AFLEWO Tanzania kuomba kwa ajili ya Viongozi wa Serikali na Dini

Katika kuelekea Mkesha Mkubwa wa AFLEWO Tanzania ikiwa imebaki siku moja kufanyika Baadhi ya viongozi wamezungumza mbele ya waandishi wa habari kuhusianana Mkesha huo pale DPC Kinondoni.

 Maandalizi yamekamilika kwa asilimia 90 mpaka sasa kuanzi Mass Choir hadi mambo mengine,hivyo kilicho baki ni kuanza Mkesha huo Kesho saa 3:00 kamili usiku BCIC Mbezi Beach
(Kituo cha Jogooo) katika kanisa la Bishop Gamanywa wa Wapo Mission International 

Katika Mkesha huo kunategemewa kuwa na wageni kutoka Nchi za jirani na mikoa ya jirani kama Mwanza,Moshi,Arusha na mahala pengine nje ya Jiji la Dar es salaam.

Mkesha Mkubwa wa AFLEWO utakuwa na kusifu na Kuabudu na Maombi kwa Taifa na Viongozi wa Nchi pia kuomba kwa ajili ya Viongozi wa Dini zote ukizingatia kama Taifa tunapitia katika changamoto na tofauti za kidini,hivyo tuna hitaji kwenda mbele za Mungu kwa mambio katika Mkesha wa AFLEWO Tanzania,Alisema hayo Pastor Fredie Kyara alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari.

Walio Pichani Kushoto ni Samuel Sasali, Mkurugenzi wa Habari Aflewo, Bishop Freddie Japhet Kyara Mlezi Wa Aflewo Tanzania, Pastor Paul Safari Mlezi wa Aflewo Tanzania, Samuel Rodin Mwangati Music Director wa Aflewo.


 Bishop Freddie Japhet Kyara Mlezi Wa Aflewo Tanzania akizungumza na waandishi wa kwa msisitizo na kuhusu Mkesha huo
Samuel Sasali, Mkurugenzi wa Habari Aflewo, Bishop Freddie Japhet Kyara Mlezi Wa Aflewo Tanzania, Pastor Paul Safari Mlezi wa Aflewo Tanzania, Samuel Rodin Mwangati Music Director wa Aflewo.

No comments:

Post a Comment