“Msitarajie utukufu mnapomtumikia Mungu’

Kumtumikia Mungu si kazi ya heshima mbele ya wanadamu, bali kwa Mungu pekee, hivyo waliojitoa kikamilifu kuingia katika shamba la Bwana wasifanye huduma hiyo wakitaraji mrejeo chanya toka kwa viumbwa.

Hayo yalisemwa na Mchungaji Ismaili Mwipile, wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Ukonga jijini Dar es Salaam, alipokuwa akihubiri katika mkutano wa injili uliokuwa kanisani hapo wiki iliyopita.

Mchungaji Mwipile aliwataka waamini wa dini ya Kikristo kutokukata tamaa pale wanapoamua kuifanya kazi ya Bwana, kwani heshima kubwa inatoka kwa Mungu ikiambatana na thawabu tele.

Aliwaasa waamini kuwa wavumilivu na wasio kata tamaa, wakijitahidi kuondokana na imani haba katika changamoto wanazokutana nazo, huku akifananisha na gereza la vifungo vya mafanikio.

"Paulo na Sila walikaa gerezani, licha ya kupata mateso, lakini walikuwa na imani na Mungu pekee waliyemwamini na ndiye aliyewaweka huru pale milango ya gereza ilipofunguka," alisema Mchungaji Mwipile.

No comments:

Post a Comment