini na kero zinazoikabili jamii, hivyo kufikia tarajio la kuwa maisha bora.

Pia alikosoa tabia ya baadhi ya viongozi hususani watawala, kupiga picha zenye mwelekeo wa kushiriki na kutatua kero za jamii, huku lengo likiwa ni kupata nafasi kwenye vyombo vya habari.

Alisema miaka 52 ya Uhuru ilitosha kwa kutatua umasikini na kero nyingine zinazoikabili nchi.

Badala yake, alisema walio katika dhamana ya kufanikisha azma hiyo, wameshindwa kufikisha tumaini la maendeleo kwa wananchi hasa wa vijijini, licha ya ukweli kwamba maendeleo mijini yanakua kwa kasi.

Mhashamu Mdoe, alisema watu kama maafisa kilimo ambao damu zao zipo kwa kuwatumikia watu, hawapaswi kukaa maofisini wakiwa wamevaa suti, bali kuhakikisha wantekeleza wajibu wa kuwahudumia wakulima.

Alisema kuna maeneo mengi ya nchi yasiyofikiwa na mahitaji muhimu kwa jamii kama umeme, maji, afya na elimu bora, hivyo kuwafanya wasinufaike na matunda yanayotokana na Uhuru na rasilimali za nchi.
\
CHANZO: NIPASHE

Mwalimimu Lilian Ndegi akamia Kuukomboa Uzao wa Mwanamke



Mwalimimu Lilian Ndegi 

Wito umetolewa kwa Wanawake Wajawazito,Wakina Mama walio katika Malezi  pamoja na Mabinti kusoma kitabu cha MUNGU NA UZAO WANGU kilichoandikwa na MWL. LILIAN NDEGI wa Kanisa la Living Water Centre chini MTUME ONESMO NDEGI lililopo Kawe jijini Dar-es-salaam nchini Tanzania. 

 Akitoa wito huo katika uzinduzi wa kitabu hicho hivi karibuni, Mwalimu huyo wa Neno la Mungu Lilian Ndegi amesema kuwa, kitabu hicho ni msaada mkubwa kwa wakinamama wajawazito kwani watapata maarifa ya Ki-Mungu yatakayowasaidia kuwaondoa katika uharibifu wa mimba tangu inapotungwa,inapolelewa,pamoja na wakati wa kujifungua mtoto na kwamba hiyo inawahusu pia na mabinti ili kuwasaidia kuwa na uzazi mwema hapo baadae. 

 Akifafanua zaidi amesema Serikali ya Tanzania imeweka utaratibu mzuri wa kujenga vituo vya Afya kuwasaidia wakina mama wajawazito, Mila na Desturi nazo zina kanuni zao, lakini wakati umefika kwa Kanisa kujihoji Mungu anasema nini juu ya uzao wa Mwenye Haki  na kwamba litembee katika Kanuni zipi ili kuweza kupata ushindi mkubwa katika Uzazi. 

 Aidha  amesema kitabu hicho  kimebeba Ujumbe Wa Mungu wenye kusudi maalum juu ya maisha ya kiroho na kimwili, utakaofungua ufahamu wa watu na kuliona Pendo Kuu la Mungu juu ya maisha yao na Uzao wao maana Mungu anaanza kushughulika na uzao wa Mweye haki kizazi hata kizazi.

 Mwl. Lilian Ndegi ameongeza kuwa kama ambavyo ilikuwa kwa Ibrahim kupitia kitabu hicho cha MUNGU NA UZAO WANGU,Wazazi na Walezi kwa ujumla watajifunza mambo muhimu ambayo Mungu anawaagiza kufanya, kama sehemu ya wajibu wao  kwa mfano; Mume kumtunza mkewe siku zote ,kuwalea na kuwatunza watoto pamoja na kuziona athari za kinywa katika ulimwengu wa roho zinavyoweza kuathiri maisha ya uzao wao kutokana na kuwanenea maneno au kuwapa majina yasiyofaa kama vile kumwita Mtoto Mateso na nk.

 Kwa upande wake Mgeni Rasmi ambae ni Mkuu wa Makanisa ya  Living Water Center nchini Tanzania Mtume Onesmo Ndegi  Mume wa Lilian Ndegi,amewaasa Wanaume kuwa chachu ya mabadiliko katika ndoa zao, badala ya kujifanya wana misimamo isiyobadilika, na kuwataka kubadilika wao kwanza katika mitazamo yao juu ya wake zao na ndipo itakapo kuwa chachu za wake zao kubadilika kitabia na mienendo katika ndoa.

 Aidha ametoa wito kwa vijana wa kiume kuwa na Mungu zaidi katika ujana wao ili kumpata Mke Mwema atokae kwa Bwana atakaeweza kuwa msaidizi wa kweli katika maisha kiroho na kimwili huku akimshukuru Mungu kwa ajili ya Mke wake  Lilian alie mtaja kuwa wa Maana Sana katika maisha yake na  kwamba amefanyika baraka na msaada tosha katika Huduma yake na Familia kwa ujumla.

 Hata hivyo amewataka wanaume wote kuiga mfano huo wa kuwasifu wake zao na kuwashukuru pamoja na kuomba msamaha wanapokosea ili ndoa zao zijengwe katika misingi ya urafiki na penzi la kweli na sio ubabe kama ilivyo miongoni mwa wanajamii wengi.


Kitabu cha MUNGU NA UZAO WANGU kimezinduliwa Jumapili iliyopita ambapo pamoja na mambo mengine Mwl. Lilian Ndegi ameelezea kwa kina juu   ya Uzao wa Mwenye Haki,Nalikujua kabla ya Mimba Haijatungwa Tumboni mwa Mama Yako,Nafasi ya Mwanamume Wakati wa Ujauzito Mpaka Malezi,Magonjwa na Mateso Mengineyo Katika Kipindi cha Ujauzito,Mtazamo wa Wazazi juu ya Uzao Wao,Mtazamo wa Mungu juu ya Uzao wa Mwenye Haki,Mwanamke anahitaji ujasiri Mwingi wakati wa Kujifungua pamoja na uzazi wa Mpango ndizo sura 8 za kitabu hicho

                  Hiki ni kitabu cha pili kikitanguliwa na kitabu chake cha kwanza JE UNASAMEHE? Ambavyo vyote vinapatikana madukani jipatie nakala yako.
kwa jumla na rejareja simu nambari 0754465578 au 0655465578 barua pepe lilyonesmo@gmail.com web: www.lwc.or.tz.


 Story:Ritha Chuwalo
                          
Apostle Onesmo Ndegi


Living Waters walihudumu siku hiyo
Ilikuwa furaha sana kwa kwa upande wa akina mama siku hiyo
Watumishi wa Mungu mbalimbali wakitamka Neno na kukiweka wakfu kitabu hicho
Mzee Ernest Tarimo,Mmoja wa watu waliotoa mchango katika uandishi wa kitabu hicho akipokea bahasha ya shukrani siku hiyo
Mmoja wa watu waliotoa mchango katika uandishi wa kitabu hicho ni Dr kwa tahaluma akipokea bahasha ya shukrani siku hiyo

 Apostle Ndegi na Mke wake Lilian Ndegi  wakikata keki
Lilian Ndegi akimlisha keki mme wake Apostle Ndegi kumshukuru lakini pia  kumpongeza kwa kazi kubwa ya kumtia moyo katika kipindi cha uandishi wa kitabu cha MUNGU NA UZAO WANGU
Mtume Onesmo Ndegi akimlisha keki mke wake Lilian Ndegi kumshukuru lakini pia  kumpongeza kwa kazi kubwa ya uandishi wa kitabu cha MUNGU NA UZAO WANGU,sherehe za uzinduzi huo zilifanyika hivi karibuni katika kanisa lao Living Water Center Kawe jijini Dar-es-salaaNa hapa chini ndio picha ya keki yenyewe mfano wa kitabu hicho MUNGU NA UZAO WANGU kabla ya kukatwa.

Mtumishi wa Mungu Rose Mushi alikuwepo katika Uzinduzi huo akiwa ni mmoja wa watu waliohusika katika kitabu hicho kukamilika.
Ritha Chuwalo Mtangazaji wa Wapo Redio FM akilishwa keki baada ya kununua kitabu siku hiyo ya uzinduzi wa kitabu hicho cha MUNGU NA UZAO WANGU
Grace Kakiziba akilishwa keki baada ya kununua kitabu siku hiyo ya uzinduzi wa kitabu hicho cha MUNGU NA UZAO WANGU
Edna Luvanda Mke wa Antony Luvanda MC maarufu nchini akilishwa keki baada ya kununua kitabu siku hiyo ya uzinduzi wa kitabu hicho cha MUNGU NA UZAO WANGU
Hadson Kamoga akimmiminia Apostle Ndegi Champagne ikiwa ni katika kujipongeza baada ya kuzindua kitabu  cha MUNGU NA UZAO WANGU
 
Wamama wa Living Water Centre na Lilian Ndegi

Mwalimu wa Vijana mwandishi wa Vitabu Rose Mushi akiwa na Mwalimimu Lilian Ndegi
Watumishi wa Mungu kutoka huduma na Makanisa mbalimbali waliokuwepo kuhudhulia uzinduzi huo wa kitabu  cha MUNGU NA UZAO WANGU

Praise The Lord Concert @ CCC - The Favor Of The Lord


Islamic Extremists in Nigeria Attack Christians at Sunday Worship Every Week in January

JOS, Nigeria – Islamic extremists have attacked villages in three states in Nigeria every Sunday this month, killing at least 15 Christians.
Christian leaders in the Agatu Local Government Area of central Nigeria's Benue state said ethnic Fulani herdsmen were responsible for raids on two villages that left seven Christians dead on Sunday morning (Jan. 19), though a Fulani spokesman said the assailants must have come from elsewhere as there are no Fulani herdsmen known in the area.

The previous Sunday (Jan. 12) in northeastern Nigeria's Borno state, Christian leaders said terrorists from the Islamic extremist Boko Haram group attacked Sabon Gari village in the Gwoza Local Government Area, killing eight Christians. In Kaduna state the Sunday before that (Jan. 5), churchmen in the Manchok area mobilized in time to repel attacks by Fulani herdsmen, Christian leaders told Morning Star News.

The Rev. Yakubu Gandu Nkut of the ECWA in Zankan village, near Manchok.
In the Benue state attacks, Fulani herdsmen raided Oweto and Utuluewu villages at about 10 a.m., destroying homes and maiming and killing Christian residents, two Christian leaders said.

"They killed seven of our community members in Oweto and Utuluewu villages in Agatu, while many others were injured in the attack," John Ngbede told Morning Star News. "There was sporadic shooting in these two Christian communities in the early hours of Sunday, at about 10 a.m., when they were in their churches. This incident has forced Christian surviving residents of the two communities to flee their villages."
Ngbede said the names of the slain Christians were not immediately available.

"However, I am sure of the casualty figure of those killed by the Fulani herdsmen," he said. "Seven of them were killed in the attack."

Sule Audu, another Christian community leader in the area, told Morning Star News by phone that a relative, 60-year-old Isah Onum, was among the seven killed.
"I do not understand the rationale behind these incessant killing of our people and the destruction of their homes," Audu said.

Daniel Ezeala, police spokesman for the Benue State Command, confirmed that seven Christians were killed in Sunday's attacks in Agatu. Five soldiers were also killed in the course of intervening.
The state secretary of the Myetti Allah Cattle Breeders Association of Nigeria, Garus Gololo, reportedly said the assailants must have come from outside the area as he was not aware of any herdsmen in the Idoma-speaking areas of Agatu.

"I'm so sad over the killings in the area," he said. "I'm also told that the soldiers fell in the middle of the crossfire between the Agatu and Fulanis. The killers should be arrested and prosecuted."
In the attacks that killed eight Christians in Borno state, Boko Haram Islamists stormed Sabon Gari village in the Gwoza Local Government Area the night of Jan. 12, according to area Christian leader Peter Biye Gumte. The onslaught came after Boko Haram members destroyed a Church of the Brethren in Nigeria building in Bzuba village on Jan. 8.

Boko Haram insurgents last month attacked four predominantly Christian villages in the Gwoza, Damboa and askira-Uba Local Government Areas, leading to death of at least 26 Christians and destroying about 40 homes. The attacks in Bdagu, Izge, Hartsa and Yazza villages took place from Dec. 8 to Dec. 11.
In Plateau state, Fulani herdsmen in the Langtang North Local Government Area on Jan. 16 killed three Christians and wounded four others in Nwore and Yokdara villages, an area res

"The attackers were Fulani herdsmen, Muslims," Nanpon Miri told Morning Star News. "They attacked the two villages during the morning hours, at about 10 a.m."
Repelling the Fulani
In Kaduna state, the attempt by churchmen to defend themselves against armed Fulani herdsmen on Jan. 5 escalated into clashes in a cluster of villages, killing at least five of the assailants and leaving one Christian wounded.

Christian leaders in Manchok in the Kaura Local Government Area said they were thankful to God that Catholic parishioners leaving worship at about 11 a.m. caught sight of two vehicles full of invading ethnic Fulani gunmen – unknown to area Fulanis – in time for churchmen to mobilize to repel them. They said the Fulani herdsmen sought to kill Christians during Sunday worship.

"The gunmen shot indiscriminately at Christians who prevented them from gaining entrance into churches," the Rev. Yakubu Gandu Nkut of the Evangelical Church Winning All (ECWA) in Zankan village, near Manchok, told Morning Star News. "All churches in Manchok, Zankan, Sabon Gari, Fadan Attakar, Gizagwai, Zangang, and in surrounding villages were forced to end their worship services abruptly because of the early morning invasion by these Fulani gunmen."

The Fulani began shooting at crowds of Christians that had gathered to confront them by a church in the Sabon Gari area of Manchok, he said."A member of my church was shot by the gunmen and was injured," said Nkut, also chairman of the local chapter of the Christian Association of Nigeria.

Eyewitnesses told Morning Star News that some of the armed attackers were killed in the fracas as they attempt to gain access to churches in Manchok. Kumai Badu, chairman of the Kaura Local Government Council, said five people died in the thwarted attack on area churches but declined further comment.

"It is true that some gunmen were here to attack churches, and this led to a clash between some Christians and Fulani herdsmen, which led to the killing of five persons this morning," Badu said on Jan. 5. "There was a quick intervention from the military stationed here, and everywhere is calm."

A Fulani herdsman in Bungen village, near Manchok, 23-year-old Hashimu Pati, told Morning Star News that some Muslim Fulani gunmen unknown to area herdsmen came to Manchok and caused problems between them and Christians with whom they had been living peacefully.

"Yes, some Fulani armed gunmen were seen in Manchok town – they have brought problems between us and our Christian neighbors," Pati said. "I appeal to the government to help us by assisting to rebuild some of our houses destroyed in the aftermath of the aborted attack on churches."

Christian leaders said the incursion resulted in chaos and confusion in Manchok and all surrounding villages, and houses and vehicles were destroyed in clashes between assailants and Christians.Services at Baptist, Catholic, Church of Christ in Nations, Pentecostal and ECWA churches were cut short, Nkut said.

Bwayan Silas, a Catholic leader in Bungen village, near Manchok, said the raid stopped his worship.
"We were in the church here, the St. Peter's Catholic Church, when we heard sounds of gun shots," Silas said. "We all ran out of the church and found that some Fulani gunmen had invaded the town of Manchok and other communities around. Scared about what was happening as we saw gunmen rushing into our village, we all took to our heels in different directions."

A resident of Manchok said the gunmen left a note in the town threatening further attacks on Christian communities in the area since the Jan. 5 attack was thwarted."The Fulani gunmen yesterday [Jan. 8], dropped a letter in the town warning Christians to be prepared for a total war in the coming weeks," Solomon Musa told Morning Star News

Soul Breakfast Tour


Viongozi wa dini wataka gesi inufaishe Watanzania

Viongozi wa dini kutoka madhehebu mbalimbali nchini wameitaka serikali kuhakikisha kwamba rasilimali ya gesi asilia inawanufaisha kwanza wazawa kabla ya kupelekwa nje.

Maombi hayo kwa serikali yalitolewa na viongozi hao wa dini mbele ya Rais Jakaya Kikwete katika kongamano lao lililofanyika jana jijini Dar es Salaam kujadili matumizi ya rasilimali za madini, gesi na mafuta kwa ajili ya manufaa ya Watanzania na taifa kwa ujumla.

“Pamoja na serikali kufungua milango kwa wawekezaji lakini iweke kipaumbele cha kwanza kwa wawekezaji wazalendo ili waweze kunufaika na rasilimali za nchi yao kisha iwatazame wawekezaji wa nje,” alisema Sheikh Abubakar Zubeir, aliyewasilisha maombi hayo kwa serikali kwa niaba ya Baraza la Waislamu Tanzania (Bakwata).

Sheikh Zubeir aliongeza: “Pamoja na kuwa makini na mikataba inayowekwa iwe ni kwa maslahi zaidi kwa nchi na wananchi wake na kuwalinda na athari mbaya zinazoweza kusababishwa na uwekezaji usiozingatia taratibu, sheria na kanuni na kuisababishia nchi kuingia kwenye matatizo.”

Viongozi hao waliongeza kuwa serikali haipaswi kusema kuwa Watanzania hawana mtaji wa kuvuna rasilimali hizo ikiwamo gesi asilia kwani kwa kufanya hivyo kunatoa mwanya kwa mataifa ya kigeni kunufaika nazo badala ya wazalendo.

“Kusema Watanzania hawana mtaji wa kuvuna rasilimali hizi ni sawa na kufumbwa macho, na ni mtazamo potofu kwani wageni wanatumia udhaifu huo huo kwa ajili ya kuja kutawala rasilimali zetu kwa kusema kwamba wao wenyewe wamesema, hatuwezi kuvuna gesi kwa kuwa hatuna mtaji,” alisema Dk. Padri Charles Kitima, Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (Saut).

Aliitaka serikali kuwapa wazawa uhuru wa kutafakari na kupendekeza maamuzi juu ya manufaa ya rasilimali za nchi na kwamba umiliki wa rasilimali hizo ndiyo unaofanya nchi husika kusonga mbele kiuchumi badala ya kusema inakusanya kodi huku wageni wakiendelea kunufaika nazo.

Padri Kitima pia aliwataka viongozi wa dini waliohudhuria kongamano hilo kuwafunda viongozi wa serikali ili wabadilike na kuwa waadilifu katika matumizi sahihi ya rasilimali hizo.

Pia, waliwataka Watanzania kutokubali kutumiwa kuhujumu rasilimali za nchi na kwamba wanapaswa kuwa na moyo wa uzalendo kwa kutambua kuwa rasilimali yoyote inapopatikana katika maeneo yanayowazunguka siyo yao pekee, bali kwa wananchi wote ili kulinda maslahi ya utaifa.

Kadhalika, waliitaka serikali kuweka taratibu nzuri za kulinda rasilimali za nchi ili ziwanufaishe wote sambamba kuundwa kwa taasisi zenye uadilifu.

Vile vile, viongozi wa dini waliitaka serikali kuwa makini na baadhi ya wanasiasa na wanaharakati wanaotumia nafasi zao kuipotosha jamii na kuleta mafarakano na machafuko kwa ajili ya manufaa yao.

KAULI YA RAIS KIKWETE
Akizungumza kwenye kongamano hilo lililokusanya viongozi wa dini takribani 120 kutoka mikoa mbalimbali nchini, Rais Jakaya Kikwete alisema serikali itahakikisha sehemu kubwa ya gesi asilia itakakayovunwa inatosheleza kwanza mahitaji ya nchi kabla ya kuuzwa nje. Alisema haiwezekani gesi ikaanza kuuzwa nje ikiwa nchi bado haijanufaika vya kutosha kwa ajili ya maendeleo ya viwanda vikubwa.

Kuhusu ushiriki wa wazawa kwenye rasilimali za nchi, Rais Kikwete alifafanua kuwa, serikali haijaizuia kampuni yoyote, wala mtu au mbia yeyote kwenda katika ofisi za Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) kununua fomu ya kuomba kutafuta rasilimali hiyo.

Kwa mujibu wa Rais Kikwete, kinacholeta malumbano makubwa kuhusu gesi ni kwa kampuni husika kutaka kupewa upendeleo na kutengewa eneo maalumu kwani utafutaji wa rasilimali hiyo hadi kuipata ni kama mchezo wa kubahatisha.

Aliongeza kuwa, rasilimali za nchi zisipolindwa vizuri zitaleta maangamizi badala ya neema kwani kuna nchi nyingi duniani ambazo zimeendelea kuteseka na matumizi mabaya ya utajiri wa rasilimali hizo.

Akitolea mfano wa mitambo ya kisasa iliyojengwa baharini kwa ajili ya kutafuta gesi, alisema utafutaji wake una gharama kubwa kwani unahitaji kampuni kubwa zenye fedha zake ambazo ni zaidi ya maelfu ya bajeti ya serikali ya Tanzania.

Rais Kikwete pia aliliagiza TPDC kujiandaa kuchukua leseni kwa ajili ya kuanza utafutaji wa gesi kama kampuni zingine zinazojitegemea badala ya kusimamia tu na kutangaza tenda.

Aliongeza kuwa kwa sasa serikali inataka kulifanya jiji lote la Dar es Salaam kuanza kutumia nishati ya gesi lengo ni kuokoa mazingira pamoja na kupunguza ukataji wa miti ovyo kwa ajili ya kupata mkaa wa kupikia.

Alisema serikali inatarajia kupata umiliki wa gesi wa asilimia 65 hadi 70 kutoka kampuni za ndani wakati kwa kampuni za nje itapata umiliki wa asilimia 70 huku asilimia 30 ikienda kwa kampuni husika.

Waziri wa Nishati na Madini, Prof. Sospeter Muhongo, alisema, rasilimali ya gesi ndiyo itakayowatoaWatanzania katika wimbi la umaskini kwani shughuli za uvuvi wa samaki na biashara ambayo ilianza enzi za utumwa, lakini hazijaweza kuwaondoa wananchi kutoka katika wimbi hilo.

Jumuiya za dini zilizowakilishwa ni Bakwata, Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT), Jumuiya ya Makanisa ya Kipentekoste Tanzania (CPCT), Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) na Kanisa la Wasabato Tanzania (SDA).

Sorcce:Nipashe

Mahusiano yako na Mungu ni ya Muhimu zaidi kuliko Mahitaji yako Kujibiwa, naye na Mungu hutumia sana uhitaji wetu kuimalisha mahusiano yake nasi


Carlos Ricky Wilson Kirimbai
 Swala la mahusiano yako na Mungu ni la muhimu zaidi kwa Mungu kuliko swala la kujibu maombi yako kwa hiyo Mungu anapenda sana kama una uhitaji au changamoto, wewe mwenyewe uende mbele zake na hitaji lako kuliko kuwaambia wengine tu wakuombee. Ukienda mbele za Mungu na uhitaji wako itatoa fursa ya vitu viwili vikubwa kutokea.

1. Kuimarika kwa mahusiano yako na Mungu maana siku zote mazungumzo kati ya wawili huimarisha mahusiano kati yao.

2. Uhitaji wako kujibiwa na Mungu na hivyo kukufanya wewe kukua katika kumjua kwako Mungu.

Zaburi 103: 7

7Alimjulisha Musa njia zake,
Wana wa Israeli matendo yake.

Usiwe mtu tu wa kutamani kuyajua matendo ya Mungu uwe mtu anayetamani kuzijua na njia zake pia.

Wana wa Israeli waliyajua tu matendo ya Mungu maana kila wakipata changamoto walikuwa wanamfuata Musa. Utakuwa mpendwa anayejua tu matendo ya Mungu kama kila unapopata changamoto wewe ni mbio kwa mchungaji wako, au mtumishi fulani wa Mungu au watu wengine wao wakuombee.

Musa alijua njia za Mungu kwa sababu kila akipata changamoto alikuwa akienda kwa Mungu na hakuwa na mtu wa katikati wa kumwendea.

Tamani kuwa kama Musa na sio wana wa Israel.

Ayubu anatuambia kwenye Ayubu 22: 21.

21 Mjue sana Mungu, ili uwe na amani;
Ndivyo mema yatakavyokujia.

Ukimjua sana Mungu utakuwa na amani. Amani ni neno Shalom linalomaanisha hakuna kilichopungua na hakuna kilichovunjika. Ukimjua Mungu hakuna kitakachopungua na hakuna kitakachokuwa kimevunjika maishani mwako na mema yatakujia.

Kwanini usitamani kumjua Mungu ili uwe na amani na mema yakujie? Kwanini Mchungaji wako amjue Mungu zaidi kupitia changamoto zako wewe?

Daudi anatuambia kwenye Zaburi 34: 10.

10Wana-simba hutindikiwa, huona njaa;
Bali wamtafutao BWANA hawatahitaji kitu cho chote kilicho chema.

Tafuta kumjua Mungu. tafuta kumsogelea wewe na sio mwingine amsogelee kwa niaba yako.

Celebrating Dreamers Year 2014


Rais Kikwete afungua Kongamano la Viongozi wa Dini Kuhusu Matumizi ya rasilimali za Nchi, Gesi,Mafuta na Madini kwa Maendeleo ya Tanzania

Rais Kikwete akisalimiana na baadhi ya viongozi wa Dini siku ya jana alipo kuwa akiwasili katika Kongamano hilo White Sand Jijini Dar es salaam,Kongamano hilo la Viongozi wa Dini Kuhusu Matumizi ya rasilimali za Nchi, Gesi,Mafuta na Madini kwa Maendeleo ya Tanzania
Rais Kikwete katikati walipopiga picha ya pamoja na viongozi wa Dini siku ya jana baada ya Kongamano hilo la Viongozi wa Dini Kuhusu Matumizi ya rasilimali za Nchi, Gesi,Mafuta na Madini kwa Maendeleo ya Tanzania. White Sand Jijini Dar es salaam


HOTUBA YA MHESHIMIWA JAKAYA MRISHO KIKWETE, RAIS WA
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, WAKATI UFUNGUZI WA
KONGAMANO LA VIONGOZI WA DINI KUHUSU MATUMIZI YA
RASILIMALI ZETU ZA GESI ASILIA, MAFUTA NA MADINI  KWA
AMANI NA MAENDELEO YA TANZANIA, WHITESANDS HOTEL,
TAREHE 20-22 JANUARI 2014

Waheshimiwa Viongozi wa Dini;
Waheshimiwa Mawaziri;
Waheshimiwa Wakuu wa Mikoa;
Ndugu Makatibu Wakuu;
Wageni Waalikwa;
Mabibi na Mabwana;

Naomba nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu, mwingi wa rehema,
kwa kutujaalia uzima na kutuwezesha kukutana hapa siku ya leo kujadili matumizi
ya rasilimali zetu za gesi asilia, mafuta na madini kwa amani na maendeleo ya nchi
yetu.  Kwa  namna  ya pekee nawashukuru viongozi  wa  dini  kwa  kunishirikisha
kwenye  Kongamano  hili  muhimu  na  la  aina  yake.   Mmenipa  heshima  kubwa
ambayo sikuitegemea.  Asanteni sana.
Nawapongeza sana kwa uamuzi wenu wa busara wa kuandaa Kongamano
hili.   Mmedhihirisha kwa vitendo uhodari  wenu wa kutekeleza jukumu lenu la
msingi la kulea taifa letu kiroho na kushiriki kikamilifu katika masuala mengine
muhimu yahusuyo maendeleo na ustawi  wa Tanzania na watu wake.  Ninyi ni
wazalendo wa kweli.  Ni matumaini yangu na ya Serikali ninayoingoza kuwa ubia
wa aina hii utaimarishwa na kudumishwa kwa faida ya nchi yetu.
Najua mlianza kwa kukereketwa na athari  za matumizi  makubwa ya miti
kwa matumizi ya nishati jambo ambalo linachangia sana kuharibika kwa mazingira
duniani.  Mmeishia kwenye Kongamano hili.  Lina uwiano kabisa kwani tunakata
miti kwa ajili ya kuni na mkaa.  Tukitumia gesi itatoa huko.  Ni dhamira yetu hiyo.
Ndugu Viongozi wa Dini;
Kongamano  hili  linafanyika  katika  kipindi  mwafaka  kabisa,  kipindi
ambacho ugunduzi mkubwa wa gesi tayari umefanyika na dalili za kugunduliwa
zaidi zipo.  Kipindi ambacho hazina ya madini mbalimbali inazidi kugunduliwa na
makampuni ya utafiti yanatupa moyo kuwa mambo huenda yakawa mazuri zaidi.
Pia,  ni  kipindi  ambacho  rasilimali  zetu za  wanyamapori  na  misitu  zinatishiwa
kutoweka.  Ni kipindi ambacho wakulima na wafugaji na wafugaji na wahifadhi
wa misitu na wanyamapori wanashindania ardhi ya kufanyia shughuli zao. 

 Sasa
hivi ni kipindi mwafaka kabisa kukaa chini na kutafakari jinsi gani rasilimali hizi
zinaweza kulindwa na kutumika kwa manufaa ya nchi yetu na watu wake wote
zikiwanufaisha kule ambako rasilimali hizo zipo na hata kule ambako hazipo.    
Ni ukweli usiopingika kuwa Mwenyezi Mungu ameijalia nchi yenye utajiri
mkubwa wa rasilimali za asili.  Ametujaalia ardhi kubwa yenye rutuba, madini ya
aina mbalimbali,  misitu na mbuga za wanyama wa kila aina, hali ya hewa nzuri,
bahari, maziwa makubwa, mito mingi, watu wengi na kadhalika.  Rasilimali hizi,
kwa  tabia  yake,  inatakiwa  zitumiwe  vizuri  ili  kuboresha  hali  na  maisha  ya
Watanzania wote sawia na kwa miaka mingi na hata milele.  Vinginevyo rasilimali
hizi  zinaweza  kugeuka  kuwa  chanzo  cha  mifarakano,  magomvi  na  mauaji.
Zinaweza kuwa balaa na kuleta maangamizi  nchini  badala  ya kuwa baraka na
neema.
Mifano ipo ya nchi mbalimbali  duniani zilizojikuta zina migogoro na vita
vya wenyewe kwa wenyewe kutokana na kugombania utajiri wao wa rasilimali za
asili.    Watu wa nchi hizo wanajuta kuwa na rasilimali ambazo zimekuwa chanzo
cha kuhatarisha amani,  utulivu, usalama na hata uhai wao.  Kwa hapa Tanzania
tunashukuru Mungu rasilimali hazijageuka kuwa balaa na tunaomba hilo lisitokee.
Tangu  Tanganyika  ipate  uhuru  na  Zanzibar  kufanya  Mapinduzi  Matukufu  na
hatimaye nchi zetu mbili kuungana  na kuwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
Serikali  za  awamu  zote  zimesimamia  kwa  makini  rasilimali  za  nchi  yetu  ili
ziwanufaishe Watanzania wote.  Tumetunga sheria na sera mbalimbali kuhakikisha
kuwa lengo letu hilo linatimia. 
Hata  hivyo,  usimamizi  wa sheria  hizo na utekelezaji  wa  sera  zetu nzuri
umekuwa  unakabiliwa  na  changamoto  mbalimbali  kwa  nyakati  mbalimbali.
Mpaka hapa tulipofika ni umahiri wa viongozi wetu ndiyo uliotuwezesha kuzuia
mambo yasiharibike na kugeuka kuwa matatizo makubwa.   Tumefanikiwa kiasi
chake ingawaje hatujaweza kuzuia kabisa matatizo yasitokee hapa na pale.  Taarifa
za kugombea rasilimali  zimekuwa zinasikika na nyingine zikiwa zimesababisha
watu kupoteza maisha, kujeruhiwa na mali kuharibiwa.  Tutafanya nini kukomesha
hali hiyo isijitokeze, ni jambo ambalo sisi kama taifa, yaani Serikali, wananchi na
wadau mbalimbali,  wakiwemo viongozi wa dini  hatuna, budi kulizungumza na
kulipatia ufumbuzi.


Ndugu Viongozi wa Dini;
Nimefarijika sana na uamuzi wenu wa kufanya mkutano huu kuzungumzia
rasilimali  ya mafuta na gesi.   Juhudi za kutafuta mafuta na gesi  imeanza tangu
ukoloni, zikaendelea katika awamu zote baada ya Uhuru. Shirika la Maendeleo ya
Petroli  (TPDC)  lilianzishwa  mwaka  1969 kuongoza juhudi  hizo na kusimamia
sekta ya mafuta nchini kwa manufaa ya Watanzania wote.  Hatujajaaliwa kupata
mafuta mpaka sasa lakini tumefanikiwa kupata gesi.  Ugunduzi wa kwanza wa gesi
asilia ulifanyika Songosongo mwaka 1971 na baadae Msimbati,  Mtwara mwaka
1982.  Utafutaji na ugunduzi huo uligharimiwa na Serikali yetu na hivyo gesi hiyo
ni mali ya Serikali.  Baada ya ugunduzi huo makampuni binafsi yalipata shauku ya
kutafuta mafuta na gesi nchini.
Mwaka 1980 ikatungwa Sheria ya Utafutaji wa Uzalishaji wa Mafuta kwa
nia ya kuweka masharti na utaratibu wa makampuni kushiriki katika utafutaji na
uzalishaji  wa mafuta na gesi  nchini.   Pia unatoa mwongozo wa mgawanyo wa
mapato  baina  ya  makampuni  na  Serikali.   Sheria  hiyo  imeendelea  kufanyiwa
maboresho  kwa  nyakati  mbalimbali  kulingana  na  mahitaji  ya  wakati  husika.
Kuanzia mwaka 2007 shughuli za utafutaji wa mafuta na gesi asilia ziliongezeka
kwa  nguvu  na  kasi  kubwa.   Juhudi  hizo  zilizaa  matunda  mwaka  2010  kwa
uvumbuzi  wa  kwanza  wa  gesi  katika  Bahari  Kuu uliofanywa  na  Kampuni  za
Orphir na British Gas.  Baada ya hapo ugunduzi umeendelea hadi kufikia futi za
ujazo trilioni 46.5 za rasilimali ya gesi nchini mpaka sasa.  Utafiti unaendelea na
matumaini ya kupata gesi  zaidi yapo.  Kufuatia ugunduzi huo, Tanzania sasa ni
moja ya nchi zimazohesabiwa kuwa na gesi nyingi duniani na ni nchi inayovutia
wawekezaji  wengi katika sekta ya gesi.   Kwa sababu hiyo, tukaamua kuifanyia
mapitio  Sheria  ya  Utafutaji  na  Uzalishaji  wa  Mafuta  na  Gesi.   Mwaka  2013
tumetunga  Sera  ya  Gesi  na  kurekebisha  masharti  ya  Mkataba  wa  Kugawana
Mapato yatokanayo na gesi  (Production Sharing Agreement)  na kuongeza mgao
wa Serikali.


Ndugu Viongozi wa Dini;
Sera  ya  Gesi  Asilia  iliyopitishwa  mwezi  Oktoba,  mwaka  jana  (2013)
imeeleza  wazi,  tena  kwa  lugha  nyepesi,  kuwa  gesi  ya  Tanzania  ni  mali  ya
Watanzania wote na itatumika kwa manufaa ya Watanzania wote – wa kizazi hiki
na kijacho.  Katika matumizi  ya gesi,  kipaumbele kitakuwa matumizi  ya ndani.
Msingi wa hoja yetu ni ule ukweli kwamba ukiuza nje gesi yote,  unapata mapato
peke yake lakini unakosa faida nyinginezo.  Ukiitumia ndani unapata mapato na
faida nyingine nyingi, kwa mfano, uzalishaji wa umeme, matumizi ya majumbani,
kwenye  magari  na  viwandani  kuzalisha  bidhaa  mbalimbali.  Hivyo  basi
mnapoitumia ndani gesi inakuwa kichocheo kikubwa cha maendeleo ya nchi yetu. 
Vilevile  tupo katika  mchakato  wa  kuandaa  sera  ya  kuwashirikisha  zaidi
Watanzania (Local Content Policy) ili wanufaike zaidi na rasilimali  yao ya gesi.
Kwa  sasa  nimewaagiza  TPDC  wajiandae  kushiriki  katika  utafutaji  wa  gesi,
uzalishaji  wake  mpaka  inapofika  sokoni.   Wasiwe  wagawaji  vitalu  tu  pekee.
Katika  sera  hiyo  mpya  pia  tunaangalia  shughuli  zinazoweza  kufanywa  na
Watanzania ili  tuone njia bora ya kuwawezesha kushiriki.   Kwa sasa tunadhani
wanaweza  kushiriki  kwa  urahisi  katika  utoaji  wa  huduma  kwa  kampuni
zinazofanya  utafiti  na  uzalishaji  wa  gesi  na  mafuta.   Wapo  walioanza  na
wanafaidika.  Nia yetu ni kuona idadi yao inaongezeka.


Mabibi na Mabwana;
Tumeanza  pia  mchakato  wa  kuiboresha  TPDC ishiriki  katika  uwekezaji
kwenye sekta ya mafuta na gesi kwa niaba ya Watanzania.    Katika utaratibu huo,
baadaye TPDC itauza hisa zake kwenye Soko la Mitaji ili Watanzania washiriki
moja ka moja katika kumiliki rasilimali hii muhimu.
Ndugu Viongozi wa Dini;
Mambo yote hayo yanafanyika ili kuhakikisha masilahi ya taifa yanalindwa
na  Watanzania  wote  wananufaika  na  rasilimali  zao  kwa  usawa.   Changamoto
kubwa tunayoiona kuhusu ushiriki wa Watanzania kwenye utafutaji na uzalishaji
wa mafuta na gesi  ni uwezo mdogo wa fedha, utaalamu na teknolojia tulionao.
Fedha zinazohitajika kwenye shughuli ya utafutaji mafuta na gesi, kwa mfano, ni
nyingi mno na Watanzania wenzetu hawanazo na hakuna uhakika wa benki iliyo
tayari kumkopesha mtu asiyekuwa nacho. 
Namna  nyingine  ni  kuwapa  maeneo  ili  wao  watafute  wabia  wawekeze.
Lakini,  mnapokuwa  mnasheria  inayoshirikisha  ubia  baina  ya  Serikali  na
mwekezaji,  kuamua kuacha Serikali  ili  badala yake apewe Mtanzania binafsi  si
uamuzi rahisi sana kuufanya.  Mtu binafsi ananufaika mwenyewe wakati Serikali
inanufaisha wengi.  Ninachokiona nafuu kufanya ni kutumia mwanya wa ushiriki
wa TPDC ili tuone baadhi ya hisa ziuzwe kwa Watanzania.  Hapa kunakuwa na
ubia wa TPDC na wananchi upande mmoja na Serikali upande mwingine.
Jambo  lingine  tunalolifanya  ni  kuhakikisha  kuwa  rasilimali  ya  gesi
inatumika vizuri, kwa manufaa ya kizazi cha sasa na vizazo vijavyo.  Tutaanzisha
mfuko maalum wa kuhifadhi mapato ya gesi na kuwekewa masharti ya matumizi
yake.  Tutatunga sheria maalum kwa ajili hiyo na tutafanya hivyo kwaka huu.


Mabibi na Mabwaba;
Kwa  upande wa  rasilimali  ya madini  mabadiliko makubwa  ya kiuchumi
yaliyoanza miaka 1980 katikati, Serikali ilijitoa katika uwekezaji na ikabaki kuwa
mhamasishaji  na  kuweka  mazingira  mazuri  ya  uwekezaji.   Kufuatia  hali  hiyo
wawekezaji wengi walianza kuja kuwekeza katika maeneo mbalimbali pamoja na
utafutaji na uchimbaji wa madini.  Serikali ikaweka Sera (1997) na Sheria (1998)
ya madini kusimamia sekta hiyo.  Ni kweli mapato ya Serikali na fedha za kigeni
ziliongezeka kutokana na uzalishaji wa madini.  Lakini palikuwa na manung’uniko
mengi kutoka kwa wananchi kuwa hawafaidiki sana na rasilimali zao.
Kamati  mbalimbali  ziliundwa  kuangalia  tatizo lipo wapi  ili  jawabu lake
litafutwe.   Nilipochaguliwa  kuwa  Rais  wa  nchi  yetu   mwaka  2005  niliyakuta
manung’uniko hayo na kuamua tuyatafutie jawabu.  Mwaka 2006 nikaunda Kamati
ya  Jaji  Bomani  ili  ichambuwe  mapungufu  yaliyopo na kutoa mapendekezo  ya
hatua za kuchukua.  Matokeo ya taarifa ya Kamati  ile ni Sera Mpya ya Madini
(2009) na Sheria Mpya ya Madini (2010).  Sera  na Sheria hii inalenga kuongeza
faida zaidi kwa Serikali na jamii, bila kuwasahau wale wanaozunguka migodi.
Faida  hizo  ni  pamoja  na  kuhimiza  kampuni  za  uchimbaji  wa  madini
kufungamanisha uchumi kati ya sekta ya madini na nyingine.  Vilevile tumewataka
waongeze nafasi ya ajira kwa Watanzania na ununuzi wa huduma na bidhaa nchini.
Aidha,  tumeamua  Serikali  iwe  inapata  hisa  katika  migodi  mikubwa
itakayoanzishwa siku za usoni.   Ndiyo maana tunaendelea kufanya mazungumzo
na kampuni  zitazochimba  uranium na  nickel.   Hatujamaliza  lakini  tunakwenda
vizuri.
Halikadhalika, Sheria na Sera vimeweka mkazo wa kuendeleza wachimbaji
wadogo  ambao  ni  Watanzania  tu.   Katika  kutekeleza  hilo,  tumeanza  kutenga
maeneo kwa ajili yao.  Changamoto kubwa inayowakabili  ni ukosefu wa mitaji,
vifaa na utaalamu.  Kuhusu fedha, tumeanzisha mfuko wa kuwasaidia na mwaka
huu wa fedha tumewatengea jumla ya shilingi bilioni 2.5.  Vile vile tunakamilisha
taratibu za kuanza kuwakodisha vifaa kupitia ofisi zetu za madini za Kanda.
Jambo lingine kubwa ambalo tunajiandaa kulifanya ili kunufaisha wananchi
na  nchi  yetu  ni  kutunga  Sheria  itakayohakikisha  kuwa  madini  mengi
yanayochimbwa  nchini  yanaongezewa  thamani  hapahapa  nchini.   Hatua  hii
itachangia sana kuongeza mapato na fursa ya ajira kwa watu wetu.


Nduvu Viongozi wa Dini;
Nimeyasema  haya  yote  kuwaonesha  kuwa  Serikali  haina  mchezo  katika
usimamizi wa rasilimali zetu za asili.  Tunafanya hayo kwa vile tunafahamu kuwa
zinaweza kutuletea maendeleo ya haraka.  Lakini pia zinaweza kusababisha nchi
yetu kuingia kwenye dimbwi la migogoro inayotokana na rasilimali.  Yote mawili
yanaweza kutokea kutegemea tutasimamiaje na kuzitumiaje rasilimali zetu.
Jambo  la  muhimu  ni  kusaidiana kuelimisha  jamii  ya  Watanzania  namna
tulivyojipanga  kusimamia  rasilimali  zetu  za  gesi  asilia,  mafuta  na  madini.
Waelewe  kuwa  utajiri  huu  ni  mali  yao  na  hivyo  ni  haki  yao  kunufaika  nao.
Wafahamu kuwa ni wajibu wao kulinda na kuzitunza rasilimali hizo ili zisipotee.
Ninyi mnayo dhamana ya kuelimisha jamii  waelewe nia hiyo njema ya Serikali.
Pia napenda kusema kuwa siyo kweli kwamba Serikali haijali rasilimali za nchi au
haitaki Watanzania wafaidike nazo; siyo kweli eti Serikali inapendelea wawekezaji
wageni kuliko wazawa na hakuna mkoa au eneo linapuuzwa au kubaguliwa.  Mimi
na  Serikali  ninayoiongoza  tutakua  watu  wa  mwisho  kupuuza  wazawa  na
kupendelea wageni au kupuuza watu wa maeneo ambako rasilimali  zinapatikana
au hazijapatikana.


Ndugu Viongozi wa Dini;
Naomba muendelee kutekeleza jukumu lenu la msingi la kulea taifa kiroho.
Mhimize waumini wenu wawe waadilifu na wazalendo.  Waache kujihusisha na
vitendo viovu vya wizi,  ubadhilifu,  matumizi  mabaya ya madaraka na rushwa.
Mkifanikiwa hilo, rasilimali zetu zitakuwa salama.  Vile vile muendelee kuhubiri
upendo miongoni mwenu, miongoni mwa waumini wenu na miongoni mwa watu
wote.  Watu wakumbushwe kuwa sisi wote ni viumbe wa Mungu na mbele yake
sisi  wote  ni  ndugu na  inabidi  kuheshimiana  na  kuvumiliana  kwa  tofauti  zetu.
Tukifaulu kwenye hili nchi yetu itabaki salama daima milele.
Nafahamu  kuwa  wapo  baadhi  ya  watu  ambao  wanafanya  vitendo  vya
kuhujumu rasilimali  zetu.  Wapo wanaoingia mikataba isiyozingatia maslahi ya
taifa  katika  uvunaji  wa  rasilimali  zetu.   Wapo wengine  wanaokula  njama  na
wawekezaji  ili  Serikali  ipunjwe mapato yake.  Watu wa aina hiyo wapo katika
jamii  ye yote ile na sisi  kuwa nao si ajabu.    Napenda mfahamu kuwa Serikali
inapinga vitendo vya aina yoyote vya kuhujumu rasilimali  zetu.  Ndiyo maana
watu  wa  aina  hiyo  wanapobainika,  wanachukuliwa  hatua  na  vyombo
vinavyohusika.  Ninyi pia msichoke kuwafichua, wapo miongoni mwa waumini
wenu.


Mabibi na Mabwana;
Kabla  ya  kumaliza,  napenda  kumshukuru Waziri  wa  Nishati  na  Madini,
Profesa Sospiter Muhongo na timu yake Wizarani kwa kushirikiana na viongozi
wa dini katika jambo hili  muhimu.   Naamini hatua hii  ya kuwapa taarifa sahihi
viongozi  wa  dini  kuhusu  matumizi  ya  rasilimali  zetu  hususan  gesi  na  madini
itasaidia  kuongeza  uelewa  wa  waumini  wenu  na  wananchi  kwa  jumla.
Watafahamu fursa zilizopo na jinsi ya kuzitumia ili wafaidike nazo.  Nakushukuru
pia kwa kusimamia vizuri utekelezaji wa sera na mipango ya Serikali katika sekta
ya nishati na madini.  Kazi yenu nzuri inaonekana na sisi wote ni mashahidi.
Mwisho,  nawashukuru  viongozi  wa  dini  kwa  kunishirikisha  kwenye
Kongamano lenu.  Naamini mkitoka hapa mtakuwa mabalozi wazuri wa kueneza
ujumbe kuwa rasilimali za Watanzania zipo kwenye mikono salama. Baada  ya
kusema hayo, napenda kutamka kuwa Kongamano la Viongozi wa Dini kujadili
matumizi  ya  rasilimali  zetu  za  gesi  asilia,  mafuta  na  madini  kwa  amani  na
maendeleo ya nchi yetu limefunguliwa rasmi.  Nawatakia kila la heri na mafanikio
katika mwaka huu wa 2014. 
Asanteni sana kwa kunisikiliza.