Living Water Centre Kawe Katika Uzinduzi wa Logo na Bango Jipya 2014





Kiongozi wa Kanisa la Living Water Centre Apostle Onesmo Ndegi

Living Waters Praisse team wakiongoza sifa wakati wa Ibada
Wapiga vyombo vya mziki wa Living Waters Praisse

Bango lenye logo na ujumbe mpya kwa ajili ya mwaka huu 2014

Kutemeba Katika Mapenzi na Kusudi la Mungu kwa ajili yako Kutakuletea tija Sana mwaka huu 2014.

Pastor Carlos Kirimbai Manna Tabernacle Bible Church

Mna hila nyingi moyoni mwa mtu; Lakini shauri la BWANA ndilo litakalosimama. (MIT. 19:21 SUV).

Tafsiri ya Bibilia ya Habari Njema inasema:

Kichwani mwa mtu mna mipango mingi, lakini anachokusudia Mwenyezi-Mungu ndicho kitakachofanyika. (Methali 19:21 BHN).

Tafsiri ya Neno inasema:

Kuna mipango mingi ndani ya moyo wa mtu, lakini kusudi la BWANA ndilo litakalosimama.

Tukijumuisha yale yasemwayo katika tafsiri zote hizi tatu tunaweza kutoa muhtasari kwa kusema,

Japokuwa tunapanga mipango mingi ni ile iliyo sawa na kusudi la Bwana kwa ajili yetu ndiyo itakayo simama.

Sasa kama ni kusudi la Bwana ndilo litakalo simama, kwanini tupoteze muda kupanga mipango ambayo hatuna uhakika ni kusudi la Bwana au la kwa ajili yetu? Kwanini kusiwe na namna ya kujua kusudi la Mungu kwa ajili yetu ili tunapopanga mipango yetu tuipange kwa kuzingatia kusudi la Bwana kwa ajili yetu?

Tena maandiko yanaendelea kusema sehemu nyingine:

Maana tu kazi yake, tuliumbwa katika Kristo Yesu, tutende matendo mema, ambayo tokea awali Mungu aliyatengeneza ili tuenende nayo. (EFE. 2:10 SUV).

Kumbe Mungu alipotuumba, alituumba ili tutende matendo mema fualni maalum ambayo yalishaandaliwa ili tuenende nayo. Sasa kwanini nisijue yale ambayo niliumbwa niyafanye alafu niyafanye?

Mungu anatuambia kwenye kitabu cha Yeremia:

Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema BWANA, ni mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho. (YER. 29:11 SUV).

Kwa mujibu wa hili andiko yapo mawazo ambayo Mungu anatuwazia sisi. Ni mawazo ya mema na siyo ya mabaya, kutupa mwisho uliyojaa matumaini.

Tafsiri ya Bibilia ya Habari Njema inasema:

Maana, mimi Mwenyezi-Mungu ninajua mambo niliyowapangia. Nimewapangieni mema na si mabaya, ili mpate kuwa na tumaini la baadaye. (Yeremia 29:11 BHN).

Kwa hiyo ipo mipango ambayo. Mungu ametupangia. Ametupangia mema na si mabaya ili tuwe na tumaini la baadaye.

Sasa kama Mungu anayo mawazo mazuri kwa ajili yetu, na Mungu anayo mipango mizuri kwa ajili yetu, kwanini tusitafute kujua hayo mawazo na hiyo mipango ili nasi tuwaze na kupanga sawa na hiyo? Maana Yeye anajua kwanini alituumba na Yeye anajua alituumbia uwezo wa kufanya nini ndani yetu. Kwanini tusitafute kuyajua mawazo ya Mungu kwa ajili yetu na mipango hiyo aliyo nayo kwa ajili yetu ili tusiishi maisha yetu tukipoteza tu muda na mipango ambayo sio ya Mungu kwa ajili yetu ambayo haiwezi kufanikiwa hata hivyo?

Tafsiri ya Neno ya andiko hili la Yeremia inasema:

Kwa maana ninajua mipango niliyo nayo kwa ajili yenu,’’ asema BWANA. “Ni mipango ya kuwafanikisha na wala si ya kuwadhuru, ni mipango ya kuwapa tumaini katika siku zijazo.

Mipango ya Mungu kwa ajili yetu itatufanikisha. Mafanikio yetu katika maisha haya yanategemea sisi kulifahamu kusudi la Mungu kwa ajili ya maisha yetu na kutembea katika hilo.

Napenda maneno ninayoyasoma katika kipande cha mstari kwenye kitabu cha Waefeso:

na ndani yake sisi nasi tulifanywa urithi, huku tukichaguliwa tangu awali sawasawa na kusudi lake yeye, ambaye hufanya mambo yote kwa shauri la mapenzi yake. (EFE. 1:11 SUV).

Mungu hufanya mambo yote kwa kushauriana na mapenzi Yake kwa ajili yako. Kama hilo analotakwa alifanye litasaidia katika kudhibitisha mapenzi Yake katika maisha yako atalifanya. Kama analotakwa alifanye litavuruga mapenzi ya Mungu katika maisha yako, hakika hatalifanya.

Najuaje sasa mapenzi ya Mungu kwa ajili yangu? Naujuaje huo mpango wa Mungu kwa ajili yangu?

Kwanza kabisa badilisha kufikiri kwako. Anza kufikiri kwa namna ambayo kutaweka madai kwenye upeo wa kufikiri kwako juu ya kuujua mpango wa Mungu kwa ajili ya maisha yako.

Wala msiifuatishe namna ya dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu. (RUM. 12:2 SUV).

Ukifanya upya nia yako utajua mapenzi ya Mungu yaliyo mema, yaliyo kubalika na yaliyo kamili kwa ajili ya maisha yako.

Akili yako lazima igeuzwe. Akili yako lazima ibadilishwe. Kinachoweza kubadilisha akili yako kwa kiwango hicho ni kusoma kwako kwingi. Usomaji wako kwa wingi kutakugeuza akili yako na kupanga kufikiri kwa akili yako sawa na kusudi la Mungu na mapenzi ya Mungu kwa ajili yako.

Alipokuwa akijitetea hivi, Festo akasema kwa sauti kuu, Paulo, una wazimu, kusoma kwako kwingi kumekugeuza akili. (MDO 26:24 SUV).

Sasa ni nini hicho natakiwa kukisoma kwa wingi ili akili zangu zigeuzwe, zifanywe upya ili nipate kuyajua mapenzi ya Mungu kwa ajili yangu alafu nitembee katika hayo?

Macho yako yaliniona kabla sijakamilika; Chuoni mwako ziliandikwa zote pia, Siku zilizoamriwa kabla hazijawa bado. Mungu, fikira zako zina thamani nyingi kwangu; Jinsi ilivyo kubwa jumla yake! Kama ningezihesabu ni nyingi kuliko mchanga; Niamkapo nikali pamoja nawe. (ZAB. 139:16-18 SUV).

Siku zangu na zako zilizoamriwa na Mungu zimeandikwa chuoni mwa Mungu au katika neno la Mungu. Tunapokuwa wasomaji wazuri wa neno la Mungu, siku zetu zilizoamriwa na fikra au mawazo au mipango ya Mungu kwa ajili yetu inafunuliwa kwetu.

Kumbuka hili:

Neno lako ni taa ya miguu yangu, Na mwanga wa njia yangu. (ZAB. 119:105 SUV).

Neno la Mungu ni taa ya miguu yetu ikimaanisha itatusaida kuona tulipokanyaga, tulipo sasa hivi na ni mwanga wa njia yetu maana yake litatuonyesha tunapopaswa kwenda.

Nimalize kwa andiko hili:

Ndipo niliposema, Tazama nimekuja, (Katika gombo la chuo nimeandikiwa,) Kuyafanya mapenzi yako, Ee Mungu wangu, ndiyo furaha yangu; Naam, sheria yako imo moyoni mwangu. (ZAB. 40:7, 8 SUV).

Ukishajua yale yaliyoandikwa kukuhusu kwenye gombo la chuo kwa ajili yako ni rahisi kuyafanya mapenzi ya Mungu uliyozaliwa kuyatumikia.

Jenga ukaribu na neno la Mungu. Lisome kwa wingi neno la Mungu. Litakufungua kuwaza ikupasavyo kwa habari ya mpango wa Mungu kwa ajili yako.

Uncreated One | Christ For The Nations Music


Pakistani Christian leader needs your prayers and support

Nobel peace prize nominee, Mr. Julius Salik is currently promoting his mission of world peace, a former federal minister, who is the true and genuine leader of not only Christian community but the other minorities. He has been elected 3 times MNA, as an independent member of the parliament, whose constituency was whole Pakistan (for more Information visit www.jsalik.com)

Mr. J Salik challenged the ordinance of Gen Pervez Musharraf regime in Supreme Court of Pakistan on which Justice Muneer A Sheikh gave remarks in the presence of larger bench which was consisted of Chief Justice Sheikh Riaz, Justice Munir A Sheikh, Justice Nazim Hussain Siddiqui, Justice Ch Muhammad Iftikhar and Justice Qazi Muhammad Farooq, that a change is required for electing the minorities and ladies reserved seats during the hearing in October 2002 at Supreme Court.

Mr. J Salik says “I feel that I have a right to bring your attention to those injustices, prejudices and discriminations which Christians and other minorities are facing in this Islamic Democracy of Pakistan, which came into being to be a welfare state. The following points need your serious consideration; and so-called democracy the major political parties have been given the powers to nominate members of minorities in parliament. Which are not the true and genuine representatives of the minorities because they are not elected by the votes of minorities; they are only selected by the major political parties. So they have nothing to do with minorities and their problems. Moreover in the present parliament there are only 2 representatives of Christian community where as Hindus are holding 8 seats and there is no representative of Parsi, Sikh, Buddhist and Ahmedi communities in the present parliament”

Mr. Salik further adds “In 1985 the total strength of National Assembly was 207 and 217 including 10 (4 Christians, 4 Hindus, 1 Parsi, Buddhist, Sikh and 1 Qadyani) minorities’ members, while the current strength of National Assemble is 342 including 60 reserved for women, and 10 from minorities. Note that after years the no of minorities’ seats remains the same, which shows that Christian minorities are barren”

In light of above mentioned circumstances:

During the hearing of this petition, Chief Justice Sheikh Riaz adjourned the hearing and gave the date after election. On this decision, Mr. J Salik showed his anger and took the petition back. He said that I do not have any hope of justice from this court.

After this Mr. J Salik decided to file and admit the petition in the Shariat Court, with the hope that being a non-Muslim citizen of Pakistan, I will get speedy justice from Shariat Court, but in the very first hearing of the petition, due to the absence of a Judge of a Full Bench, no a action was taken. Again once again, being hopeless from the Shariat Court, he decided to take the petition back after long period of 4years.

Then he waited for 8years long period that the time will come when this dictatorship of Gen Pervez Musharraf will end and the democracy will be restored, but after the restoration of the democracy, this democratic government very shamefully turned this ordinance into a constitution by 18th amendment.

Than once again, Mr. J Salik decided to challenge the 18th amendment into Supreme Court. On this petition the renowned Justices of the Supreme Court have passed the following remarks;

1. Justice Jawad Khawaja said on 2nd September, 2010, that more than 30% of the members of parliament are so-called representatives of their people.

2. Justice Javed Iqbal said on 6th September, 2010 that the present way of selection of minorities’ and reserved seats is the opposite of democratic reign.

3. Justice Khalil Ul Rehman said on 28th September 2010 the present parliament has not made any law regarding the election of minorities’ seats.

4. Chief Justice Iftikar Muhammad Chaudry said that the selection of the minority members in the Parliament is against the Article 226 of the constitution.

And at the present situation the Minorities affairs ministry is being devolved according to the cabinet meeting held yesterday which was chaired Prime Minister Yousaf Raza Gillani.

The minorities have their own importance in the federal and as this ministry was formed by late Zulifikar Ali Bhutto who was maker of laws in 1973 to show the importance of the minorities to the world and by devolving the minority affair ministry the government is degrading the federal

As according to the open commitment made on the national flag of Pakistan with the Christian in Holy Trinity Church, Karachi by first prime minister of Pakistan by showing the Christians that the white colour on the flag represents the Christians and the other minorities will also benefit from this.

Hereby I request all the true lovers of democracy and human rights to pray for us and to provide us with your support as we are in the need of funds to arrange campaigns to motivate the people around the globe, to spread the awareness of the importance of minority ministry and minorities elections, to arrange corner meetings an major conferences

For Further Details Do feel Free to Contact Mr. J.Salik

Cell: 0314 5252309 / 0345 8567926

Email: wmapeace@yahoo.com , info@queenofdemocracy.com

Web: www.jsalik.com

For your support and Help

J.Salik

Account No. 1018262-6

UBL Aabpara Branch

Islamabad

Note : Western Union and Money Gram can also be accepted for support

Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani Papa Francisko atoa salamu za Mwaka Mpya

Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani, Baba Mtakatifu Francisko
Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani, Baba Mtakatifu Francisko ametoa ujumbe maalumu wa salamu za Mwaka Mpya, akisema vitendo vya rushwa na ufisadi ndivyo vinavyotishia kuuvuruga umoja na amani dunia.

Katika ujumbe huo alioutoa Makao Makuu ya Kanisa Katoliki mjini Vatican, Papa Francisko alilitaja tishio jingine la dunia ni uahalifu wa makundi.

“Rushwa na ufisadi pamoja na uhalifu wa makundi ni mambo yanayotishia udugu,” inaeleza sehemu ya ujumbe huo wa Papa, uliohaririwa na Padri Richard Mjigwa, wa Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican.

Alitoa ujumbe huo wa mwaka mpya wakati Kanisa Katoliki duniani likiwa kwenye maombi kuomba amani duniani kwa siku  50, kwa kile kilichoelezwa kuenea kwa chuki, machafuko na kusababisha uhasama na vita sehemu nyingi.

Alisisitiza kuwa njia pekee ya kuvunjilia mbali uhalifu na vitendo hivyo viovu duniani ni jamii kuwa na moyo wa kuhurumiana na kujenga undugu.

“Udugu unavunjilia mbali ubinafsi ambao ni chanzo cha mifumo ya rushwa na ufisadi, uhalifu na uvunjifu wa utawala wa sheria,” alisema Papa Francisko.

Alisisitiza kuwa rushwa na ufisadi ni mambo ambayo yanachangia kwa kiasi kikubwa kudhalilisha utu na heshima ya binadamu pamoja na mazingira.

Maaskofu: Watawala heshimuni maoni ya wananchi Katiba mpya

Maaskofu wa Makanisa mbalimbali mchini, wamezungumzia kwa nyakati tofauti mustakabali wa Taifa huku wakitaka watawala kuheshimu maoni yaliyotolewa na wananchi kuhusu Katiba mpya pamoja kuchukua hatua mapema kwa viongozi waliopewa dhamana za kuongoza na kushindwa kuwajibika.
 
Katika mahubiri yake kwenye Kanisa Kuu la Utatu Mtakatifu, Askofu Mkuu wa Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Morogoro, Godfrey Seheba, alitaka watawala kuheshimu mapendekezo yote yalitolewa katika rasimu ya pili ya Katiba iliyowasilishwa na Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji mstaafu Joseph Warioba.
 
Askofu Seheba alisema kuwa mapendekezo hayo yaliyotolewa na wananchi iwapo yataheshimiwa na kupitishwa katika Bunge la Katiba, yatasaidia kuleta umoja na mshikamano ili kuifanya nchi kuwa na amani na utulivu kama ilivyokuwa na sifa yake.
 
Hata hivyo, Askofu Seheba alisisitizia umuhimu wa Watanzania kuendelea kuombea rasimu hiyo ili ipatikane kwa Katiba mpya itakayokidhi mahitaji ya Watanzania kwa maslahi ya nchi na ustawi wa jamii.
 
Naye Askofu Mkuu wa Kanisa la Kilutheri la Kiinjili Jimbo la Morogoro, Jacob Mameo, akizungumza katika mahubiri yake katika Kanisa la Mji mpya, alisema mwaka 2014, uwe ni mwaka wa serikali kuchukua hatua za haraka kwa viongozi waliopewa dhamana ya kuongoza na kushindwa kuwajibika badala ya kusubiri madhara kujitokeza kwa wananchi.
 
Askofu Mameo alisema mwishoni mwa mwaka jana, Taifa lilishuhudia madhara makubwa waliyopata wananchi wakati wa Operesheni Tokemeza kutokana na viongozi hao waliopewa mamlaka kushindwa kusimamia ipasavyo.
 
Alisema hali hiyo isipodhibitiwa mapema itazidi kuleta athari kwa wananchi. Askofu Mameo aliwataka viongozi wanaopewa dhamana kuwa na hofu ya Mungu katika utendaji wao wa kazi na kuweka maslahi ya taifa mbele ili kuleta maendeleo na kudumisha amani iliyopo.
 
Kwa upande wake, Mhashamu Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Morogoro, Telesphori Mkude, alisisitiza umuhimu wa waumini wa dini zote kuendelea kuliombea Taifa ili kuwa na amani hasa katika kipindi hiki cha mchakato wa kupata Katiba mpya.
 
Askofu Mkude aliwataka Watanzania kuepuka mifarakano na uvunjifu wa amani na badala yake wawe kitu kimoja hasa katika kipindi hiki cha kuibuka kwa rasilimali mbalimbali za taifa ikiwamo gesi na mafuta.

Askofu Mkuu wa Anglikana aasa amani ilindwe mithili ya mboni ya jicho

Maaskofu: Watawala heshimuni maoni ya wananchi Katiba mpya
Askofu Mkuu wa Kanisa la Anglikana Tanzania, Jacob Chimeledya, amewataka Watanzania kuilinda amani kama mboni ya jicho ikiwa ni pamoja na kuitii mamlaka ya Mungu iliyopo.
 
Akitoa salamu za Mwaka Mpya kwa waumini wa kanisa hilo pamoja na Watanzania katika ibada iliyofanyika Dayosisi ya Mpwapwa mkoani hapa,

Askofu Chimeledya alisema kuwa mwaka 2013, ulikuwa na changamoto mbalimbali, hivyo Watanzania wajifunze kusamehe ili kuwa na amani ya kweli.

 
Alisema kuwa katika mataifa mbalimbali, watu wenyewe kwa wenyewe wanapigana kwa tatizo la kutosamehe wakati hayati Nelson Mandela, ni mfano mzuri na amefundisha kusamehe.
 
"Hakuna namna yoyote itakayofanya bila kusameheana ili kuwa na amani ya kweli," alisisitiza Askofu Chimeledya.

Aliwataka Watanzania kuwa na chachu ya ukombozi ili kuleta mabadiliko chanya katika jamii.
"Pia nawasihi mjenge moyo wa uzalendo ili kulisimamia taifa kwa uadilifu...wazee wa makanisa waendelee kuhubiri ukombozi," alisema Askofu Chimeledya.
 
Akizungumzia suala la tatizo la dawa za kulevya, Askofu Chimeledya aliomba serikali kuongeza nguvu kusimamia jambo hilo kwa kuwa lina watu fulani wanaojihusisha na inawezekana wanafahamika.
 
"Serikali ichukue hatua thabiti ya kukabiliana na tatizo la dawa za kulevya kwani vijana wanaathiriwa sana," alisema Askofu Chimeledya
 
Aidha, alisema kuwa ni jambo jema kumshukuru Mungu kwa kuuona Mwaka Mpya wa 2014. Hata hivyo, alisema kumekuwapo na mafanikio katika taifa kwa mwaka 2013 ikiwa ni pamoja na mchakato wa Katiba mpya ambao umeleta historia. Pia alisema ugunduzi wa gesi, madini ya uranium, ni neema ya mwaka 2013 ambapo sasa kunahitajika kuwa na sera na usimamizi mzuri kwa manufaa ya Watanzania wote.
 
Kuhusu maandamano na migomo, Askofu Chimeledya alisema kuwa watu wapewe nafasi ya kusikilizwa ili kusiwapo na migomo wala maandamano yanayosababisha athari kwa taifa.
 
"Niwaombe sasa Watanzania kutafuta haki kwa kuandamana kwa amani bila kuleta vurugu...kuandamana kwa kutafuta haki lakini yasiwe ya kuvunja amani iliyopo," aliasa Askofu Chimeledya.

CHANZO: NIPASHE

Ilala TAG laandika Historia ya Miaka 40

Ilikuwa ni siku nzuri jumapili ya Desember 15 mwaka jana, kwa waamini wa kanisa la Tanzania Assemblies of God Ilala jijini Dar es salaam, wakiongozwa na shujaa wao Mchungaji Titus Mkama na Mke wake Mary, walipoadhimishwa miaka 40 ya kuzaliwa kwa kanisa hilo wakiwa na ushindi mkubwa.

Akihubiri katika ibada hiyo iliyohudhuriwa na maaskofu wachungaji na viongozi mbalimbali wa dini na serikali, Askofu Mkuu wa kanisa la Tanzania Assemblies of God Dk Barnabas Mtokambali  alisema kuwa,
Mchungaji Titus Mkama wa Kanisa la Tanzania Assemblies of God Ilala Jijini Dar es salaam
Katika ibada hiyo iliyokuwa na mvuto wa hali ya juu, kutokana na historia  ya mtumishi wa Mungu  Mchungaji Titus Mkama kwa mambo mbalimbali pamoja na mapito makali aliyopitia kwa kipindi cha utumishi wake, Askofu mkuu wa TAG Dr Mtokambali aliongoza maombi mbalimbali ya kumuombea mtumishi huyo na mke wake huku wengine walitokwa na machozi.

Askofu Dk. Mtokambali alisema, kwa nini Mungu anatutaka tuwe na maadhimisho maalumu ya matukio ya maisha yetu, Mungu aliwaagiza watu wake kufanya maadhimisho kama hayo kama neno la Mungu linavyoeleza, kutoka katika kitabu cha kumbukumbu la Torati (16:9-17)

  Alisema kuwa, Mungu anatambulisha sherehe na maadhimisho siyo maonesho wewe ulivyo, bali ni kufanya kwa mapenzi ya Mungu na siyo vinginevyo.

 Aidha alisema kuwa maadhimisho yanawaletea watu wa Mungu kufurahi na kukomaza ushirika wao. Askofu huyo alisema kuwa maadhimisho pia yanatumika kama wakati wa matoleo ambapo alisisitiza watumishi wa Mungu waliohudhuria sherehe hiyo kufanya changizo la kiasi cha pesa zilizohitajika sh. Milioni 150, kwa ajili ya upanuzi wa jingo la ibada, ambapo wageni na watumishi wa Mungu walihudhuria ibada hiyo na kutuoa hadi mbalimbali .

  Naye mchungaji kiongozi wa kanisa Dk. Titus Mkama alitoa shukrani zake kwa Mungu na kwa watu wote waliohudhuria na kuwezesha kufanikiwa maadhimisho hayo ambapo kwa kukamilisha furaha yao Askofu pamoja na mtumishi huyo na wengine walilishana keki maalumu pamoja na ndafu iliyoandaliwa.

  Ibada hiyo ya maadhimisho ilipambwa na kwaya, waimbaji mbalimbali wa nyimbo za injili ambapo furaha, vifijo na vigelegele vilitgawala siku hiyo isiyo ya kawaida.

  Akisoma historia fupi ya Kanisa hilo, Mtumishi wa Mungu, Mchungaji DK. Titus Mkama alitoa shukrani zake kwa viongozi mbalimbali kwa Makanisa waliohudhuria na kwa watu alioanza nao pamoja huduna hiyo.

Dk. Mkama alisema kuwa wanamshukuru Mungu kuwa kanisa hilo limekuwa la kwanza kupewa kibali na Serikali ya Tanzania kuhubiri magerezani huduma ambayo waendelea nayo hadi sasa.
  Alisema kuwa katika huduma ya jamii wamekuwa wakiwatunza wazee, kuwalea watoto yatima ambao wengine wameweza kuwaendeleza hadi chuo kikuu.

  Pamoja na mafanikio hayo lakini pia wanazo changamoto kama vile upanuzi wa viwanja vya kuhubiria injili baada ya viwanja vya serikali kuzuiliwa.

  Kanisa la TAG ilala ilianzishwa mwaka 1973, shule ya uhuru kariakoo, na baadaye walihamia katika maeneo ya msimbazi Centre Ilala baada ya eneo la zamani kuonekana kuwa halitoshi kukidhi ongezeko la waumini kutokana na ufinyu wake.

Mkesha wa Mwaka Mpya Dar Es Salaam Pentecostal Church( DPC), Matukio Katika Picha


Pastor Safari Paul akiongoza Kwaya ya Rivers of Life katika Mkesha huo

John Lisu

Dr. Onna

Bale

Rivers of Life ya DPC

Abel Majaliwa Mchungaji Kiongozi wa Dar Es Salaam Pentecostal Church akihubiri katika usiku huo wa mwaka mpya

Abel Majaliwa Mchungaji Kiongozi











Watu wakiombewa kuanza mwaka 2014 na Bwana kwa ushirika mzuri katika mkesha huo

Vijana walipata kuokoka katika Mkesha huo wa mwaka mpya


Askofu Kakobe ataja vyama vya Kufutwa



 

Askofu Mkuu wa Kanisa  la Full Gospel Bible Fellowship, Zacharia Kakobe, amezitaka mamlaka zinazohusika kuvifuta vyama vyote vya siasa vinavyoendeshwa kwa misingi ya ukabila havivurugi nchi.

 Askofu Kakobe, amezungumza Kanisa kwake hivi karibuni kwenye ibada ya sikukuu ya Krismas
alisema miaka kadhaa iliyopita nchi haikuwa akiandamwa na vitendo vya ukabila tofauti na sasa ambapo hali imekuwa mbaya.

  Alisema kuna baadhi ya vyama vya siasa nchini ambavyo kwa kipindi kirefu kimejulikana kuwa vinendeshwa  kikabila tofauti na sasa ambapo hali imekuwa mbaya.

   Alisema kuna baadhi ya vyama nya siasa nchini ambavyo kwa kipindi kirefu vimeendeshwa kikabila, jambo ambalo ni kinyume na sheria za nchi.

    Askofu Kakobe, alizishauri mamlaka zinazohusika kuvifuatilia vyama hivyo kuvifuta katika orodha ya vyama vya siasa kwani ni hatari katika mustakabadhi wan chi na wananchi wake.

 Akizungumza suala zima la uongozi wanachi, hususani kitendo cha mawaziri kadhaa kuondolewa katika nyadhifa zao, alisema ubovu wa viongozi unachangia na mfumo wa kuteua viongozi.

   Askofu Kakobe alisema kwa kawaida uongozi ni kipaji, hivyo watu wanapoona kunakuwa na viongozi wasiowajibika kikamilifu, wajue kuwa kuna tatizo katika uteuzi wao. Moja ya tatizo kubwa linaloathiri nchi kwa sasa alisema ni kuchagua watu kwa kuangalia maenao wanayotoka.