Viongozi wa Dini wakutana Arusha kwa ajili ya kuomba Amani kwa Nchi za EAC

Viongozi wa dini wakiwemo wachungaji zaidi ya 400 kutoka katika nchi za Jumuiya ya Afrika ya Mashariki wamekutana Jijini Arusha katika Kongamano  kwa ajili ya kujadili mambo mbalimbali ya uongozi wao pamoja na kuombea nchi hizo amani hasa ya Nchi ya Kenya na Tanzania.

 Akiongea na chanzo kimoja cha habari jana mratibu wa kongamano hilo ambalo limeandaliwa na mtandao wa wachungaji mkoa wa Arusha,alisema kuwa kongamano hilo lina manufaa makubwa sana kwa Nchi hizo

 Ayo alisema kuwa amani ya nchi inatakiwa ipite hata kwa viongozi wa dini kwa kuwa wao wana nafasin kubwa sana ya kuweza kuhubiri amani tofauti na viongozi wengine wowote hivyo basi mtandao huo umechukua nafasi hiyo kwa ajili ya kuhakikisha kuwa nchi hizo zinakuwa na amani

 Alisema kuwa wachungaji hao zaidi ya 400 ambao wamekutana Jijini Arusha wameweza kujadili mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na hata jinsi ya kulinda amani ambayo baadhi ya Nchi imepotea kwa sababu mbalimbali hivyo kupitia kwa waumini wao wataweza kuwafanya wananchi walinde amani

 “Tumekutana hapa kuhakikisha kuwa tunajadili mambo mbalimbali ya msingi lakini pia kuhakikisha kuwa kila Kiongozi anakuwa balozi wa kulinda amani na wala sio kwenye serikali kwani sisi Viongozi wa dini tuna nafasi kubwa sana ya kutekeleza suala hilo ambalo wakati mwingine tunaachia Serikali pekee’aliongeza Ayo

 Mbali na hayo aliwataka Viongozi wa dini kuhakikisha kuwa wanajiwekea utaratibu wa kuhakikisha kuwa mbali na kuomba amani kwa nchi husika lakini watumie nafasi mbalimbali ambazo wanazo kwa kuwataka waumini wao waweze kufanya kazi kwa bidii na kisha kupambana na Umaskini

 Alifafanua kuwa kama Viongozi wa dini wataweza kufanya hivyo basi wataweza kuondoa Mataifa ya jumuiya ya Afrika ya Mashariki hususan Tanzania kutoka katika  hali ya umaskini ambayo ipo na kufika katika viwango vya hali ya juu ambapo hata hali ya ugumu wa maisha wakati mwingine inachangia sana uharibifu wa amani, pamoja na umaskini.

 “Kwa sasa kuna changamoto kubwa sana za masuala ya kimaisha lakini viongozi wa dini wanatakiwa kuhakikisha kuwa wanaweka utaratibu wa kusisisitiza watu wahakikishe kuwa wanafanya kazi na waache kukaa kaaa ovyo mitaani na pindi wanapokaa mitaani ndipo wanapofanya na kuwaza hata mbinu za kuharibu amani’aliongeza Ayo

Source: fullshangweblog.com

No comments:

Post a Comment