TAG kusherehekea miaka 75 ya uhai wake Tanzania

Kanisa la Tanzania Assemblies of God (TAG) linakusudia kuadhimisha miaka 75 tangu kuanza kwake nchini, sherehe ambazo zitafanyika kitaifa mkoani Mbeya mwakani.

Hayo yalibainishwa na Askofu Mkuu wa kanisa la TAG, Dk. Barnabas Mtokambali, katika uzinduzi wa Mkutano Mkuu wa Idara ya Maandiko na Uanadunzi uliofanyika katika Ukumbi wa mikutano wa Highland Camp Morogoro, Jumatano iliyopita.
Askofu Mkuu wa kanisa la TAG, Dk. Barnabas Mtokambali

Kiongozi huyo wa kitaifa alisema kuwa Halmashauri kuu ya kanisa hilo imeamua kuwa sherehe hizo zitafanyika katika Uwanja wa Sokoine mkoani Mbeya mwaka 2014.

Alisema kuwa maadhimisho hayo yataanzia katika ngazi ya kanisa la mahali pamoja na baadaye ngazi ya Jimbo na fainali itakuwa ni ngazi ya taifa mkoani Mbeya.

Kanisa la TAG, ambalo linaongoza miongoni mwa makanisa ya TAG, kukua kwa kasi nchini linatimiza miaka 75, tangu lianze nchini huku likienea kila mahali kuanzia mijini mpaka vijijini.





No comments:

Post a Comment