AFLEWO (Africa Lets Worship) 2013 Kenya



AFLEWO An interdenominational prayer and worship event whose theme is “Re-establishing Kenya to GOD” will be going down this Friday 31st May from 4pm-6am at the ultra-modern Winners Chapel auditorium on Likoni Road off Mombasa Road.

The event shall be held on the eve of Kenya;s 50 years of independence known as, ‘Madaraka’ Day.
AFLEWO, which is in its 9th year, inspires belief in Kenya and Africa through its vision, ‘To stir up hope in Jesus across Africa through annual events of worship in Music and Prayer by 2017’.

This year’s event will bring together over 20,000 people and leaders representing diverse backgrounds in prayer and worship led by a 700-voice choir drawn from all AFLEWO local chapters in Nakuru, Mombasa, Nyeri, Meru and Nairobi.

This event will feature prayers and declarations over the key ‘mind shapers’ of a nation led by various men and women representing these areas which are: government, media,
business, family, education, sports, science and technology and the
church.


AFLEWO 2013 is a special event unlike previous AFLEWO events. AFLEWO is excited to have more than 15 hours of worship for the first time in 9 years. The AFLEWO 2013 vision involves the government in leading the nation in prayer as we celebrate 50 years of independence.As a result of Madaraka Day celebrations on 1st June, 2013, AFLEWO 2013 will commence at 4 p.m.(guests to be seated by 2 p.m.) led by the government.

Usikose Drum Stick with Christ


Askofu Mkuu Dk. Barnabas Mtokambali,Roho ya Mpinga Kristo imeingia Tanzania

Kanisa la Tanzania limeitwa kusimama imara na kuchagua njia salama ya kuelekea, wakati huu ambao roho ya Mpinga Kristo imeingia nchini na kusababisha mateso makali, na hata mauaji ya watu wasio na hatia.

Katika hotuba yake kwenye ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Idara ya Maandiko na Uanafunzi, ya Kanisa la Tanzania Assemblies of God, Askofu Mkuu wa Kanisa hilo, Dk. Barnabas Mtokambali alisema kuwa, kwa sasa roho ya Mpinga Kristo inatenda kazi nchini na ndiyo iliyosababisha Watanzania kuingia katika orodha ya wale wanaoteswa duniani.

“Hii si mara ya kwanza, kanisa la kwanza liliwahi kuingia katika mateso makali na maangamizi, ukisoma Biblia katika kitabu cha Matendo ya Mitume, unaona hatua kadhaa za kanisa lilipopitia katika mateso na hatua ambazo lilichukua hata kuishinda,” alisema kiongozi huyo.

Akichukua tahadhari kubwa, Dk. Mtokambali alisema kuwa, roho ya mpinga Kristo ilishaangamiza Ukristo katika mataifa kadhaa ambayo awali yalikuwa ni ya Kikristo kwa asilimia 80 hadi tisini lakini sasa umefutika.

Alitaja baadhi ya mataifa ambayo Ukristo umemalizwa kuwa ni pamoja na Misri, Tunisia na Lebanon, ambayo sasa asilimia 80 ya watu wake sio Wakristo tena.

Huku akinukuu maandiko ya Biblia kutoka katika vitabu vya Matendo ya mitume na Yohana, alisema kuwa kanisa la kwanza lilipoingia katika mateso kama lilivyo kanisa la Tanzania, halikukimbilia siasa wala harakati, bali lilipiga magoti na kumuabudu Mungu wa mbinguni.

“Naliita Kanisa la Tanzania kuachana na siasa, kuachana na mambo ya harakati lichukue hatua ile ambayo kanisa la kwanza, lilichukua. Kanisa lidumu katika maombi kwa kuwa masuala haya ni ya rohoni, hatuwezi kuyashinda kwa njia nyingine yoyote,” alisema Askofu na kuongeza:

“Mateso ya kanisa hayawezi kupata suluhu kutoka kwa mawanadamu, hatuwezi kupata msaada kutoka kwa Mbunge, chama cha siasa au mabadiliko ya uongozi…..msaada wetu watoka mbinguni tu. Kwa kutambua hilo nimeagiza maombi ya mwaka mzima ili kukabiliana na roho hii ambayo inataka kuufuta Ukristo kabisa kwenye sura ya nchi.”
Alisema, swali kubwa analojiuliza ni hatua gani Kanisa la Tanzania linachukua baada ya kuwa sasa limeingia katika mateso?
“Ikiwa Kanisa la Tanzania litachukua hatua zilizochukuliwa na kanisa la kwanza, ninahabari njema kwao kuwa Mungu atalitetea kama alivyowatetea mitume waliokuwa kwenye mateso,” alisema kiongozi huyo.

Alinukuu maandiko kutoka Matendo ya Mitume 12:12, huku ujumbe wake ukiwa na kichwa; Utendaji wa Mungu kutuokoa.

Kiongozi huyo alisema kuwa, wanasiasa wanamtazamo wao, wanaharakati wana mtazamo wao, lakini kanisa linapaswa kuwa na mtazamo wa kiroho katika kipindi chote cha mateso yake.

Alisema kuwa, historia inaonesha kuwa wakati wote ambao kanisa liliiingia katika mateso likamgeukia kristo ulitokea uamsho mkubwa, hivyo hata wakati huu ambao kanisa la Tanzania linateswa, ni vyema likachukua hiyo kama fursa ya kuamka na kuhubiri Injili kwa nguvu zote.

“Nasema tena, usalama wa Tanzania upo kanisani tu, kanisa likilala amani haitakuwepo, usalama hautakuwepo, naliita kanisa liamke na kuingia katika maombi marefu bila kuchoka,” alisema.

Tamasha la Uimbaji KKKT usharika wa Segerea


Katika kuelekea Dini moja Tangazo la hatari latolewa.

Aprili 25, mwaka huu dunia ilipiga hatua kubwa katika safari ya kuelekea kwenye serikali moja, dini moja na sarafu moja,  wakati viongozi zaidi ya 300 walipofanya maamuzi magumu  na kutoa kile kinachoelezwa kuwa ni tangazo la hatari.

Kwa kauli moja, baada ya kujadili kwa kina, wakala pamoja na kunywa pamoja, viongozi hao walitoa azimio linalosomeka:“Sisi, washiriki 300 kutoka zaidi ya nchi 70 za mabara sita, tukijumuisha Wayahudi, Wakristo, Waislamu  ni miongoni mwa dini zilizokutana Doha Ritz Carlton kwa ajili ya kongamano kubwa linaloandaa maisha bora zaidi ya mwanadamu kuishi. Tunaiandaa dunia kuwa kisiwa kimoja chenye muelekeo mmoja tukiabudu pamoja ......”

Pamoja na mambo mengine zingatia maazimio ya kuwa wamoja kuishi pamoja na kuabudu pamoja.
Hebu jiulize ni vipi Waliookoka (Pentekoste) Waislamu, wabudha, wapagani  na waabudu shetani wataabudu pamoja kwa umoja?

Ni Mungu yupi anayekubaliana na dini zote hizo zenye mielekeo na misingi tofauti? Usistaajabu kwa kuwa wakati umefika na viongozi hao isipokuwa Wapentekoste, aliendelea kutamka hivi:
 “ Katika Kongamano letu lililodumu tangu Aprili 23 hadi 25, 2013 tunasema kuwa, tunatambua ukarimu wa  Sheikh Hamad Bin KhalifaAl-Than, na watu wa Qatar walioshirikiana na waandaaji wa kongamano hili, Wizara ya mambo ya kigeni na Chuo kikuu cha Qatar.”

Kabla ya kufikia maazimio, uongozi wa kongamano chini ya uenyekiti wa  Dk. Aisha al-Mannai, Dk. Ibrahim al-Naimi na Waziri wa Sheria,  Mheshimiwa  Hassan Bin Abdulla Al-Ghanim, waliwakaribisha washiriki na kuwataka kuzingatia mapendekezo yaliyomo kwenye dhima ya kongamano isemayo `Mwenendo bora katika mjadala wa mambo ya imani.

Miongoni mwa maazimio yaliyofikiwa katika kongamano hilo ni pamoja na kuhakikisha  kuwa somo la ushikiano wa upendo, ukilenga katika dini moja na kumuabudu Mungu mmoja na fundisho moja la dini linafundishwa kwa kila taifa kabila na lugha.

Njia za siri zilizokubaliwa kutumika katika promosheni ya hiyari ni pamoja na misaada zaidi kwa mataifa yatakayoitikia na kuanza kufundisha  somo la dini moja ukiwa ni mtaala rasmi utakaotumika kwenye mashule yote duniani.
Kuondoa tembo zenye kuleta ubaguzi wa miungu, kama vile mavazi ya dini, kama misalaba, hijab  na mengineyo na kufuata vibao vya amri kumi za Mungu au mikutano ya maombi yenye kubagua wengine.\
Pamoja na maamuzi ya siri, maamuzi ya wazi ni pamoja na kuimarisha taasisi ya Interfaith  kila nchi na kusimamia  mpango wa ibada za pamoja ili kuwazoezesha watoto wa kizazi kipya kushirikiana katika ibada.

Wachunguzi wa mambo ya imani wanaeleza kuwa maamuzi ya mkutano wa Doha ambao ni wa 10, tangu taasisi hiyo ianze kukutana katika taifa hilo la kiislamu kama kituo chake rasmi ni hatari kuliko mengine yote yaliyowahi kufikiwa.

Baadhi ya viongozi wenye kuhemika sana katika ulimwengu wa dini walihudhuria mkutano huo,  isipokuwa Wapentekoset ambao wanaamini kuwa ushirika huo ni wa kuandaa kiti cha Mpinga Kristo anayetajwa katika Bibilia kwenye kitabu cha Ufunuo 13.

Katika maadhimisho ya  kumi ya Kongamano  hilo la  imani zilitolewa tuzo maalumu kwa  wale waliostahili kutunzwa , tuzo hiyo inaitwa “Doha  International Award for Interfaith Dialogue 2013”.  Kati ya waombaji 150 kutoka kwa watu binafsi na mashirika kutoka kila kona ya Ulimwengu, tuzo ilimwendea  Dk. Muhammad al-Sammak ambapo watu watatu binafsi na mashirika matatu nao pia walitajwa kipekee kama waliostahili  shukrani kwa mchango wao kuhusiana na kongamano hilo na kufikia mafanikio hayo.

Katika kipindi maalum  baada ya uzinduzi, washindi wote wa tuzo kutoka  Lebanon, Bosnia, Marekani, Morocco na Kanada  walibadilishana uzoefu wao na washiriki wa kongamano hilo.
Kongamano lilikuwa na vipengele vikubwa vinne:

Katika kipindi cha Taaluma, ilijadiliwa kuwa  wanafamilia wana wajibu mkubwa katika kuwakuza vijana katika misingi ya roho hiyo ya Interfaith. Vyuo vikuu na Mamlaka za Elimu kwa ujumla wanahimizwa kuingiza mtaala wa imani moja katika mfumo wao na inapaswa kufundishwa kuanzia ngazi ya familia. Ilihimizwa kuwa watafiti kutoka taasisi za elimuya juu watanufaika wakifanya kazi zao kwa ukaribu na  mashirika ya Interfaith, lengo likiwa kuendeleza mihadhara ya Interfaith duniani kote na kila mtu lazima ielimishwe kwanza kabla ya kushurutishwa ikibidi.
Sheria
Wazungumzaji katika kipengele cha sheria walizungumzia mambo muhimu ya kuanzisha sheria za kijamii, ,kiuchumi na kitabibu katika ngazi mbalimbali za miji kwa mtazamo wa ushirikiano kidunia na Umoja wa Mataifa kwa dhana ya kinga- miongoni mwa haki nyingine mbalimbali.
Walisisitiza kuwa na chombo cha umoja wa taasisi wa kisheria kama chombo chenye kushirikisha dhana na kuhudumia watu wa imani zote. Waislamu, wakristo na wayahudi watashikamana pamoja katika kutafuta njia bora za kupiga vita umaskini, ambapo watu wengi hawaelewi chochote juu ya hili.
Umoja kama huu unapaswa kushereheshwa, ili kwamba umma uelewe umuhimu wao katika mambo yenye kujenga. Kongamano la Doha linaweza kuifanya kazi ya kukuza ushauri wa kisheria wa pamoja kwa ajili ya masualaya kisheria ya siku za usoni.
Utatuzi wa migogoro na Amani

Taarifa zote zilizitaka jumuiya zote za Interfaith kuendelea kushirikiana  kwa dhati ili kupata uwanja wa pamoja katika kufanikisha kuunda jumuiya za kisheria kwakuwajengea uwezo viongozi wa kidini na kijamii ili kuushinda mgawanyiko uliopo sasa.
Wale wanaoshjindania mambo ya kijinga watakandamizwa kwa hoja ili kukubali kukaa pamoja na kujenga dunia moja yenye ladha moja na yenye kuheshimu utu wa mtu.
Tamaduni za vyombo vya habari

Kongamano limeona kuwa mwingiliano wa vyombo vya habari katika maisha  ya kila siku, hasa  katika karne moja iliyopita ni dhahiri kwamba vimekuwa msaada mkubwa katika jamii inayotuzunguka, kutokana na nguvu iliyopo katika vyombo hivyo, lakini pia vimekuwa mchango mkubwa katika kuinua mambo mbalimbali.

Hivyo kuna haja ya kuwa na utamaduni moja wa kuchambua mwenendo wa vyombo hivyo na promosheni maalumu kwa wale watakaitazama ineterfaith kwa jicho  chanya.Inaamini kuwa hizo ni harakati za mwisho kabisa katika kuelekea kumpata mpinga Kristo atakaye usuka suka ulimwengu akiulazimisha kumuabudu. Tayari idadi kubwa ya makanisa yametia sahihi  mkataba wa kuundwa kwa umoja wa kidini.

Waziri Mkuu Msaafu Sumaye akemea udini na ufisadi

Waziri Mkuu Mstaafu, Frederick Sumaye, amekemea harakati zinazoendelea nchini za kutaka kupandikiza mapambano ya kidini, ufisadi na kuwataka wasomi kuacha kusononeka na badala yake wachape kazi huku wakieneza amani.

Akihutubia jana katika harambee ya kuchangia kanisa la Chuo Kikuu cha Iringa, kinachomilikiwa na Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Iringa, Simaye aliwafunda wasomi wa chuo hicho akiwataka watumie nafasi waliyonayo kwa ajili ya kueneza amani na kuachana na masikitiko yasiyokwisha yanayotokana na  baadhi yao kutojituma katika kazi.

Alisema maandiko matakatifu ya Bibilia yanaeleza kwamba rushwa na ufisadi ni dhambi kubwa katika taifa na kuonya kwamba dhambi hiyo ikilelewa inasababishia matatizo makubwa.

Alisema kaburi pekee la mambo machafu ni ujenzi wa kanisa hilo na matumizi yake kutumika kwa malengo ya kuhubiri amani na kukemea ufisadi.

"Mfano ni nani kati yenu amepata kutozwa rushwa na mkulima? Rushwa inatozwa na wenye nafasi na hivyo lazima vijana wasomi mkimaliza hapa muende kubadilisha taifa .... ndiyo maana nilipoitwa na baba askofu kwa ajili ya harambee ya kanisa nikasema nitafika kwani ni jambo jema," alisema Sumaye.

Bila kutaja jina, Sumaye alisema kumshangilia mtu anayeendesha gari la kifahari kwa kulipata kwa njia ya wizi ni hatari.

Alisema hivi sasa watu wanajenga chuki kati ya wanyonge na matajiri na kuwa hivi sasa limezuka jambo baya zaidi kwa watu kuchukiana kwa misingi ya dini zao na kuwa  nchi yeyote itakayoingia katika machafuko ya imani ni hatari.

Sumaye alisema vita ya kiimani ni mbaya zaidi. “Na siku zote vita hiyo huwa haina mshindi hivyo ni vema kila dini kuanza utaratibu wa kuwafundisha vijana wake ili kuwa na uzalendo katika taifa hili.”

Aidha,  alisema mapambano ya dini yanayoendelea mbali ya kutokuwa na mshindi, hata vita nayo haitakuwa na mshindi na hivyo ni vyema kila mmoja kuachwa akiendelea kuamini kile ambacho ana amini hata kama ni chini ya mti na kuwataka Watanzania wasiruhusu vita hiyo kupandikizwa.

Sumaye alisema anafurahishwa kuona nyumba za ibada zinaendelea kujengwa na hivyo ni imani yake kuwa zitasaidia kuhubiri amani na utulivu pamoja na uzalendo miongoni mwa Watanzania.

Mbali ya Sumaye, harambee hiyo pia ilihudhuriwa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Christine Ishengoma pamoja na Mbunge wa Iringa Mjini (Chadema), Mchungaji Peter Msigwa.

Wafungwa wamsifu na kumuabudu Mungu

Waswahili husema historia hujirudia, hilo lilijidhihirisha hivi karibuni baada ya wafungwa wa gereza la vijana kusahau shida zao wakaruka ruka wakimsifu na kumuabudu Muumba wao kwa kicho na kububujika machozi, kama walivyofanya akina Paulo na Sila.

Hayo yalijitokeza hivi karibuni katika Kanisa la TAG Wami eneo la Gereza la vijana, Kilosa mkoani Morogoro, ambapo wafungwa walipata fursa ya kufika kwenye Ibada na kushiriki kikamilifu vipindi vyote, huku wakisindikizwa na Askari; ambapo pia walipewa nafasi ya kuimba nyimbo zilizosisimua waumini na kushangiliwa.

Miongoni mwa nyimbo zilizosisimua ni ile ya ‘Majaribu ni mtaji na wa kuinuliwa ni Mungu, wimbo uliowafanya baadhi ya washirika kusimama na kuanza kushangilia.

 Vijana hao walionekana kufunzwa vyema, kwani licha ya kuwa ni wafungwa, lakini walionyesha nidhamu ya hali ya juu wakati wote walipokuwa kwenye Ibada, kitu ambacho ni sehemu ya haki zao wapatazo wanapokuwa kifungoni.

Sula la wafungwa kumkumbuka Mungu wao na kuimba nyimbo za kuwatia moyo waumini linafananishwa na tendo la Mtume Paulo aliyeandika Nyaraka kadhaa akiwa gerezani za kuwapa moyo waumini waliokuwa wakipitia mateso mbalimbali.

Kadhalika wafungwa hao walipata fursa ya kusikiliza semina kuhusu Roho Mtakatifu, iliyoendeshwa na Walimu kutoka Kanisa la TAG Ubungo Christian Centre, la jijini Dar es Salaam, baadaye waliombewa ujazo wa Roho Mtakatifu pamoja na waumini wengine wa kanisa hilo.

Mchungaji Wilbald Ulomi, wa Kanisa hilo, mwisho wa ibada hiyo aliwashukuru wote waliohudhuria, ikiwa ni pamoja na walimu waliotoka Dar es Salaam.

Ungana na Ask.Dk. Mtokambali kutembelea Maeneo matakatifu ya Israeli

Askofu Mkuu wa Kanisa la Tanzania Assemblies of God (TAG), Dk. Barnabas Mtokambali
Askofu Mkuu wa Kanisa la Tanzania Assemblies of God (TAG), Dk. Barnabas Mtokambali, ataongozana na kundi la Maaskofu, Wachungaji pamoja na Wakristo kutoka sehemu mbalimbali nchini Tanzania, kwenda Israel  kutembelea  na kushuhudia kwa macho maeneo matakatifu yaliyoainishwa kwenye Bibilia. Safari Septemba  23, Mwaka huu 2013.

Iwapo unapenda kuambatana nao  tafadhali jiandikishe mapema, kwani nafasi zimebaki chache na wenye kiu ya safari hii ya kihistoria ni wengi .

NANURI SAFARI COMPANY LIMITED ndiyo itaratibisha safari hiyo.Gharama ya safari ni Dola  za Marekani 2700  zikibeba gharama zote za safari ambazo ni:-(1)    Usafiri wa ndege kwenda na kurudi (2)    Chakula(3)    Malazi(4)    Viza(5)   Malipo ya kuingilia maeneo tutakayotembelea (entrance fees)
(6)Usafiri wa gari tutakalotumia huko Israel.
Tuma fedha katika: NANURI SAFARI COMPANY LIMITED
NMB – ILALA BRANCH
ACCOUNT NO: 2036600111
DAR ES SALAAM.
Ukiwa na swali lolote usisite kutuuliza kwa namba zifuatazo:
0715 – 640 777; 0782 – 640 777; 0716 – 316 109
au Fika katika Ofisi zetu zilizopo Mwalimu House ghorofa ya 6, Ilala Boma, jijini Dar es Salaam.

KUMBUKA NAFASI NI CHACHE SANA WAHI SASA.

Semina ya Neno la Mungu na Askofu Emmanueli Lazaro


Askofu Emmanuel Lazaro aliyekuwa Askofu Mkuu wa kwanza wa Tanzania Assemblies Of God kwa zaidi ya miaka 26 anaedelea na semina ya Neno la Mungu katika Kanisa la TAG  Ubungo ilipo makao makuu ya Kanisa la TAG Semina hiyo imekuwa ikiendelea mpaka sasa na kuhitimihswa kesho kanisani hapo.

Semina hiyo iliyoanza siku ya jumatano tarehe 8 mpaka siku ya kesho tarehe 12.Watu wote wagonjwa na wenye shida mbalimbali wanaombewa.

Watu Wote Mnakaribishwa katika Semina hiyo inayoendelea leo kuanzia Saa 10 Kanisani hapo mpaka siku ya Jumapili, Njoo uone Udhihirisho wa Nguvu za Mungu Kupitia Neno lake.


Askofu Emmanuel Lazaro aliyekuwa Askofu Mkuu wa kwanza wa Tanzania Assemblies Of God
 

Waliofariki katika Mlipuko wa Bomu Kanisani Arusha wazikwa

Misa ya Mazishi ya wahanga wa mlipuko wa bomu la Jumapili iliyopita kwenye parokia teule ya Olasiti ilianza katika eneo lile lile mlipuko ulipotokea siku ya jana Jijini Arusha.Misa hiyo iliongozwa na Muadhama Polycarp Kardinal Pengo, Askofu Mkuu wa Dar es Salaam.

Maandamano yalianzia toka chumba cha kuhifadhia maiti, miili ikapelekwa makao makuu ya Asofu Mkuu, Burka na baadaye ikawasilishwa kanisani

Kardinali Pengo alisema Ndugu zangu nafasi hii inaunganisha mawazo ya furaha na uchungu kutokana na kilichotukutanisha leo,mazingira haya yanaweka ugumu wa kupata cha kusema.Ila sisi ni watu wa imani. napenda kueleza imani yetu kama tunavyopaswa kuwa kwenye mazingira haya.

Tumejumuika ili kuwaweka kwenye nyumba ya milele hawa marehemu, lakini pia tunatumia nafasi hii kubariki Kanisa.

Kila mbatizwa ni kiungo cha mwili wa Kanisa. Kila kiungo cha mwili kinapaswa kuungana na kichwa cha Mwili ambae ni Yesu Mwenyewe,Kristo akipitia kwa mdomo wa mtume Paulo anatufundisha kuwa “Msijaribu kushindana na uovu kwa uovu, lakini shindeni uovu kwa wema”.

Nawauliza waumini: “Wale waliotekeleza ubaya huu, akija mbele yetu akasema ni mimi ndiye, tungefanya nini kama waumini kwa kufuata mfano wa Yesu?”

Mimi nawaambia “Tujifunze kutoka kwa Bwana wetu Yesu Kristo: ‘Tusidiriki kulipia uovu kwa uovu, lakini tutende mema ili kushinda uovu’.”

Amemalizia kwa kusema: Tukio hili na tukio la mauaji ya Padre Mushi, isiwe sababu ya kuacha amani ya nchi yetu isambaratike.Lakini ni jukumu la wananchi wotte kuhakikisha nchi yetu haisambaratiki.

Wenye mamlaka watimize wajibu wao.Sisi wakristo tusamehe, tusijibu uovu, tudumishe amani na upendo katika taifa letu,alimaza kwa kusema!



source:arusha-yetu.blogspot.com

Watuhumiwa ugaidi kanisani watajwa

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas
Idadi ya watuhumiwa wa tukio la kulipua bomu katika Kanisa la Mtakatifu Joseph Mfanyakazi, Parokia ya Olasiti, mkoani Arusha Jumapili iliyopita, imeongezeka kutoka tisa hadi 12.

Watuhumiwa hao wametajwa na Jeshi la Polisi kuwa ni Victor Ambrose Kalisti (20) na Joseph Yusuph Lomayani (18), ambao wote ni waendesha bodaboda wakazi wa Kwa Mrombo, mkoani Arusha.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas, akizungumza na waandishi wa habari jijini Arusha jana, aliwataja watuhumiwa wengine wanaoshikiliwa kuwa ni George Batholomeo Silayo (23), ambaye ni mfanyabishara na mkazi wa Olasiti; Mohamed Sulemani Said (38) mkazi wa Ilala, mkoani Dar es Salaam, ambaye polisi imemtaja kuwa ni mwenyeji wa watuhumiwa raia wa Uarabuni na kwamba ndiye aliyewafuata kwa gari binafsi uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es Salaam na kuwachukua hadi Arusha katika hoteli moja iliyoko karibu na kituo kikuu cha mabasi yaendayo mkoani humo na nje ya mkoa.

Wengine wanaoshikiliwa ni Said Abdallah Said (28), ambaye ni raia wa Falme za Kiarabu, katika mji wa Abudhabi; Abdulaziz Mubarak (30), ambaye ni mkazi wa Saudi Arabia; Jassini Mbarak (29), ambaye ni mkazi wa Bondeni Arusha; Foud Saleem Ahmed (28), ambaye ni raia wa Falme za Kiarabu na Said Mohsen, ambaye ni mkazi wa Najran Falme za Kiarabu.

IGP ATOA BINGO YA SH. MILIONI 50
Aidha, Jeshi la Polisi nchini kupitia Mkuu wake, Inspekta Jenerali (IGP), Said Mwema, limetangaza donge nono la Sh. milioni 50
kwa mtu yeyote atakayefanikisha kufichua mtandao wa kigaidi nchini.

Kamanda Sabasi alisema hayo alipokuwa akitoa taarifa kuhusu hatua zilizochukuliwa tangu kutokea kwa mlipuko wa bomu hilo Jumapili saa 4.30 asubuhi kwenye kanisa hilo.

Kamanda huyo ambaye jana alizungumzia tukio hilo kwa mara ya kwanza, alisema siku ya tukio kulikuwa na uzinduzi wa kanisa hilo na mgeni rasmi alikuwa  Balozi wa Vatican nchini, Askofu Mkuu Francisco Padilla, na alipokuwa akijiandaa kukata utepe kama ishara ya uzinduzi, ghafla mtu mmoja aliyejificha kwenye choo cha jirani, upande wa Kaskazini, alirusha kitu kizito.

Kamanda Sabas alisema kitu hicho kilirushwa umbali wa mita 20 na kilikuwa na ukubwa wa ngumi ya mtu mzima, kuelekea kwenye mkusanyiko wa waumini na kilipotua chini ulitokea mlipuko mithili ya bomu na kusababisha watu 66 kujeruhiwa, ambao kati yao watatu walipoteza maisha.

Alisema watuhumiwa hao bado wanaendelea kuhojiwa na tayari jalada la mashtaka dhidi yao limepelekwa kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), kwa ajili ya maamuzi ya kisheria.

Kamanda Sabas alisema uchunguzi wa awali umebaini kuwa bomu hilo siyo la kienyeji na pia wageni hao walikuwa na VISA halali ya kukaa nchini, kwa madai kuwa walikuja harusini.

“Watuhumiwa hawa wa Falme za Kiarabu tulipowahoji, walidai wamekuja harusini, lakini tunaendelea nao,” alisema.

Alisema watuhumiwa watatu wanaendelea kuhojiwa na kwamba kutokana na hali hiyo, majina yao hayawezi kutajwa.

MAZISHI KUFANYIKA LEO
Alisema ulinzi umeimarishwa katika kanisa lilikotokea mlipuko ili kuhakikisha hakitokei kitu chochote kabla na baada ya mazishi ya watu waliuawa na bomu hilo.

Ibada ya mazishi inatarajiwa kufanyika leo saa 2:00 asubuhi kwenye kanisa hilo na itahudhuriwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, na viongozi wa dini mbalimbali, akiwamo Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki Arusha, Josephat Lebulu.

Pia ibada hiyo itaanza kwa maandamano kutoka eneo la Burka kwenye makazi ya Askofu Lebulu hadi eneo la Olasiti kanisani na itahudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali na dini.

HALI ZA WALIOHAMISHIWA MUHIMBILI
Majeruhi saba waliohamishiwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), jijini Dar es Salaam baada ya kujeruhiwa na mlipuko wa bomu hilo, wameanza kupatiwa matibabu.

Akizungumza na NIPASHE jana jijini Dar es Salaam, Ofisa Habari wa Hospitali hiyo, Jeza Waziri, alisema hali za majeruhi, ambao wamelazwa kwenye wodi namba 10 kwenye Jengo la Kibasila zinaendelea vizuri na mara walipowasili walifanyiwa uchunguzi.

“Ni kweli tuliwapokea na mara walipowasili madaktari wetu walianza kuwapatia matibabu, huku wakiangalia jinsi ya kuvitoa vipande vya chuma vilivyopo kwenye miili yao na hali zao kwa ujumla ni nzuri,” alisema Waziri.
Majeruhi hao ni Faustine Shirima, Gabriel Godfrey, Abeid Njau, Jennifer Joaquim, Athanasia Reginald, Fatuma Tarimo na Apolinari Malamsha.

Source Nipashe

Tapeli wa simu alisumbua kanisa Jijini Dar es salaam!

Mtu mmoja  aliyejulikana kwa jina la Grace Ngailo, amekuwa kero kubwa kwa watumishi wa Mungu jijini Dar es Salaam, akijaribu mara kadhaa kuwatapeli kwa kutumia majina yao anayoyakuta kwenye matangazo hasa yale yanayochapwa kwenye magazeti.

Bila haya mhalifu huyo ambaye mara kwa mara amekuwa akibadili simu na kusajili zingine kwa majina tofauti lakini kwa lengo la kutumia simu hizo kwa utapeli, amekuwa akiomba fedha kiasi kidogo akijipachika jina la mtu mwingine na kudai yuko mkutanoni aazimwe fedha atarudisha baadaye.

Kwa Mfano, wiki iliyopita, tapeli huyo alijifanya Mhariri wa Gazeti la Jibu la Maisha, kisha akatuma ukumbe kwa Mchungaji Ray Seng’enge wa Kanisa la Dar es Salaam, International Church, akidai eti Mhariri yuko mkutanoni simu yake ina matatizo hivyo atumiwe kiasi cha Shilingi 50, 000.

Jumbe za aina hiyo zimekuwa zikitumwa kutoka katika jina la mtumishi mmoja kwenda kwa wengine na kwa mara chache tapeli huyo amefanikiwa kujipatia fedha kwa wale wasiojua mchezo huo mchafu unaofanywa na tapeli huyo.

Wiki kadhaa zilizopita akitumia jina la Mhariri huyo tapeli hilo liliweza kujipatia shilingi 30,000 kutoka kwa Mwanasheria wa Kituo cha Sheria na haki za Binadamu Bi. Flaviana Charles. Mwanasheria huyo alipowasiliana naye, alimjibu kwa kiburi kuwa yeye angekula wapi anasumbuliwa na njaa tu.

 Habari kutoka kwa wachungaji mbali mbali jijini Dar es Salaam, zinasema kuwa tapeli huyo amekuwa akitumia majina yao kujaribu kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu na kusababisha usumbufu mkubwa.
Inadaiwa kuwa tapeli huyo pia husikiliza  mahubiri kwenye radio za dini na kusoma matangazo kwenye vyombo vya habari za kikristo ambapo hujipachika cheo cha Mhariri Mkuu na afisa yeyote kuwaomba wahusika kiasi cha shilingi elfu 50 na 30 akidai ana matatizo .

Baada ya matukio hayo kushamiri, uongozi wa Gazeti la Jibu la Maisha liliwahi kutoa taarifa katika kituo kidogo cha Polisi cha Urafiki ambapo mpaka hivi leo watu wanaendelea kutapeliwa na hakuna juhudi zozote ambazo zimefanyika kumkamata tapeli huyo, licha ya kufuatilia kituoni hapo kwa zaidi ya mara kumi na kuahidiwa kuwa wapelelezi wanafuatilia barua kutoka kwa mkuu wa upelelezi, ilikuomba ushirikiano wa makampuni ya simu, kwa lengo la kumfuatilia.

Wananchi wanateswa na tapeli huyo wamestaajabu ni vipi polisi wanashindwa kumkamata mhalifu huyu wakati simu zote zimesajiliwa. Aidha wamemuomba Kamanda wa Polisi wa mkoa wa kipolisi wa wa Mkoa wa kipolisi wa Kinondo Charles  Kenyela, kuingilia kati kuzuia uhalifu huo.

Mwandishi wa Jibu la Maisha alipowasiliana na Kamanda kenyela kwa simu yake ya mkononi alisema, hana taarifa na anaomba yeyote ambaye ametapeliwa kufika kwake na kuandikisha maelezo pamoja na vielelezo vya ushahidi wa jumbe ili mhusika asakwe.

TAG kusherehekea miaka 75 ya uhai wake Tanzania

Kanisa la Tanzania Assemblies of God (TAG) linakusudia kuadhimisha miaka 75 tangu kuanza kwake nchini, sherehe ambazo zitafanyika kitaifa mkoani Mbeya mwakani.

Hayo yalibainishwa na Askofu Mkuu wa kanisa la TAG, Dk. Barnabas Mtokambali, katika uzinduzi wa Mkutano Mkuu wa Idara ya Maandiko na Uanadunzi uliofanyika katika Ukumbi wa mikutano wa Highland Camp Morogoro, Jumatano iliyopita.
Askofu Mkuu wa kanisa la TAG, Dk. Barnabas Mtokambali

Kiongozi huyo wa kitaifa alisema kuwa Halmashauri kuu ya kanisa hilo imeamua kuwa sherehe hizo zitafanyika katika Uwanja wa Sokoine mkoani Mbeya mwaka 2014.

Alisema kuwa maadhimisho hayo yataanzia katika ngazi ya kanisa la mahali pamoja na baadaye ngazi ya Jimbo na fainali itakuwa ni ngazi ya taifa mkoani Mbeya.

Kanisa la TAG, ambalo linaongoza miongoni mwa makanisa ya TAG, kukua kwa kasi nchini linatimiza miaka 75, tangu lianze nchini huku likienea kila mahali kuanzia mijini mpaka vijijini.





“Msitarajie utukufu mnapomtumikia Mungu’

Kumtumikia Mungu si kazi ya heshima mbele ya wanadamu, bali kwa Mungu pekee, hivyo waliojitoa kikamilifu kuingia katika shamba la Bwana wasifanye huduma hiyo wakitaraji mrejeo chanya toka kwa viumbwa.

Hayo yalisemwa na Mchungaji Ismaili Mwipile, wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Ukonga jijini Dar es Salaam, alipokuwa akihubiri katika mkutano wa injili uliokuwa kanisani hapo wiki iliyopita.

Mchungaji Mwipile aliwataka waamini wa dini ya Kikristo kutokukata tamaa pale wanapoamua kuifanya kazi ya Bwana, kwani heshima kubwa inatoka kwa Mungu ikiambatana na thawabu tele.

Aliwaasa waamini kuwa wavumilivu na wasio kata tamaa, wakijitahidi kuondokana na imani haba katika changamoto wanazokutana nazo, huku akifananisha na gereza la vifungo vya mafanikio.

"Paulo na Sila walikaa gerezani, licha ya kupata mateso, lakini walikuwa na imani na Mungu pekee waliyemwamini na ndiye aliyewaweka huru pale milango ya gereza ilipofunguka," alisema Mchungaji Mwipile.

'Waliookoka wako kwenye vita kali’

Mwinjilisti wa Kanisa la Calvary Assemblies of God,   la Matarawe, Songea mkoani Ruvuma,  John Tembo, amewataka Wakristo waliofanikiwa kupata wokovu kutambua kuwa; wapo kwenye vita kali dhidi ya shetani, hivyo wanastahili kusimama imara nyakati hizi ni za mwisho.

 Wito huo alitowa mapema wiki jana, wakati akihubiri katika kanisa hilo, kwenye ibada ya Jumapili iliyokuwa na mguso mkubwa wa nguvu za Mungu, na watu zaidi ya 30 waliitikia wito wa Injili wakayakabidhi maisha yao kwa Yesu, huku waliosetwa na ibilisi wakifunguliwa.

 Mwinjilisti Tembo, alisema kuwa nyakati hizi ni za mwisho kwa mujibu wa maandiko, hivyo ni vema watu wakasimama imara kumuomba Mungu ili awaepushe na majaribu yanayowasonga.

 Alisema, watu wa Mungu waliouona mkono wa Bwana ndio waliopo kwenye changamoto mbalimbali za kishetani, kwa kuwa shetani naye anawatafuta watu kama hao ili awaangamize.

   “Nawaambieni watu wa Mungu katika nyakati hizi za mwisho shetani anafanya kazi ya kushika fahamu za watu wenye uelewa wa Mungu ili kusiwepo na utambuzi wa mambo mema, badala yake yatendeke mabaya,” alisema Mwinjilisti huyo na kuongeza:

 “Kuna baadhi ya watumishi wa Mungu wameshikwa ufahamu na shetani, na ninyi wenyewe mnaona, wanahubiria watu  vitu ambavyo havipo kwenye maandiko na mnamwamini,  ni hatari sana kwa nyakati hizi.”
 Aidha Mtumishi huyo wa Mungu aliwageukia waumini waliookoka ambao wamenunua simu kwa bei mbaya kwa malengo ya kuangalia picha za kishetani zilizopo ndani yake, na kulaani kitendo hicho kuwa ni kinyume na matumizi ya simu.

Maznat mdau wa Blog aadhimisha miaka 10 ya Taasisi yake na Kuzindua shule ya Urembo


 Mke wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Asha Bilal, akiwasili kwenye Ukumbi wa VIP wa Diamond Jubilee, jijini Dar es Salaam jana jioni kwa ajili ya kuhudhuria sherehe za maadhimisho ya miaka 10 ya Taasisi ya Maznat, kama Mgeni rasmi sambamba ya kuzindua Shule ya Taasisi hiyo inayofundisha masuala ya urembo.
Mke wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Asha Bilal, akihutubia wakati wa sherehe za maadhimisho ya miaka 10 ya Taasisi ya Maznat, iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Diamond jijini Dar es Salaam, jana, sambamba na sherehe hizo pia Mama Asha, alizindua rasmi shule ya masuala ya Urembo inayosimamiwa na Taasisi hiyo.
Mke wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Asha Bilal, akihutubia wakati wa sherehe za maadhimisho ya miaka 10 ya Taasisi ya Maznat, iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Diamond jijini Dar es Salaam, jana, sambamba na sherehe hizo pia Mama Asha, alizindua rasmi shule ya masuala ya Urembo inayosimamiwa na Taasisi hiyo.
Sehemu ya wageni waalikwa waliohudhuria sherehe hizo.
Mmiliki wa Saluni na Taasisi ya Maznat, Maza Sinare, akiwalisha keki baadhi ya wageni waalikwa wakati wa sherehe za maadhimisho ya miaka 10 ya Taasisi ya Maznat, iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Diamond jijini Dar es Salaam jana, sambamba na sherehe hizo pia Mgeni rasmi mke wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Asha, alizindua rasmi shule ya masuala ya Urembo inayosimamiwa na Taasisi hiyo.
 Msanii wa muziki wa Injili, Bahati Bukuku, akiimba jukwaani kutoa burudani wakati wa maadhimisho hayo.
The Voice

Ungana na Ask.Lazaro na Mtume Onesmo Ndegi kutembelea Israel

Askofu Mkuu mstaafu wa Kanisa la Tanzania Assemblies of God, Emmanuel Lazaro, akiongoza kundi la viongozi mbalimbali wa makanisa na baadhi ya waumini wanaosafiri kwenda Israeli kutembelea maeneo matakatifu yaliyopo kwenye Bibilia, ambapo pamoja na mambo mengine wataliombea kanisa na nchi kwa ujumla.

Kampuni ya Nanuri Safari LTD inayoratibu safari hiyo ya kihistoria inakukaribisha kujiunga nao ili kukupa fursa ya kipekee ya kushuhudia kwa macho maeneo hayo matakatifu kama yalivyoainishwa katika Bibilia.

Askofu Mkuu mstaafu wa Kanisa la Tanzania Assemblies of God, Emmanuel Lazaro

Mtume Onesmo Ndegi
Utaratibu wa Safari ni kuwa msafara huu utaondoka jijini Dar es Salaam, tarehe 14/07/2013 na kurudi tarehe 22/07/2013. Katika safari hiyo, Askofu Lazaro pamoja na mkewe, watafuatana na, Mtume Onesmo Ndegi, Maaskofu, Wachungaji na Wakristo mbalimbali.

Gharama za safari yote ni ni Dola  za Marekani 2700, ikiwa ni pamoja na gharama za malazi, chakula cha mchana na usiku, usafiri wa kwenda maeneo mbalimbali nchini Israel, kibali cha kuingia maeneo ya nchi, VIZA na usafiri wa ndege.

Wanaotaka kujiunga na safari hiyo ya Baraka, ambayo imeratibiwa na NANURI SAFARI COMPANY LIMITED walipe fedha hizo kupitia:

NANURI SAFARI COMPANY LIMITED
NMB – ILALA BRANCH
ACCOUNT NO: 2036600111
DAR ES SALAAM.

Ukiwa na swali lolote, wasiliana nao kwa mawasiliano yafuatayo:
0715 – 640 777; 0782 – 640 777;  0716 – 316 109

AU
Fika katika Ofisi zao zilizopo Mwalimu House ghorofa ya 6, Ilala Boma jijini Dar es Salaam. Kumbuka nafasi ni chache wahi mapema kabla hujachelewa.

Waziri Mkuu atembelea Kanisa lilipolipuka Bomu na Kuzungumza na waumini na Viongozi wa Kanisa.


Waziri Mkuu, Mizengo Pinda  akizungumza na Viongozi na Waumini wa Kanisa Katoliki la Olasiti Jijini Arusha  May 7,2013 alikokwenda kutoa pole kufuatia mlipuko wa bomu la kutupwa kwa mkono uliotokea kanisani hapo May 6,2013 na kusababisha vifo na majeruhi. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu







 

Masikitiko ya mjane wa Mch. Kachila aliyeuwa kinyama katika mgogoro wa kuchinja

Katika mahojiano na Mwandishi wa Shirika la CBN News, mjane wa Mchungaji wa Kanisa la Kipentekoste aliyeuwa kinyama katika mgogoro wa kuchinja, Rev. Mathayo Kachila, Bi. Generosa Kachila, alitamka maneno yanayoashiria uchungu wa moyo wake kutokana na mkasa wenyewe na hata jinsi hatua za kisheria zilivyochukuliwa.

Kwa uchungu mama huyu alisema: "I shouted, my Jesus, my Jesus, why have you forsaken me?"  tafsiri isiyo rasmi “Nilipaza Yesu wangu Yesu wangu mbona umeniacha?” kilio hiki cha mshtuko wa kuuawa kwa mumewe aliyekuwa kiongozi wa familia, kumemuacha mjane huyu akiwa  mlezi pekee wa watoto 12.

Jambo baya zaidi ni kuwa mahojiano ya mama huyu yanaashiria uchungu zaidi kwa vile waliotekeleza  unyama huo hawajakamatwa na mwenyewe anaamini kuwa wako Mjini Mbeya na wengine  wamevuka mpaka na kuingia nchini  Burundi.

Ni wazi kuwa mjane huyo anaona jinsi juhudi zilivyofanyika kwa kuwatumia  wapelelezi wa kigeni kuwapata wauaji wa kasisi kule Zanzibar, kwa kuchorwa mchoro uliowezesha mtuhumiwa kukamatwa, na angependa kuwaona wahusika wa mkasa ule kuanzia wachochezi mpaka watekelezaji wakisimama mbele ya sheria.

Tunaamini kuwa  machozi ya mama huyu ni mashtaka mbele za Mungu ambaye Biblia inamuelezea kuwa ni baba wa yatima na Mume wa wajane.

Kwa kuwa yeye ndiye pia mhukumu Mkuu wa dunia  tuna hofu kuwa ikiwa tutazembea  kwa namna yoyote ile  kutenda haki iliyostahili, yaani kuwasaka wauaji wa mumewe kwa nguvu kubwa kama ile iliyotumika katika  matukio mengine yaliyoonekana ya muhimu.

Kwa mujibu wa utafiti wa Mwandishi wa CBN,  miongoni mwa watuhumiwa wakuu ni yule anayetajwa kwa jina moja la Abdallah ambaye inaelezwa kuwa yupo nchi jirani ya Burundi.

Tunaishauri serikali yetu kuimarisha msako wa watuhumiwa wote ili haki itendeke na wale waliopoteza mpendwa wao waione na kuitambua haki  hiyo.

Ni vyema pia serikali ikafahamu kuwa suala hili sasa lina sura ya kimataifa na ulimwengu unasubiri kusikia hatua madhubuti zinazochukuliwa katika kuilinda amani ya  nchi.Hatua hizo madhubuti zitafuata kile kilichoelezwa karibuni na mmoja wa wahubiri wa kimataifa kutoka  Ulaya kuwa mataifa ya magharibi yana kampeni maalumu ya kuionyesha dunia kuwa Tanzania si kisiwa cha amani tena.

Tunaamini kuwa haki ndiyo nguzo kuu ya amani yetu, tusipojali haki hata ya mnyonge  amani yetu itakuwa bandia au woga na wala si ile inayojengwa na nguzo ya upendo na undugu wa kweli.

Pia tunaishauri tena serikali kuliamua suala la uchinjaji ambalo ni chanzo cha  mauaji ya mchungaji huyo, liamuliwe kwa mujibu wa sheria na katiba ya nchi ambao ndio mkataba baina ya watawala na watawaliwa.
Wakati huu wa kusubiri serikali kuamua, pia wachungaji na viongozi wengine wa dini wajiapushe na lugha kali zinazoweza kuchochea chuki zaidi.

Wadumu katika kuomba, kushauri kwa upendo na kuelekeza kwa kuwa dunia inawatarajia kuwa waamuzi wakati mambo yanapoharibika.

Ni vyema watanzania nao wakajitambua  na kujitenga na watu wenye  nia mbaya wawe ni wa ndani au wa nje ya nchi wanaotaka kuona damu ya watu ikimwagika. Ni wazi kuwa kila mmoja wetu anajua kilichotokea katika mataifa jirani kuanzia, Rwanda, (mauaji ya kimbari 1994) Kenya ( mauaji ya baada ya uchaguzi wa mwaka 2007) na hata yale ya Burundi na Kongo.

Chingafirst aja na mbinu mpya uimbaji nyimbo za injili

Kutokana na kukua kwa kasi kwa muziki wa Injili nchini, na kufanya miziki ya dunia kushuka katika tasnia ya muziki, mwimbaji William Chingafirst amekuja na staili mpya ya kumtukuza Mungu kwa njia ya uimbaji.
Mwimbaji Chingafirst, akiongea na chanzo ca blog jijini Dar es Salaam, alisema amekuja kivingine katika kumtukuza Mungu, pasi na ushindani, japo nyimbo zake zimeonekana kuleta ushindani maeneo ya Kahama, Geita na Tabora.

Akiongelea kuhusu albamu yake yenye nyimbo 11, alisema ameimba na kucheza kwa mitindo tofauti tofauti ikiwemo;  kwaito yenye asili ya Afrika Kusini, Rumba na Sebene toka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, sambamba na Dansi asili yake Tanzania na nyimbo za kuabudu zenye mchanganyiko wa lugha ya kiingereza, kiswahili na kifaransa.

Alisema lengo lake ni kumwimbia Bwana kama ilivyo kule mbinguni ambapo malaika, wazee 24 na watakatifu wanavyomsifu Mungu kwa ukuu wake.

Aidha, aliongeza kuwa, yuko tayari kuimba kwenye kanisa lolote linalomhubiri Kristo aliye hai, linaloamini habari ya wokovu na tayari alishafanya katika baadhi ya makanisa jijini Dar es Salaam, akitamba na wimbo wa Sina Deni Aka Mie japo wimbo uliyobeba albamu yake ni Namshangilia Mwokozi.

Mwimbaji huyo anabainisha kuwa, uimbaji ni ibada tosha mbele za Mungu, huku akiongeza kuwa, Neno linahubiriwa kwa sababu watu wamemuacha Mungu, lakini kinachoendelea mbinguni katika ulimwengu wa roho ni sifa na kuabuudu.

Miongoni mwa nyimbo ndani ya albamu hiyo ni; Niko huru (mwanawane), This is the day you have made for me, Namshangilia Mwokozi, Ibelieve in You, Sina Deni Aka Mie, Tanzania Tunaweza kuuponya ulimwengu kwa jina la Yesu, Heri Wenye Moyo Safi, Twende kwa Bwana, Tutaimba Milele, Mtakatifu na Kila Jambo.
Alisema nyimbo hizo zimesanifiwa kiroho katika studio ya Hosana na maproduza tofauti tofauti.

Bomu larushwa kanisani Arusha, mmoja afariki wengine kujeruhiwa!

Mtu mmoja amefariki dunia na wengine 59 kujeruhiwa akiwamo Balozi wa Vatican na Mwakilishi wa Papa nchini Tanzania, Askofu Mkuu Francisco Montecillo Padilla jana asubuhi baada ya mtu asiyejulikana kurusha bomu wakati wa sherehe ya uzinduzi wa Jengo la Kanisa la Parokia ya Mtakatifu Joseph Mfanyakazi, Olasiti, Arusha.

Miongoni mwa majeruhi, imeelezwa kuwa wanne ni mahututi.Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas amelielezea kuwa tukio hilo kuwa ni la kigaidi hasa kutokana na kumlenga Balozi wa Papa nchini na kwamba mtu mmoja anashikiliwa akihusishwa nalo.

Wataalamu wa mabomu wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) wanachunguza aina ya bomu lililotupwa lakini uchunguzi wa awali unaonyesha lilikuwa limetengenezwa kienyeji.

Watu walioshuhudia tukio hilo wanasimulia kuwa bomu hilo lilirushwa yapata saa nne asubuhi wakati mgeni rasmi akijiandaa kufungua jengo la kanisa baada ya ujenzi wake kukamilika.

Shambulio hilo lilitokea wakati balozi huyo akiwa amesimama na mwenyeji wake, Askofu Mkuu, Josephat Lebulu, mapadri na watawa kutoka mashirika mbalimbali ya Jimbo Kuu la Arusha kwa ajili ya kukata utepe wa uzinduzi.

Kamanda Sabas alisema mtu aliyerusha bomu hilo alitokea nyuma ya kanisa hilo la ghorofa na kurusha bomu hilo kwa mkono wa kulia... “Alifanya jitihada za kupenya ili awafikie viongozi lakini alishindwa kutokana na wingi wa waumini waliokuwapo kwenye eneo hilo.”

Padri Moses Mwaniki aliyemshikia Balozi Padilla maji ya baraka yaliyotumika kubariki kanisa hilo, alisema kilichosaidia bomu hilo kutomfikia mwakilishi huyo wa Papa ni kutua mgongoni mwa mmoja wa waumini na kuanguka chini kabla ya kulipuka na kujeruhi watu.

“Ingawa hatuwezi kusema kwa uhakika, tunaamini mlengwa mkuu alikuwa mgeni wetu, Balozi Askofu Mkuu Padilla. Tunatakiwa kuliombea sana Taifa liondokane na matukio mabaya kama haya,” alisema Padri Mwaniki.

Baada ya tukio hilo, Balozi Padilla, Askofu Lebulu na viongozi wa kanisa hilo waliondolewa na kuhifadhiwa katika moja ya vyumba vya kanisa hilo kabla ya kutolewa kwenye eneo hilo yapata saa 5.30 asubuhi chini ya ulinzi mkali wa polisi.

Msemaji wa Kanisa Katoliki, Jimbo Kuu la Arusha, Padri Festus Mangwangi alisema aliyerusha bomu hilo alishuhudiwa na mtoto mdogo aliyekuwapo kanisani hapo.
Mapaka sasa mtu mmoja ashikiliwa na  Jeshi la Polisi kwa wa uchunguuzi wa tukio hilo

Baada ya bomu kuulipuka na jereuhi watu,watu wakikimbia kutafuta msaada katika sherehe hiyo.


Mahali ambapo inasemekana bomu lililipuka
Kanisa ambalo mbele yake ndio ilikuwa inafanyika sherehe hiyo na bomu kulipuliwa
Makamu wa Rais Dk. Gharibu Bilal akimsikiliza Askofu mkuu wa Kanisa la KKKT Tanzania Askofu Dk Alex Malasusa akizungumza katika matukio hayo kusho wakati akizungumza na majeruhi na wafiwa waliopteza ndugu katika milipuko ya mabomu iliyotokea leo jijini Arusha

Waandishi wa habari Afrika Mashariki watakiwa kuepuka habari za uchochezi

Dk. Richard Sezibera
Waandishi wa Habari wa nchi za Afrika Mashariki wametakiwa kuzitangaza nchi zao kwa kuandika habari zenye kuleta tija kwa taifa husika na kuepuka habari za kuharibu amani.

Wito huo umetolewa jana na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Dk. Richard Sezibera, wakati alipokuwa akifungua mkutano wa Afrika wa siku mbili wa maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa habari duniani, unaofanyika mjini hapa.

Alisema kuwa umuhimu wa vyombo vya habari duniani ni mkubwa na hasa nchi za Afrika Mashariki, kwa kuwa zaidi ya watu milioni 33 Afrika Mashariki wanategemea vyombo vya habari kupata habari za nchi zao.

“Kutokana na hili naomba sana nyie waandishi wa habari nchi hizi muunganishe nguvu kwa kuzitangaza nchi zenu mambo mazuri kama vivutio vya asili na vingine, ili pia muweze kuwabadilisha viongozi pale wanapokwenda pabaya,” alisema.

Dk. Sezibera, alisema habari zinapatikana kupitia simu na kompyuta yenye mitandao ya jamii, hivyo kikubwa kuhakikisha wanahabari mnadumisha amani kwa kuandika mazuri ya nchi zenu. Akitoa mfano alisema uchaguzi wa Kenya kila mtu aliyekuwa nje ya nchi hiyo aliweza kufuatilia uchaguzi huo mwanzo hadi mwisho, kupitia vyombo vya habari, hivyo ni jambo la kupongezwa.

Aidha aliwasihi wanahabari, kujenga utamaduni wa kuandika kwa wingi matukio yanayofanyika nchi za Afrika Mashariki, badala ya kutegemea kupata habari za nchi zao kupitia CNN.

“Mimi nasikitika sana kuona habari za nchi zetu hizi za Afrika Mashariki zinaelezewa kwa kiasi kikubwa na nchi zingine, jamani tubadilike,” alisisitiza.

Aliwapa pole waandishi wa habari wote waliopatwa na majanga, vifo mbalimbali wakati wa ufanyaji wa kazi zao.

Naye Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-Moon na Mkurugenzi Mkuu wa UNESCO, Irina Bokova, ametoa ujumbe wake uliosomwa na Vibeke Jensen na Mkurugenzi wa UNESCO, kwenye maadhimisho hayo. Alisema uhuru wa kujieleza kama unavyoelezwa kwenye kifungu cha 19 cha tamko la ulimwengu la Haki za Binadamu ni muhimu kuwawezesha watu na kujenga jamii huru na za kidemokrasia.

Alisema Ikiwa ni haki ya msingi, haki hii ya kujieleza pia ndani yake ina maelekezo ya jinsi ya kulinda na kuendeleza haki nyingine zote za binadamu.

“Lakini utekelezaji wake hauji tu, unahitaji mazingira salama ya mjadala, ambapo kila mmoja anaweza kuongea kwa uhuru na uwazi, bila woga wala wasiwasi wa kulipiziwa kisasi,” alisema.

Alisema kwa sasa kuna changamoto nyingi tangu miaka 20 ipite ya maadhimisho hayo, sababu waandishi wengi wamekuwa walengwa wa mara kwa mara wa vitendo vya vurugu.

“Zaidi ya waandishi wa habari 600 duniani wameuawa katika miaka kumi iliyopita wengi wao wakiwa kazini kuripoti tena kwenye maeneo ambayo hayana vurugu,”alisema.