NIGHT OF WORSHIP.....CITY HARVEST


Spika wa Bunge aonya hatari ya Freemason nchini.

“Maombi yanaweza kuleta katiba nzuri, amani na umoja, licha ya kuwa na tofauti za kiitikadi. Mimi uspika nilipewa na Mungu, ni msalaba, lakini namshukuru Mungu kwangu ni mwepesi, Roho Mtakatifu ananitia nguvu.”

SPIKA wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Anne Makinda, ameliomba kanisa limsihi Roho Mtakatifu aingilie kati kuikoa Tanzania, huku akiwaonya vijana kuacha kukimbilia kwenye ofisi za kundi la kishetani  la Freemason kwani halitatatua matatizo yao, bali litawaingiza mautini.

Spika Makinda alitoa rai hiyo siku chahe zimepita, mbele ya maelfu ya wanawake watumishi wa Kristo, (WWK) wa Kanisa la Tanzania Assemblies of God (TAG) waliokutana katika Mkutano wao Mkuu uliofanyika kwenye Ukumbi wa Chimwaga mkoani Dodoma.


Kiongozi huyo, mmoja wa mihimili mikuu mitatu inayounda dola, aliyeongozana na Mkuu wa mkoa wa Dodoma Dk. Rehema Nchimbi, na viongozi wengine wa serikali alionya kuwa taifa linamhitaji sana Roho Mtakatifu ili kuvuka katika hatua iliyopo.

Alisema kuwa, vijana wengi wamekumbwa na tamaa ya kutafuta mafanikio bila ya kufanya kazi na wanahangaika kusaka ofisi za kundi la Freemason ili kupata mafanikio.
“Freemasons ni kazi ya shetani, huko hakuna kitu, ni ushetani mtupu, vijana wanapaswa kujitazama sana na kuwa makini juu ya kundi hili, lakini ikiwa watamtambua Mungu wa Kweli, basi wataweza kushinda, wanawake nyie ni jeshi kubwa, mkimlilia Bwana atawasikiliza na kuinusuru nchi,” alisema Spika huyo.

Mama huyo aliyeweka rekodi ya kuwa Spika wa kwanza Mwanamke, katika historia ya Tanzania huru, alienda mbali zaidi  na kuujongelea ulimwengu wa kitheolojia alipoitwaa Biblia takatifu akaifungua na kusoma maandiko kutoka katika kitabu cha  2Timotheo 3:1-7 . andiko hilo linasema:

 “Lakini ufahamu neno hili, ya kuwa siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari. Maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kutukana, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio safi…….. wasaliti, wakaidi, wenye kujivuna, wapendao anasa kuliko kumpenda Mungu…..”

Akiisha kukariri andiko hilo, Spika Makinda alilifafanua akisema kuwa, shetani hujibadilisha kwa sura tofauti ili kupumbaza ufahamu wa watu, hivyo ni wajibu wa vijana kufahamu na kutubu maovu yao kwa kuwa Mungu ni mwingi wa rehema, atawasamehe.

Mbali na hilo, Spika Makinda aliwasihi wanawake hao, kutenga muda wao mwingi kumlilia Mungu alete amani, umoja na mshikamano katika taifa wakati huu ambao mambo mengi yanatisha.Akiamini wanajua hali isiyo ya kawaida inayoendelea nchini na duniani kwa ujumla, kama vile uasi wa ndoa za jinsia moja, Ubakaji, dawa za kulevya, kumwagiana tindikali na uchomaji wa makanisa, aliwakumbusha kuwa maombi yao yataleta tumaini jipya.

“Ninyi si wanawake watumishi tu, ni wanawake watumishi wa Kristo, Mungu husikiliza kilio cha wacha Mungu, ndani ya ukumbi huu mmefurika iombeeni nchi, matukio ni mengi na ya kutisha, watu wanabaka hadi watoto wao,” alisema.

Hakuacha kuwaomba wanawake hao kupeleka maombi yao kwa Bwana, kuhusiana na mchakato wa upatikanaji wa Katiba mpya, ambapo Novemba 11, 2013 kutakuwa na Bunge la Katiba litakalojadili rasimu iliyokwisha tayarishwa na Tume ya Katiba chini ya jaji Joseph Warioba.

“Watu wa Mungu mwombeni Mungu kwa bidii, suala nyeti kama la Katiba linamhitaji Mungu kwa namna tofauti, mataifa mengi leo yamekuwa na machafuko kutokana na masuala ya kushindwa kuelezwa na kukubaliana kwenye katiba,” alisema na kuongeza:

“Miaka Kumi ya Mavuno!… Tanzania kwa Yesu…… salamu hii nzuri sana nimeipenda kweli,” alisema Spika Makinda, huku akiachia tabasamu lililosababisha ukumbi kulipuka kwa kelele toka kwa akina mama hao ambao wakati wote wa hotuba ya mheshimiwa huyo walikuwa katika nyuso za furaha, wakisikiliza kwa makini na wengine kuandika dondoo kwenye vitabu vyao.

Hapo mama Makinda anayetarajia kuachana na mambo ya siasa, akiongozwa na Askofu Mkuu wa Kanisa la TAG, Dk. Barnabas Mtokambali na mkewe, Gladmery sambamba na Mkurugenzi wa Idara ya WWK, Mchungaji Faraja Hamuli; kusalimiana  wakugurenzi wa majimbo, na wageni kutoka Marekani wakapata  wasaa wa kubadilishana mawili matatu.

Naye, Dk. Mtokambali akiongea kwenye mkutano huo, uliofurika umati wa wajumbe wa WWK kutoka kila kona ya Tanzania, wakiwa  na sare maalum zenye rangi ya  damu ya mzee, yenye kusindikizwa na ujumbe kutoka katika Biblia kitabu cha Yeremia 47:7 “Utawezaje kutulia, ikiwa BWANA amekupa agizo……” alisema anaamini katika mwanamke.

Dk. Mtokambali alimsifu Mhe. Makinda kwa kujitahidi kumudu uendeshaji wa vipindi vya bunge, licha ya wakati mwingine kutofautiana kiasi cha wabunge wengine kuchukua uamuzi wa kususia vikao hivyo.
Hata hivyo, alimuomba mheshimiwa huyo, kwa nafasi aliyonayo kuhakikisha nchi inabaki katika amani na umoja, huku akisisitiza sheria isiwe na jicho la upendeleo.

“Sheria isimwangalie mtu jinsi alivyo, awe na pesa nyingi, kwamba ni msomi, cheo. Sheria ifuate mkondo wake, izingatie haki ya aliyenacho na asiyenacho,”alimaliza kwa kusema Dk. Mtokambali.

Askofu.Dr Moses Kulola Baba wa Wengi afariki Dunia



Msiba huo wa umetokea  leo muda wa saa 5 asubuhi  katika hospitali ya AMI (African Medical Investments) iliyopo Slipway jijini Dar es Salaam,Msiba huo umetokiea kama mwezi mmoja baada ya Askofu Kulola kutoka Nchi India alikuwa ameenda kutibiwa ugonjwa uliokuwa unamsumbua.

Alipio kuwa nchini India kwa matibabu hali yake kiafya alipata nafuu ndio akawa amerejea nyumbani Alikuwa anasumbuliwa na ugonjwa wa ini na moyo.

Msiba kwa sasa uko Kanisa la EAGT Temeke na kusuburi utaratibu mwingine wa Kanisa la EAGT kwa siku ya Jumamosi saa 2 asubuhi kanisani hapo ili kuweza kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa Askofu Kulola baada ya hapo kuwa tayari kuelekea Jijini mwanza kwa mazishi alipo agiza mwenyewe azikwe,Ndugu,jamaa na washirika wako Kanisani EAGT Temeke

Bwana alitoa Bwana emtwaa,Jina lake lihimidiwe.
Source:Willy  Kulola

Historia ya Askofu .Dr Moses Kulola kwa ufupi.
Alizaliwa mwezi Juni 1928 katika familia ya watoto kumi na kufariki mwezi Agosti 2013 katika hospitali ya AMI (African Medical Investments) iliyopo Slipway jijini Dar es Salaam. Alisomea shule ya msingi ya Ligsha Sukuma, halafu taasisi ya usanifu. Alibatizwa kikristo mwaka 1950 katika Kanisa la AIC Makongoro. Alimwoa Elizabeth wakawa na watoto kumi.

Alifanya kazi ya uchungaji wa kanisa la AIC miaka ya 1961-1962 akaendelea na masomo ya kitheolojia. Baada ya kujiunga na dhehebu la kipentekoste alifanya kazi ya uchungaji ndani ya kanisa la TAG miaka ya 1966-1991. Akajitenga na kanisa hilo na kuanzisha kanisa jipya mwaka wa 1991, kanisa la EAGT (kwa Kiingereza Evangelistic Assemblies of God) akawa askofu wao wa kwanza tangu mwaka uleule.
Source: wikipedia

Former Pope Benedict Resigned Because 'God Told Me to'

In his first statement to the press since stepping down from the papacy in February, 86-year-old former pope Benedict has said he left his office because God directed him to.

Benedict told an unnamed reporter he felt the conviction to step down in a "mystical experience" that "had lasted months" where "God told [him] to" retire to a private life of prayer. He also claimed that the "charisma" of current Pope Francis gave greater context to why God had led him to retire from the post.

Pope Benedict XV1

Benedict's comments, made several weeks ago, and which first appeared in the Catholic news agency Zenit, were his first since his abrupt resignation. The German ex-pontiff became the first head of the papacy to step down in about 600 years.

Benedict initially attributed his resignation to his waning stamina and physical wellbeing.

"My strengths, due to an advanced age, are no longer suited to an adequate exercise of the Petrine ministry," he told his cardinals in February.

His self-assessment was reiterated in the media. The Guardian reported a German journalist's assertions in a recent meeting that the former pope "was going deaf, appeared to be blind in one eye, and was emaciated and 'exhausted-looking.'"

Yet many continued to speculate that Benedict had stepped down because of shadow Vatican scandals; Benedict's butler, Paolo Gabriele, leaked his personal correspondence. The Italian press also reported on an insider pro-gay lobby within the Church.

No more information on the latter has emerged as Pope Francis' popularity has had the press gushing over his relative austerity, humility and modesty. For his part, the current pope has said that he has appreciated access to Benedict's advice.

"It's like having a grandfather – a wise grandfather – living at home," he told reporters in July.

Iran:Christian Man Jailed for Distributing Gospel of Jesus Christ

An Iranian convert from Islam to Christianity has been sentenced to a decade in prison for proselytizing, the Christian news network Agenzia Fides reports.

The man, Mohammed-Hadi “Mostafa” Bordbar, was officially charged with “crimes against state security.”

Bordbar had previously faced criminal charges for converting to Christianity. He was found guilty of “apostasy,” but was not jailed.

His latest arrest took place in December 2012. He was taken into custody following a police raid at his home, which had been used for Christian prayer meetings.

Officers found thousands of copies of the Christian Gospel, which Bordbar had been distributing in an attempt to convince others to join him in following Christianity.

The report also noted a related sentence, that of Ebrahim Firouzi, an Iranian Christian who was sentenced to one year in prison and two years of exile for “evangelization activities and distribution of Bibles… in opposition to the regime of the Islamic Republic of Iran.”

Iran has a long history of arresting Christians, and targeting converts from Islam in particular. Some “Church of Iran” members have accused the state of treating them as “enemy number one.”

Christians are facing trouble in other parts of the Middle East as well. In Egypt, Coptic Christians have been targeted by violence from the Muslim Brotherhood, while in Syria, Al-Qaeda linked rebels have threatened to kill Christians who do not join the fight against President Bashar Assad.

In Iraq, Christians have been fleeing in their thousands to escape sectarian violence, which often targets Christians specifically.

Syrian Refugees 'Hungry for Message of Jesus

As the Syria civil war rages on and the U.N. investigates claims that chemical weapons might have been used in the conflict, one Christian missionary organization helping refugees has revealed that the people are hungry for the message of Christ, and urged believers to come together and help out in one of the most urgent humanitarian crises of the new millennium.

"We executed a food distribution and ministry program where we supplied food for about a two week period to 2,000 refugees, and during the event we distributed Bibles in their language and the story of Jesus booklets," Eric English, executive director of Strategic Planning for World Compassion Terry Law Ministries told The Christian Post in a phone interview on Tuesday.

Despite efforts from the U.N., the U.S. and other government bodies, there seems to be no end to the Syrian crisis, where rebels from the Free Syrian Army are fighting President Bashar al-Assad's Syrian Armed Forces, in a conflict which began in early 2011 and has claimed over 100,000 lives to date.

The civil war has led to a mass exodus of refugees, as many as 1.9 million according to reports, while another 4.2 million people in the Islamic nation have been displaced. World Compassion, a Christian ministry which heard the people's plea for help, organized relief efforts for the 150,000 Syrian refugees who are now stationed in Northern Iraq.

While the Kurdish region has tried to accommodate the large number of refugees coming over from Syria, reports say its young government is feeling overwhelmed and does not have a lot of experience dealing with such situations.

"It's a new government and new governments may not have the bureaucratic structure to deal with a situation such as this, which they have never seen before," said William Tall, the new head of the United Nations High Commissioner for Refugees (UNHCR) North.

English, who recently returned from the region where he worked with refugees as well as high-ranking Kurdish government officials and leaders, shared with CP that the relief efforts are helped by a local pastor supported financially by World Compassion, as well as a team of volunteers.

"It was just amazing because the Bibles went faster than the food did. They were very hungry for the message of Jesus Christ," World Compassion's executive director said of the response the organization received.

He added that World Compassion felt called to help the refugees at a time of personal and national tragedy, and urged Christians to take interest in these matters and reach out to help in a meaningful way.

"At large, the Christian population has not responded. And so we took that as a real call to action and took it to heart on how we can work with these Syrian refugees."

English shared that World Compassion met with the American consulate to the Kurdish region and he communicated with them the need to get out the story of the Syrian crisis to America, which he says has been under-reported by the media and that the true story has not been told.

Several blog posts on the World Compassion website highlight powerful stories by refugees and survivors of the civil war who share of the many losses they have suffered and the atrocities committed by both the government loyalists and the rebel fighters.  "Both sides are wearing black hats," English noted.

As for his personal experience, the executive director said that he walked away with a completely different opinion of Muslim culture than he previously had.

"What I had been taught is that all Muslims are radicalized and they hate Americans," English said. "But what I learned from being there is that the vast majority of Muslims are Muslims by birth, and they are just normal people who work normal jobs, like you and I do, and they don't hate Americans – but the radicalized minority controls the country and the environment."

"They were very open to the Gospel because they were not radicalized," he added.

Although Christian Syrians make up 10 percent of the country's population, he added that he did not encounter any at the refugee camps – largely because Christians do not feel safe declaring their faith in a situation where there are few resources to keep civil order.

World Compassion offers different ways for people to help with the crisis. Financial contribution is one option; a donation program the group started says contributions goes directly to the camps and that $25 can feed one refugee for one month, while $100 can help an entire family of four for a month.

Another important way people can help is through spreading news of the refugees' plight on the internet. "They can also be a voice on social media," English said. He encouraged internet users to send and share World Compassion's blog posts about the crisis, so that more people can become informed and come together to help with what they can.

English added that at the camps in Northern Iraq, World Compassion is working with local church pastors who reach out on an ongoing basis to foster relationships with the people, and help them facilitate house churches and Bible studies.

"The tragedy of the Syrian war has created a vast opportunity for the Gospel to be ministered in the Middle East. On a social level, we have a responsibility to respond to the crisis as Christians, and to help people who are in need," the World Compassion executive director urged.

Semina ya Mpenyo (Breakthrough) Living Water Centre -Shinyanga


Sunday Celebration Praise & Worship Concert


The government of Cameroon is severely cracking down this month on Pentecostal churches, vowing to shut down nearly 100 congregations.


Paul Biya, the president of the western African nation, says the closures are an attempt to prevent Pentecostal pastors from conducting “criminal practices” that allegedly threaten Cameroon’s national security. Thus far, at least 50 churches have been shuttered by government officials, but more forced closures are on the way.

Cameroonian officials claim these Pentecostal churches are a menace to their country’s well-being because of fake healing attempts and other controversial spiritual activities. For instance, the government is citing the death of a 9-year-old girl during a prayer session last Sunday, when a Pentecostal pastor was attempting to cast out demons from her body.

 
Mbu Anthony Lang, an official with the Cameroonian government, told CNN that only 50 of the 500 Pentecostal churches in his country are technically legal.
“We will get rid of all the so-called Christian Pentecostal pastors who misuse the name of Jesus Christ to fake miracles and kill citizens in their churches,” he vowed. “They have outstretched their liberty.”


According to Operation World, 54% of Cameroon’s 20 million residents describe themselves as Christians. 800,000 Cameroonian Christians are Pentecostals, but that number is growing at an annual rate of approximately 7%.Though the country is technically a secular nation, Cameroon’s constitution provides for religious freedom, and says “freedom of religion and worship shall be guaranteed.”

Connect with Christian News
“Everyone has the right to freedom of thought, conscience and religion,” the constitution states. “This right includes freedom to change his religion or belief, and freedom, either alone or in community with others and in public or private, to manifest his religion or belief in teaching, practice, worship and observance.”

Boniface Tum, a Bishop at a Cameroonian Church of God, told CNN that the government’s crackdown on Christian churches violates basic human rights.
“Authorizing only the Catholic, Presbyterian, Baptist, Muslim, and a few other churches, is a strict violation of the right to religion,” Tum said.
After his church was shut down last week, Pastor Elie Pierre encouraged churchgoers over a loudspeaker.

“We have the right to defend ourselves!” he exclaimed.

Following the reports of church shut-downs, some were pleased. One commenter called the development “good news,” and said “I hope the rest of African countries do the same. Well done Cameroon.” Another posited, “All countries should get rid of all churches and ban those vile books called [the] Bible, Koran, etc. Religion has no place in a civilized world.”

However, Theres Nchanji, leader of another Cameroonian church that the government recently shut down, explained that all countries need Christian churches.

“No state can do without a Church and the Bible says whosoever calls the name of the Lord Jesus will be saved,” she said, according to Voice of America. “The Bible says that our weapons are not carnal—they are spiritual. When the devil attacked Jesus in the wilderness, Jesus said it is written, he never picked a stone to face the devil.”

Mahakama yaombwa inajisi Kanisa.

Mara kadhaa siku zimepita wanatheolojia wabobevu walinukuliwawakionya kuhusu hatari kubwa inayolikabili kanisa la Bwana wakati zoezi la uasi mkuu wa kimaandili, utu na hata kanuni za Muumba lilipokuwa likiendelea katika  wigo wa siasa na harakati. Kisha Julai 17, mwaka huu hatua nyingine kubwa sana ikafikiwa wakati Waziri Mkuu wa Uingereza David Comeron aliposaini hati ya kuruhusu mashoga, kufunga ndoa kisheria.

Wiki zimepita nilipost ripoti hatua hiyo kwa undani zaidi na kiapo cha Waziri huyo mkuu wa taifa lenye nguvu na hila nyingi. Siku chache baada ya tukio hilo hatua mbaya zaidi ya kuelekea kwenye uharibifu imewadia ambapo  mahakama kuu imeombwa kuliamuru kanisa limuasi Mungu.

Kwa mujibu wa Shirika laUtangazaji la Uingereza (BBC) ingawa mbele ya mahakama ni wanaume wawili waliofungua mashtaka mahakamani wakiiomba mahakama kulilazimisha kanisa kuwapa haki ya kufunga ndoa rasmi mbele ya madhabahu, mpango huo ni mpana zaidi na umebeba watu wasioonekana.
Waziri Mkuu wa Uingereza David Comeron
Bwana  Barrie na Tony Drewitt-Barlow, ambao  wanaishi kama mume na mke, japo wote wawili huvaa suti nadhifu na kukatiza mitaa ya London kwa madaha, wameutangazia ulimwengu kuwa mipango yote ya kufungua mashtaka mahakamani imekamilika na tayari wanasheria wao wamekwisha andika ‘Plantif (hati ya mashtaka) ili kumuomba Jaji alimuru kanisa kuwafungisha ndoa kwa kuwa wanastahili haki hiyo.

Hatua hiyo inaelezwa na mabingwa wa sheria wa London kuwa ni hatua ya juu sana katika kuelekea kwenye mateso ya kanisa kwani amri ikishatolewa na mahakama, mchungaji atakayegomea ndoa hizo anaweza kufungwa gerezani.

“Profesa  John Wycliffe,  Mhadhiri mbobevu wa sheria za dini katika vyuo vikuu vya Uingereza na hata mataifa mengine ya Ulaya akiandika katika Twiter alisema: “Hili ndilo nililotegemea, yale yote ya Cameron yalikuwa yakiandaa hili na wakati umefika wa kanisa kuingia katika mateso. Asomaye na afahamu kuwa chukizo la uharibifu linaingia patakatifu.”

Hawa wanaume wawili wasingekuwa na kiburi cha kuitisha mkutano wa waandishi wa habari na kutangaza hatua kubwa kiasi hiki,   kulishitaki kanisa  na taasisi zote za kidini zinazoshikilia msimamo wa kimaadili.
“Hawa jamaa wanatimiza kile bosi wao alichoahidi kuwa atahakikisha kila taifa linaisujudia sheria yake ya uasi wa kimaadili, huu ndio ujanja wa kiingereza,”alisema.

Walalamikaji wanajigamba kuwa  waliotiliana mkataba wa mahusiano ya wao kwa wao mwaka 2006, baada ya serikali kuidhinisha mambo hayo, wanataka wakabariki ndoa yao kanisani.Serikali ya Uingereza katika  mahojiano kwenye sherehe za kile ilichokiita ushindi dhidi ya wahafidhina,ilidai kuwa makanisa hayalazimishwi kufunga ndoa madhabahuni, lakini kanisa la Anglikana haliruhusiwi kabisa kufungisha ndoa hizo.Anglikana ndiyo dini rasmi ya taifa la Uingereza na Mkuu wake akishachaguliwa huidhinishwa familia ya kifalme ndipo ashike madaraka ya kuliongoza kanisa.
Ndoa ya jinsia moja
“Maadam watu wanasema jambo hili ni jema, bado sipati ninachokitaka, haijaweka wazi ulazima wa makanisa kutambua wazi ili kuondoa misuguano na mashoga wanataka kufunga ndoa, kitu cha pekee kwetu kilichobaki ni kuishinikiza Mahakama ifanye kitu dhidi ya kanisa,” alisema Drewitt-Barlow na kuongeza:
“Ni kitu cha aibu inapofikia mahali tunalazimishwa kuwapeleka Wakristo Mahakamani ili tu eti watutambue rasmi, inanivunja moyo kwa sababu mimi binafsi napenda kuwa na `BONGE` la sherehe kuanzia kanisani, na hii sidhani kama inaweza kuja yenyewe bila sisi wenyewe kuhimiza kwa nguvu za amri ya Jaji.”

Ilibainishwa kuwa, tofauti na ilivyo Marekani, nchini Uingereza kanisa la England limeshikamanishwa sana na Serikali. Lakini pamoja na harakati za usimamiaji wa haki za binadamu, chini ya uongozi wa Rais Obama, makanisa ya Marekani tayari yameanza kushauriwa kujiandaa kuwa na mtikisiko kama huo na hata kuburuzwa mahakamani na makasisi kufungwa jela watakapokataa kutii amri halali ya mahakama.

Taasisi na mashirika makubwa kadhaa duniani yanashauri makanisa kuanza kujijengea wigo wa kisheria wa kujihami dhidi ya yeyote atakayeonekana kuunga mkono kufungisha ndoa za jinsia moja makanisani mwao.
Ushauri mmojawapo kutoka taasisi moja ya kibabtisti, Kusini mwa Califonia, unaonya kuwa ni muhimu kwa wachungaji kuchukuwa hatua madhubuti za kulinda maadili ya kitheolojia ikiwa ni pamoja na namna ya uendeshaji wa sherehe za ndoa, ushauri na shughuli nyinginezo zinazowiana kama vile; matumizi ya mali za kanisa, ajira na uanachama.

Mwanasheria Kelvin Snider, wa taasisi ya masuala ya kisheria ya Pacific, ananukuliwa akiyahimiza makanisa kupembua upya na kuifanyia kazi haraka sera ya ndoa itakayokuwa kielelezo kizuri.Alisisitiza kuwa, sera hiyo haipaswi kuhusishwa na kanuni za kikanisa ila akapendekeza lazima sera hiyo iangazie mambo muhimu kama vile; muundo wa kanisa, Bodi ya Kanisa, Baraza la kanisa au hata uanachama na ikibidi katiba zibadilishwe na kuingiza kipengele cha utii wa kanuni na sheria ya Biblia kama sifa muhimu kwa mwanachama wa kanisa.

Aidha, alibainisha kuwa, sera iliyopendekezwa na PJI inasema ndoa ni ushirika ulioasisiwa na Mungu.”
“Ilikuwa taasisi ya awali kabisa iliyoasisiwa na Mungu kama ilivyo kwenye maandiko matakatifu kitabu cha Mwanzo, ambako agano la kale manabii waliifananisha taasisi hii na mahusiano yaliyopo baina ya Mungu na watu wake.

“Yesu katika Agano Jipya alielezea kusudi halisi na vigezo vya ndoa, ambapo ndoa inafananishwa na uhusiano uliopo kati ya Kristo na Kanisa, hivyo kanisa linapaswa kuitazama ndoa kama Taasisi ya Kiroho iliyoanzishwa na Mungu mwenyewe,” alisisitiza na kuongeza:

“Sera itamtaka kila mtu anayetaka kufanya sherehe itakayomshirikisha mwajiriwa yeyote wa kanisa, au hata mtu akitaka kutumia vyombo vya kanisa, lazima mambo hayo yatazamwe kikatiba kwa kuzingatia vipengele husika vya imani.”

Chini ya sera hii, kanisa linaweza kujiwekea masharti kuwa, wafanyakazi wake kamwe hawapaswi kushiriki kwa namna yoyote kwenye vyama vya watu wa ndoa za jinsia moja na kwamba, mali ya kanisa kamwe haitatumika kwa namna yoyote katika kufanikisha shughuli yoyote ya kishoga.

Kwa upande wa Uingereza, jambo hili ni tofauti kwa sababu ya mahusiano makubwa yaliyojengwa kati ya kanisa na Serikali. Hii ndiyo kusema baadhi ya sheria za kikanisa zimemegwa moja kwa moja kutoka sheria mama za Serikali.

Wiki jana Waziri Mkuu wa Uingereza, David Cameron, mbele ya waandishi wa habari, na timu yake inayoshughulikia hati inayotambua haki za mashoga, akiishukuru kwa ushirikiano na kazi kubwa iliyofanyika hadi muswada kuwa sheria. Hapo alipata wasaa wa kueleza nia yake ya kuusambaza duniani kuokoa mahusiano ya jinsia moja ambapo alidai kuwa wanyanyasika na kunyimwa uhuru wao na kuahidi kusimamia mpango huo kwa gharama ya kifo.

Wataalamu wengine  wanaonya kuwa harakati hizo za Uingereza zikishapitishwa na Mahakama itakuwa rahisi kwa nchi wanachama wa Jumuiya ya madola kama Tanzania kushurutishwa na wakubwa kuitii amri hiyo.

Rufaa ya mauaji ya Yesu yaumiza vichwa ‘The Hague’


 
Rufaa ya hukumu  ya kifo aliyohukumiwa  Bwana Yesu Kristo zaidi ya miaka 2000 iliyopita, iliyofunguliwa  mahakamani na mwanasheria mashuhuri, Bw. Dola Indidis, imezidi kusugua vichwa vya wanasheria na wanatheoloj­imeishinda mahakama kuu ya Kenya iliyohangaika nayo kwa miaka mitatu sasa imeelekeza mlalamikaji kuelekea The Hague nchini Uholanzi kuwasilisha shauri hilo kwenye Mahakama ya kimataifa ya haki (ICJ).

 Washtakiwa wanaopaswa kufika mahakamani kujitetea au wawakilishi wao ni Mtawala wa Roma, Tiberius Pontus Pilate (Pilato), Padre Annas (kiongozi wa Wayahudi, Mfalme Herode, Jamhuri ya Italia,Taifa teule la Mungu Israeli  na waalimu wa sheria za kiyahudi.

Mwanasheria huyo aliiambia korti kuwa mataifa hayo yanakesi ya kujibu kwa kuwa hadi sasa bado yanatumia sheria za utawala wa Roma na zile zilizotumika kumsulubisha Yesu msalabani  na zinaweza kutumika kuwatesa wengine
Mwanasheria mashuhuri nchini Kenya  Bw. Dola Indidis
 Mlalamikaji anasema kuwa Jaji Pilato alikiuka sheria pale aliposhuhudia mtuhumiwa akipigwa kabla ya hukumu wakati alistahili kusimamia haki ya watu wote  bila kuruhusu ukiukwaji wa haki wa aina yoyote ile.
Mateso yanayolalamikiwa ni kuwa mshtakiwa kabla ya kutiwa hatiani alichapwa na kutemewa mate, tena mbele ya jaji,  suala ambalo ni kinyume cha haki za binadamu na kwa kuwa Yesu alikuja duniani kama mwanadamu alistahili kupata haki ya kulindwa na sheria.

Mlalamikaji anasema mfumo wa maswali na adhabu aliyokuwa akiendelea kupewa tangu alipokamatwa vilikiuka kabisa sheria na haki za kiutu, hivyo anaitaka mahakama itamke kuwa Yesu hakutendewa haki.
Mwanasheria huyo alisema kuwa ameiomba mahakama ibatilishe hukumu ya Yesu na kuitamka kuwa ilikuwa batili ili wanadamu wengine wasije wakajikuta kwenye mateso kama hayo, tena analalamika kuwa Yesu hakupewa wakili wa kumtetea mahakamani.

Miongoni mwa wale waliozungumzia kesi hiyo katika muktaza wa sheria ni Wakili wa Mahakama Kuu nchini, Justin Kaleb, ambaye alisema kuwa  kesi ya mauji ya Bwana Yesu si mauaji ya halaiki ‘genoside, ni ya  mtu mmoja, inakosa sifa ya kujadiliwa na Mahakama ya  kimataifa ya uhalifu wa kivita (ICC). 

Kisha  mwanasheria huyo akahoji; mlalamikaji itabidi aihakikishie mahakama kuwa, kama  ni mpenzi au rafiki wa Yesu na kama amepewa mamlaka hayo na ukoo wa Yesu. Ukoo huo bado upo mpaka leo.
“Inamlazimu mlalamikaji kuidhihirishia mahakama iwapo yeye ameathirika kiasi gani na suala la kuteswa na hata kuuawa kwa Bwana Yesu Kristo,” alisema Kaleb.

Alifafanua kuwa hukumu ya Yesu ilikuwa sawa sawa kwa mujibu wa sheria za kiyahudi za wakati huo ambazo zilikuwa zikitamka wazi kuwa mtu akikashfu dini ya kiyahudi anahukumiwa adhabu ya kifo.
Kuhusu malipo ya fidia, Mwanasheria huyo alisema kuwa ikiwa mlalamikaji anataka alipwe fidia itamlazimu aandikishe orodha ya marafiki wa Yesu wanaostahili kupata  jambo ambalo ni gumu sana.
Lakani akasema kuwa,  pengine kipengele cha kutaka hukumu hiyo kuwa fundisho kwa mataifa mengine  kinaweza kufanikiwa na kuwa msaada kwa sheria za sasa.

MWANATHEOLOJIA
Mmoja wa waalimu wa theolojia, mchungaji Samwel Mwaluvanda, akiongea na chanzo cha habari, alisema rufaa inayofanywa na mkenya, Dola Indidis si jambo sahihi kwa sababu zifuatazo:

“Moja: anafanya dhambi ya Petro ya kupingana na kusudi la Mungu. Petro hakutaka Yesu asulubiwe maana aliwaza kibinadamu na kimaslahi binafsi, Yesu akijua kosa hilo alimkemea: “….Nenda nyuma yangu, Shetani; u kikwazo kwangu; maana huyawazi yaliyo ya Mungu, bali  ya wanadamu.” Mathayo 16:23

Pili: Lilikuwa kusudi la Yesu Mwokozi, kumtumikia Mungu na mwandamu kwa gharama ya kutoa nafsi yake, Marko 10:45. Hata Biblia ilitabiri kuwa masihi atatoa maisha yake na damu yake ili kuwakomboa wanadamu kama anavyokiri yeye mwenyewe katika Luka 24:44 - 47

Tatu: Kristo Yesu aliyatoa maisha yake mwenyewe na kwa hiari yake hakuna mwanadamu au afisa yeyote aliyemzidi Yesu na kumhukumu, kumuua, Yohana 10:18-28.

Nne: Yesu Kristo aliwatangazia msamaha wote waliomtendea mabaya, kumsulubisha na hata kumuua. Ni msamaha bila masharti yoyote Luka 23:34

Tano: Kanuni za Philosophy of Influence yaani katika kila kesi na hukumu lazima kutazama pia mitazamo ya watu kuhusu tukio. Kwa tukio la Yesu Kristo, ulimwengu umepokea na kukubali na kusherehekea tukio hilo kuwa la ukombozi kwao. Kwanini kuhukumu jambo linalokubalika?

Sita: Kuhukumiwa kifo kwa Yesu ni suala la kiroho na kiimani,  siyo suala la kisheria au kisiasa, ni mambo ya imani  na yanatambulika kwa jinsi ya imani na Roho Mtakatifu. Biblia inakataa kupeleka mambo ya imani katika mahakama za watu wa dunia wasio na Roho Mtakatifu wala wokovu, 1Wakorinthoi 6:1-12.”
Hata hivyo, mwanatheolojia huyo aliongeza kuwa, mwanasheria Indidis inaonyesha ana kiburi cha uzima, na kusisitiza kuwa amejikinai.

 “Amepoteza hofu ya Mungu, anatumia mambo Matukufu ya Mungu kujitafutia umaarufu wa kidunia kama baadhi ya viongozi wa siasa na taasisi mbalimbali 1Yohana 2:15-18,” alisema.

 Mchungaji John Masanyiwa wa Kanisa la AIC Geita, akiongea na chanzo cha habari hii kwa njia ya simu, alikuwa na haya ya kueleza: “Mgogoro uliopo baina ya Palestina na Israeli kamwe hauwezi kuisha kwa mazungumzo bali Neno lazima litimie.”

Aliongeza: “Kupoteza ukweli juu ya imani ya YESU, Tendo hilo hatuoni ajabu, watu wa jinsi hii Biblia inawataja kwamba siku za mwisho watatokea. Watafiti na wadadisi wa mambo, tutegemee mengine zaidi ya haya kuwa yanakuja.  Watu wanawaza hata sala ya Baba yetu Uliye mbinguni isiishie kutaja Baba wa mbinguni bali pia itaje mama wa mbinguni.”  

Kesi hiyo iliyofunguliwa kwa mara ya kwanza katika mahakama Kuu ya Kenya chini ya kifungu namba 65-67 cha katiba ya zamani ya Kenya, ikiwa  na walalamikaji ambao ni  marafiki wa Yesu kupitia kwa Dola Indidis  na taasisi ya kutetea haki za kiraia na Humfrey Odanga Achala.