Tamasha la Wakongwe wa Mziki wa Injili Nchini.

Siku ya Jana katika Ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es salaam lilifanyika tamasha la wakongwe wa muziki wa injili nchini,  tukio lilifanyika kwa kuhudhuriwa na waimbaji mbalimbali, viongozi na wakazi wa jiji la Dar es salaam na vitongoji vyake bila kusahau wengine waliotoka nje ya jiji hilo.

Ambapo licha ya uimbaji pia mwandaaji wa tamasha hilo aliweza kuwatunukia vyeti waimbaji hao kwa mchango wao mkubwa katika kumwinua Kristo kupitia uimbaji wao, aidha mwandaaji huyo amesema kuna changamoto nyingi ambazo wamekutana nazo katika uandaaji wa tamasha hilo ikiwemo kutaka kushitakiwa na baraza la sanaa nchini(BASATA) kutokana na kuandaa tamasha hilo la kuwatunuku vyeti wakongwe nchini.

Kwa upande wa mke wa Waziri wa uchukuzi nchini Linna Mwakyembe amechangia katika Tamasha hilo shilingi laki tano kwa ajili ya waimbaji wakongwe pamoja na hayo pia ameeleza kuwa Bwana Yesu ni Bwana na mwokozi wa misha yake ,sambamba na kumshukuru Mungu kwa kumtendea mambo mengi katika misha yake,tazama baadhi ya picha za tukio hilo.










Source:gospelkitaa.blogspot.com

No comments:

Post a Comment