Mwimbaji wa Kundi la The Voice Jijini Dar es salaam apata Ajali

Obedi John Mark Mwimbaji wa kundi la The Voice linaloundwa na vijana watano amepata ajali jana usiku majira ya saa tatu maeneo ya Sinza Kamanyola, akiwa anatumia usafiri wa bajaji. kupitia ukurasa wao wa Facebook kundi hilo limetujulisha hivi;-''Mwimbaji mwenzetu Obedi John Mark amepata ajali maeneo ya Sinza Kamanyola, akiwa na usafiri wa bajaji akiwa anaelekea Magomeni...Kwa sasa hali yake si nzuri yuko chini ya uangalizi wa Daktari Mvungi ndani ya Hopitali ya Kinondoni na ameumia sehemu za Kichwa, wapendwa tuzidi kumuombea apone haraka''.


Obedi Mark katika pozi.
Aidha mwana blogger mwingine unlce jimmytemu kupitia blog yake amefanya mazungumzo na mdogo wake Obedi nakueleza kuwa hali yake sio nzuri amepata michubuko kwenye Mikono Miguu na sehemu za uti wa mgongo.Kwa sasa yupo hospital Muhimbili.
Gospel Vision inamtakia afya njema Obedi Mungu ahusike katika matibabu yake, tungependa kumuona akijumuika na wenzake katika huduma ya kumwinua Kristo.AMEN

The Voice

No comments:

Post a Comment