Askofu mpya wa Kanisa la Anglikan duniani atawazwa.

Justin Welby, Askofu Mkuu wa Kanisa la Anglikan duniani
Askofu Mkuu Justin Welby ametawazwa rasmi kuwa Askofu Mkuu ,Kiongozi huyu wa umri wa miaka 57 ameapishwa rasmi kuwa mkuu wa Kanisa hilo na kiongozi wa kiroho wa jamii ya waumini millioni 77 wa kianglikana duniani.

Katika ibada yake ya kwanza alisema kuna kila sababu ya kuwa na matumaini mema kuhusu mustakbali wa imani ya kikristo katika dunia yetu

"Kuna kila sababu ya kuwa na uhakika wa kuendelea kwa imani ya kikiristo hapa duniani na nchini mwetu."

Waziri Mkuu wa Uingereza David Cameron na mrithi wa kifalme ni miongoni mwa wageni elfu mbili walioalikwa katika kanisa kuu la Canterbury.

Askofu Mkuu Welby aliwaambia : "changamoto zinazotukabili sasa za mazingira,uchumi maendeleo ya mwanaadamu na umasikini duniani ,zinaweza tu kukabiliwa na ushujaa kamambe uliokombolewa na ukristo.

Kwa mujibu wa utamaduni askofu alibisha mara tatu kabla ya kuingia ndani ya kanisa kuu. Alikiri kwamba watu huenda wakatofautiana kuhusu majukumu ya dola na mtu binafsi katika jamii yenye ufanisi.


Mwaandishi wa BBC wa maswala ya kidini , Robert Pigott, anasema Askofu mkuu mpya anarithi kanisa lililoshuhudia kupungukiwa na idadi ya waumini wanaohudhuria ibada katika miaka ya hivi karibuni na ambalo linajitahidi kuhubiri ujumbe wa ukristo katika jamii inayozidi kuonyesha kutotilia maanani maswala ya kidini .

Itachukuliwa kama ni jukumu lake kuliunganisha kanisa ambalo limekumbwa na migogoro kuhusu maaskofu wanawake na pengine hatari zaidi maswala ya ujinsia,Kwa mara ya kwanza katika historia ,Mwanamke Mchungaji Sheila Watson, ambae ni mkuu wa Mashemasi wa Canterbury alishiriki katika moja ya hatua mbili za kutawazwa askofu mkuu.

sourece:bbc swahili

No comments:

Post a Comment