Mkapa atimiza miaka 75 ya kuzaliwa wake

Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa jana aliadhimisha miaka 75 ya kuzaliwa kwake kwa kufanya Ibada ya Misa iliyoongozwa na Askofu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kadinali Pengo.
Katika ibada hiyo ya shukrani iliyofanyika Kanisa Katoliki la Maria Imakulata, Upanga jijini Dar es Salaam, Mkapa aliwataka Watanzania kumshukuru Mungu kwa kila jambo.
“Tunamshukuru Mungu kwa majaliwa aliyoipatia nchi yetu ya Tanzania na tunamwomba azidi kuijalia umoja katika yote tunayofanya na tunayokusudia kuyafanya,” alisema Mkapa.
Mkapa pia aliwashukuru waumini wenzake katika kanisa hilo, huku akifichua siri kwamba, Kadinali Pengo alimtaka ahamie Kanisa la Mtakatifu Joseph wakati alipokuwa rais, lakini hakukubali.
Rais Mstaafu Benjamin Mkapa akipongezwa na Mhadhama Polycarp Kardinali Pengo jana wakati misa ya jubilei ya miaka 75 ya kuzaliwa kwake. 
Kwa upande wake, Kardinali Pengo aliwataka Watanzania kuwa na tabia ya kumshukuru Mungu kwa kila jambo.
“Alichofanya Rais Mstaafu Mkapa ni cha kuigwa. Tunatakiwa kutambua kuwa hatuishi kwa nguvu zetu bali kwa uwezo wa Mungu hivyo ni lazima tumshukuru kama alivyofanya mwenzetu,” alisema Kardinali Pengo.
Baadhi ya viongozi waliohudhuria ibada hiyo ni pamoja na Mawaziri Wakuu Wastaafu, Edward Lowassa na Cleopa Msuya, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu wa Bunge), William Lukuvi na Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia.
Wengine ni waziri wa zamani, Profesa Philemon Sarungi, Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dk Alex Malasusa pamoja wakuu wa zamani wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Majenerali, Robert Mboma na George Waitara.
Source:Mwananchi

Prayer for the Philippines

Three days after super typhoon Yolanda, one of the strongest storms in history, crashed into the Philippines, many survivors are still coming to grips with the level of devastation they are facing. Humanitarian agencies around the world have mobilized in order to bring aid to the storm’s victims, but the amount of loss is staggering and progress has been slow. In this time of crisis, many churches are calling on Christians to take an active role in the relief effort. The Pope himself has expressed solidarity with the victims of typhoon Yolanda, and encouraged pilgrims to reach out to storm victims in both prayer and action. According to CNA, Pope Francis led a brief prayer for the Philippians, before continuing to address the crowd.  





“The Pontiff then exhorted, ‘let us try also to reach out to them with practical help.’ Secretary of State Parolin’s message explained that Pope Francis ‘is especially mindful of those who mourn the loss of their loved ones and of those who have lost their homes.’

‘In praying for all the people of the Philippines, the Holy Father likewise offers encouragement to the civil authorities and emergency personnel as they assist the victims of this storm,’ it continued.”

Other Christian organizations have also assembled to help those struggling with the storms aftermath, including international residents who have been unable to reach family members. One such Church is the Philippine International Bible Church in Laytonsville, Maryland. Among the congregation, several members have close relatives who were living in the path of the storm. One member, Alvenia Ropeta, recently told reporters that her 2-year-old son, Luke Ropeta, was living with her sister-in-law in a village at the time of the storm. Since then, they have been unable to contact one another, and Alvenia does not even know if they are still alive.

All Alvenia could hope to do was send messages through news reports,

“’Just be still. Just be still and hang in there. That's what I'm exactly doing over here. I'm putting all of my trust and faith that God is in control and He will make sure that we will get through all of these trials and calamities, that He will be taking care of us. And give Luke my warmest hug and kiss him for me,’ said Ropeta.”
The Christian humanitarian agency, Samaritan’s Purse, has recently launched a massive campaign in an effort to rescue those suffering from Yolanda’s aftermath. To donate, or to find more information on how you can get involved in the effort, please click here. Furthermore, CNN has provided its readers with a list of agencies currently working to provide resources to the storm-affected areas of the Philippians, for more information please click here. Remember that in all things God call us to be his hands of healing in a world full of despair. It is time for Christians to step forward and take action, please donate today.

Christina Shusho Live Katika NATAKA NIMJUE


China Asks Church for Help With Social Care

The Chinese government has welcomed the role of the church in providing social care in the country.China’s leaders have been holding a meeting this week in Beijing to discuss the economic and political agenda for the next decade, in which it seems the church will play a vital role.

“The government welcomes the support of the church,” said government official Wang Xinhua at a recent Shanghai conference on the role of Christianity in China, sponsored by the Bible Society. “We lack the resources to meet all the needs that we face, so we need religious organizations in order to do so.”

China is facing a social care crisis, particularly in caring for an increasingly elderly population. (Richard Asia/Flickr/Creative Commons)








Wang said the “beliefs” and “love” of the church were an “advantage” to society.He added that China’s charitable sector was facing “a crisis of confidence” due to corruption scandals, saying the church was a less corrupt partner to the government.

Leading academic professor Choong Chee Pang told those at the conference, “Many social problems have their root causes in social injustice, the abuse of power, inequality, the widening gap between the rich and the poor due to mismanagement of the resources, corruption and bribery.”

In an outspoken move, the professor said that as the church took up the challenge of providing social care across China, particularly among the elderly and poor, it must not lose its prophetic role.

“The church needs to be a prophet and a servant,” he said. “This is not a problem in a free or democratic society, but in other societies it can be a sensitive issue. It is hard for the Chinese church to play the role of a prophet especially with a critical voice.”

Though it is the world’s second biggest economy, China is facing a social care crisis, particularly in caring for an increasingly elderly population.

According to the Chinese Academy of Social Sciences, by 2040 nearly 20 percent of China’s rural population will be aged over 65.

At the conference, the government called on the church to provide care for the elderly, as well as offer drug prevention and rehabilitation and to work with those living with HIV.

Sixty-four-year-old Pu Ti Hua has already benefited from the social care provided by China’s churches. During the 2008 Sichuan earthquake, she and her husband were made homeless. They joined around 200 people who sought sanctuary in the local church in the town of Yanting Yunxi.

“There’s no Christianity or churches where we lived,” says Ti Hua. “But for the first time I felt the warmth of these people and their love. I had been totally shaken, but I found peace here. I lost everything: my home and all my belongings. It was very difficult. I felt terrible. I was emptied out. I had nothing. But the church helped me get over it.”

Today Ti Hua and her husband Song Cheng live in two rooms above the church. Here they return the kindness done to them by cooking food for church members three days a week.

Upendo Kilahilo kuhudumu Tamasha la Pasaka Disemba

Upendo Kilahilo

Baada ya msanii Upendo Nkone kuthibitisha kushiriki Tamasha la Krismas litakalofanyika Desemba 25 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, msanii Upendo Kilahiro naye amejitosa kushiriki.

Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya tamasha hilo, Alex Msama alisema jana kuwa tayari wamefikia makubaliano na msanii huyo na wanafurahi kwamba tamasha litaenda vile wanavyotaka.
“Kilahiro tutakuwa naye, naamini mwaka huu tamasha hili litakuwa bora zaidi kutokana na kushirikisha waimbaji wengi wakali.

“Mpaka sasa Watanzania wawili tumeshakubaliana nao, yaani Kilahiro na Upendo Nkone,” alisema Msama na kuongeza kuwa bado wanaendelea na mazungumzo na wasanii wengine wa nje na ndani ya nchi.

Baadhi ya nyimbo za msanii huyo ni Zindonga alioimba kwa Kizulu), Unajibu Maombi na Ni Salama Rohoni. Pia anatamba na albamu mbalimbali ikiwemo Ficho Langu.

Tamasha la Krismas linaandaliwa na Kampuni ya Msama Promotion ya jijini Dar es Salaam, ambayo pia huandaa Tamasha la Pasaka kila mwaka.

Waandaaji hao wamepanga tamasha hilo lifanyike Desemba 25 Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na siku inayofuata Uwanja wa Jamhuri, Morogoro.

AFLEWO Tanzania yakutanisha wachungaji katika kuelekea AFLEWO 2014

Kukutana huko kumetokea siku ya jana kata Hoteli ya Peacock Dar es salaam, kukutana huko kumeambatana na chai ya asubuhi (Pastor’s Breakfast) kwa lengo la kuwashilikisha wachungaji hao maono na mipango ya huduma ya AFLEWO 2014 na kuomba ushiriki wa wao na washira wao katika maadalizi kwa ajili ya Mkesha huo unaotegemea kufayika mwakani mwezi wa sita.

Kusanyiko limetokea siku chache kabla ya uzinduzi wa usajili na Mass Kwaya ambapo unaanza Jumapili hii saa 9:00 mchana Katika kanisa la City Christian Centre (CCC) Upanga jirani na Chuo cha mzumbe, usahili huo utaendelea mpaka Januari na kufunga usajili wa kujiunga na Mass Kwaya hiyo,

Siku ya jana kusanyiko hilo lilikuwa likiongozwa na Walezi wa huduma ya AFLEWO Tanzania  ambao ni Pastor Paul Safari (DPC), Bishop Fredrick Kyara (P.C.E.A St. Columbus), Mwenyekiti Geoffrey Obielo na Administrator wa AFLEWO Tanzania Anna Abella Munyagi.

Baadhi ya mambo yaliyozungumzwa ni pamoja wao na kuwa walezi wa AFLEWO wa sehemu kidogo katika kutoa ushirikiano pale itakapotakiwa,huduma zao kusaidia kuwa ruhusu waumini wenyewe uwezo wa kuimba kuja siku ya Jumapili ujiunga na AFLEWO Mass Kwaya,tutakapo karibia siku ya tukio mwakani kutoa nafasi yaAFLEWO kwaya kuhudumu Makanisani kwao ikiwa ni sehemu kuitangaza na taharifa kuwafikiwa watu katika makanisa mbalimbali ili uja kuhudhulia Mkesha huo.

Kwa mara ya kwanza Tanzania AFLEWO ilinza kwa kufanyika mwaka 2011 katika ukumbi wa Diamond Jubilee, 2012 ilifanyika katika kanisa la City Christian Centre (CCC) Upanga, AFLEWO 2013 ilifanyika katika Kanisa BCIC Mbezi Beach,Mwaka 2014 inategemewa kufayika mwezi wa sita tutakufahamisha mahala takapo fanyika siku zinavyozidi kwenda.

NB:Katika usajili wa Kwaya ya waimbaji vigezo wa waimbaj  na wapigaji wa vyobo ni waliokoka na Yesu Bwana na Mwokozi kwao pia uwe ueujua kuimba.Karibuni sana bila kukosa!

Mlezi wa AFLEWO Tanzania Bishop Fredrick Kyara (P.C.E.A St. Columbus),
Mlezi wa AFLEWO Tanzania Pastor Paul Safari (DPC)
Watumishi wa Mungu mbalimbali wakiwa makini kumsikiliza mzungumzaji katika kusanyiko hilo
Wachungaji kutoka huduma mbalimbali wakiwa makini kumsikiliza mzungumzaji katika kusanyiko hilo



Pastor Fred Okello kutoka Upper Roo Ministry,Pembeni ni ni mchungaji mwakilishi kutoka Mlima wa Moto kwa Mama Rwakatare Mikocheni B.

Mama Shegga

Bishop Mwende toka DPC








Kwa mawasiliano zaidi

+255 712 586 643
+255 757 332 062
aflewodar@gmail.com 

Vyuo vya KKKT vyataka maslahi ya madaktari yaboreshwe

Kiongozi wa  KKKT , Askofu Dk Alex Malasusa
Baraza la uongozi wa vyuo vikuu vinavyomilikiwa na Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) chini ya mwavuli wa Chuo Kikuu cha Tumaini-Makumira  (Tuma),limeitaka serikali kupitia 
Mpango wa Matokeo Makubwa sasa (BRN), kuboresha maslahi ya madaktari na watumishi wa sekta ya afya nchini badala ya kuacha wanataaluma hao wakafikiria kutimkia nchi za Kusini mwa Afrika kusaka maslahi. 
Mwenyekiti wa baraza hilo, Prof. Esther Mwaikambo akizungumza katika mahafali ya 14 ya Chuo Kikuu Kishiriki cha Afya na Tiba cha KCMC kwa niaba ya Mkuu wa Kanisa hilo nchini.
Askofu Dk. Alex Malasusa, alisemawanataaluma hao licha ya kutakiwa kuwa wazalendo kwa taifa lakini pia Wizara ya afya na Ustawi wa Jamii, inapaswa kuwekeza kwa kulinda wataalamu hao wasijiingize katika vitendo vya rushwa na kukimbilia nje ya nchi kutafuta maslahi yaliyoboreshwa.

Awali,Mkuu wa chuo hicho, Prof.Egbert Kessy, alisema kuwa Tanzania imeendelea kukumbwa na upungufu wa madaktari licha ya kuwepo ongezeko la wanafunzi wanaodahiliwa kujiunga na fani hiyo kila mwaka na kwamba kwa takwimu za sasa, daktari mmoja anahudumia wagonjwa kati ya 26,000 hadi 30,000.

Kessy alisema kiwango hicho ni kikubwa mara tano zaidi ya kile kinachotakiwa na Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO) na kusema ipo haja ya wahitimu kuwa wazalendo, na kupenda kufanya kazi nyumbani badala ya kukimbilia nje ya nchi kutafuta kazi zenye mishahara mikubwa.

Kwa mujibu wa Prof.Kessy, karibu asilimi 60 ya madaktari wanaohitimu mafunzo nchini hukimbilia kutafuta ajira nchi nyingine Kusini mwa jangwa la Sahara.

Source Nipashe

Happy Birthday Rais mstaafu wa awamu ya tatu, Benjamin William Mkapa


Makamu wa Rais Dkt.Bilal azindua Benki ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania;Maendeleo Benki.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akihutubia wakati wa ufunguzi rasmi wa benki hiyo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akifunua kitambaa kuashiria kuweka Jiwe la Msingi katika benki ya Maendeleo, Kulia ni Askofu Mkuu wa Kanisa la KKKT, Dkt. Alex Malasusa (kushoto) ni Naibu Waziri wa Fedha,Janeth Mbene.
 Utepe ukikatwa kuashiria kufungua Benki ya Maendeleo, wakati wa hafla ya uzinduzi

Baadhi ya wageni waalikwa wakiwemo watumishi wa Mungu,Viongozi wa Serikali na kutoka katika mashirika mbalimbali walipohudhuria hafla hiyo ya ufunguzi wa benki hiyo.
Baadhi ya wageni waalikwa wakiwemo watumishi wa Mungu,Viongozi wa Serikali na kutoka katika mashirika mbalimbali walipohudhuria hafla hiyo ya ufunguzi wa benki hiyo.
Makamu wa Rais  Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi Cheti, Rose Mushi, ambaye ni mmoja kati ya waanzilishi wa benki hiyo na wahamasishaji kwa watu na kuwa manager mradi wa Benki na kuwa katika kamati ya watu kumi waliokua wanaisimamia hiyo project. Kulia ni Askofu Mkuu wa Kanisa la KKKT, Dkt. Alex Malasusa.

Makamu wa Rais  Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi Cheti, Mchungaji, George Fupe, ambaye ni mmoja kati ya waanzilishi wa benki hiyo na wahamasishaji kwa watu kununua shea katika benki hiyo. Kulia ni Askofu Mkuu wa Kanisa la KKKT, Dkt. Alex Malasusa.

Waziri Mkuu mstaafu Lowassa aendelea kulia na kiwango duni cha elimu

Waziri Mkuu mstaafu Edward Lowassa
Waziri Mkuu mstaafu, Edward Lowassa, ameelezea kusikitishwa kwake na kiwango duni cha elimu katika shule za sekondari za kata na katika baadhi ya vyuo vya elimu ya juu.

Akizungumza katika harambee ya kuchangia mfuko wa elimu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Usharika wa kijitonyama jijini Dar es Salaam jana, Lowassa alisema, kiwango cha elimu katika shule hizo kinamsikitisha kwani ni cha chini.

Lowassa ambaye pia ni Mbunge wa Monduli (CCM) allisema: ”Napenda niseme wazi kuwa kiwango cha elimu katika shule zile za kata na baadhi ya vyuo vikuu kwa kweli ni vya chini, hili mimi linanisikitisha sana kwa sababu elimu bora ni mkombozi kwa mtoto wa Kitanzania.

” Hata hivyo alipongeza kanisa kwa kusaidia juhudi za Serikali katika kuimarisha na kuboresha elimu na kusababisha shule nyingi za kanisa kuwa na kiwango bora cha elimu.

Lowassa alisema baadhi ya watu wamekuwa wakisema mambo mbalimbali kutokana na kusindikizwa na marafiki zake katika harambee kadhaa na kumuunga mkono kwa kuchangia. Alitoa kauli hiyo baada ya mmoja wa marafiki zake ambaye ni wakili maarufu, Sadock Magai, kuwasilisha michango ya marafiki wa Lowassa katika harambee hiyo ambao walichangia Sh. milioni 50.

Miongoni mwa marafiki zake waliomchangia ni Lawrance Masha, Innocent Macha, Bashir Awale, Hamis Kindoroko na  Lemmy Bathelemew.

Aidha, walikuwapo Mbunge wa Segerea ambaye pia ni Naibu Waziri wa Kazi na Ajira, Makongoro Mahanga aliyechangia Sh. millioni tatu na Mbunge wa Kinondoni, Idd Azan, aliyechangia Sh. millioni mbili.

Lowassa alimpongeza Azan kwa kuchangia bila kujali Imani yake ya kidini. ”Nampongeza na kumshukuru sana Mheshimiwa Idd Azan kwa kuja kwake kunisindikiza na kuchangia, hii ndiyo Tanzania ninayoijua, isiyo na dini, watu wa dini zote mnashirikiana,” alisema Lowassa.

Katika Harambee hiyo, jumla ya Sh. millioni 615 zikiwa ni fedha tasilimu pamoja na ahadi zilipatikana na kuvuka lengo ambalo lilikuwa Sh. milioni 250.

Source: NIPASHE