Waimbaji wa Tamasha la Pasaka Dar watambulishwa.

Katika Kuelekea Tamasha la Pasaka mwaka 2013 baadhi ya waimbaji kama Upendo Nkone na Boniface Mwaitege wamesema Tamasha la mwaka huu wamejipanga vilivyo kufikisha ujumbe wa Neno la Mungu kwa watakaojitokeza siku ya tamasha hilo katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Upendo Nkone mbele ya waandishi wa habari
Wakizungumza na waandishi wa habari, Nkone alisema inaonekana ana wapenzi wengi zaidi  katika nyimbo za  kumtukuza mungu ndio maana wamemchagua kupitia ujumbe mfupi wa simu za mkononi, hivyo ana deni la kuwalipa siku hiyo.

“Nimepata furaha kwa waamini kutambua kazi yangu, ndio maana na mimni najihisi nna deni, na nawaahidi kuimba wimbo mpya siku hiyo ambao “Nimebaki na Yesu” ambao unachochea ibada kwa waamini,” alisema Nkone.

Mkurugenzi wa Msama Promotions Alex Msama
Nkone alisema uimbaji wa nyimbo za injili ni mgumu iwapo utafanya vibaya na jamii pia itakukataa ambako pia waamini wanatakliwa kuisoma biblia na kuielewa sambamba na kumuomba mungu kwa dhati ya kweli.

Naye Mwaitege alisema amefurahi kupata bahati ya kuwa mmoja wa wahudumu wa neno la Mungu siku hiyo kwa  sababu tamasha la mwaka jana hakupata bahati ya kushiriki kwa sababu alikuwa safarini nchini Kenya.

“Mwaka jana nilitamani kuimba pamoja na Rebecca Malope lakini bahati haikuwa yangu, ingawa nimepata bahati ya kuimba na Sipho Mwakabane ambaye naye anatokea Afrika Kusini kama Malope na Watanzania wenzangu kama akina John Lissu, Upendo Kilahiro na Rose Muhando,” alisema Mwaitege.

Aidha Mkurugenzi wa Msama Promotions ambao ni waandaaji wa tamasha hilo, Alex Msama alisema siku ya Tamasha utafanyika uzinduzi wa albam ya kundi la Ambassodor of Christ ‘Kuweni Macho’ ambayo itauzwa siku hiyo.

Tamasha hilo ambalo litafanyika pia katika mikoa ya Mbeya Aprili Mosi, Iringa Aprili 3, Aprili 6 mkoani Dodoma na Mwanza Aprili 7.
Viingilio katika tamasha hilo kwa VIP ni shilingi 50,000, Viti maalum shilingi 10,000, Viti vya kawaida 5000 na watoto shilingi 2000.
Mgeni rasmi katika tamasha hilo ni Waziri Mkuu, Mizengo Pinda

Boniface Mwaitege
kwa hisani ya fullshangweblog.com

No comments:

Post a Comment