Niko ambaye Niko Studio yatoa Ofa Kubwa kwa Wateja wake.

Studio ya kisasa ya NIKO AMBAYE NIKO, iliyojikita katika kuwawezesha waimbaji wa muziki wa Gospel, kufikisha ujumbe wao kwa jamii, imetangaza neema kwa wale wanaotaka ‘kutoka’ kimuziki, kwa kuwapunguzia karibu nusu  ya gharama za kuandaa na kurekodi muziki. Ungana na Mkurugenzi wa Studio hiyo, yanye sifa za kimataifa, Steven Wambura, katika makala haya yanayokupa mwanga wa kile kinachoendele.

Katika Mahojiano maalumu na chanzo kimoja kimoja cha habari ofisini kwake Mwananyamala, Jijini Dar es Salaam, Wambura ambaye pia ni mwimbaji wa muziki wa Injili, mpiga ala na muongozaji, lakini pia aliyejikita kikamilifu katika biashara mbalimbali, alisema kuwa, NIKO AMBAYE NIKO STUDIO,  imeamua kudhihirisha kwa vitendo kuwa, imedhamiria kuwainua watanzania wenye kiu ya kumwimbia Muumba wao.

“Lengo langu tangu mwanzo nilipoanzisha Studio hii, lilikuwa na linabaki kuwa hilo hilo, kusaidiana na wenzangu wenye ujumbe kuufikisha kwa jamii, ndio maana kwangu kupata fedha nyingi sio jambo la kipaumbele, naitazama huduma kwanza. Nafanya kila niwezalo kuhakikisha kuwa, nafikia lengo, katika kuzingatia hilo, nimeamua kuwapunguzia nusu nzima ya gharama za kurekodi, kuandaa, kupigiwa ala, na ushauri wa kibiashara na kiufundi wateja wangu wote,”alisema Wambura.
Mkurugenzi wa Studio, Steven Wambura
Alisema kuwa, Studio hiyo imezidi kujiimarisha kwa kumpata mtaalamu aliyebobea katika uzalishaji muziki (Producer), kutoka Dodoma, ambaye amekuwa chachu ya ubora wa kazi za Studio hiyo, ya kisasa zaidi jijini Dar es Salaam.
Alimtaja Producer huyo kuwa ni; Zakayo Shushu, ambaye  ni mtaalamu wa kuchanganya muziki na pia mshauri wa muziki ambaye amekuwa akiwasaidia  wasanii wengi waliofanikiwa na kazi zao kuwa lulu katika jamii.

“Mwaka huu tuna Program nyingi zilizolenga kuigusa jamii, kwa mfano; tumejipanga kuwasaidia wasanii ambao Albam zao zimedumaa, wako wengi ambao wamejaribu kutoka wakashindwa kutokana na makosa katika  hatua mbalimbali za uandaaji wa muziki.
Unajua muziki una hatua nyingi na kosa katika hatua moja tu linaweza kuifanya kazi isipokelewe na jamii kwa uzito wake hata kama maeneo mengine ni bora kiasi gani,”alisema Mkurugenzi huyo na kuongeza:

“Mtu anaweza kuwa na albam nzuri tu, lakini akakosea katika kuipa jina, au katika baadhi ya ala  na mpangilio wa mashairi na ikadumaa sokoni. Ninaposema kudumaa sokoni namaanisha, kutonunuliwa na wateja, haya mambo yanaendana sana, ili muziki wako ukubalike ni lazima kwanza upokelewe na jamii husika. Uguse hisia zao wainunue wasikilize ujumbe. Ni lazima muziki ukamilike kila eneo ndipo uiguse jamii  ivutwe kwa Yesu.


Aliziasa Kwaya, vikundi vya uimbaji, bendi na hata watu binafsi kutochezea ofa hiyo  kwa kuwa ni ya wakati tu, waende wakakutane na wenzao waliofanikiwa kimuziki.

Mbali na Studio, Wambura pia hujihusisha na Biashara ya kununua na kuuza magari  na tayari amefanikiwa kwa kiasi kikubwa. Akizungumzia biashara hiyo alisema: “Namshukuru sana Mungu, kwa kuwa alinipa fursa ya kumtumikia kwa njia nyingi, nimekuwa nikifanya biashara ya magari na kwa kweli nimefanikiwa kuwasaidia hata watumishi wengi kupata magari ya kisasa na bora  kwa gharama sahihi,” alisema Wambura na kuongeza:   “Hapa mjini mambo ni mengi na wengine wanatumia kutojua kwa wengine kama mtaji wa kuwaibia, lakini mimi nimejikita katika kuwahudumia wengine kwa hofu ya Mungu aliye juu.”
 
Wambura akifafanua zaidi alisema: “Nilianza taratibu lakini sasa nimefanikiwa kwa kiwango  cha juu nanunua na kuuza magari mengi tu, na kwangu mimi ubora na uaminifu ni silaha kubwa, hivyo nimekuwa wateja wengi na wengine wananiambia ….Wambura nataka Gari pesa sina zote nitaleta  nawaamini nawapa na wanalipa, hii ni kwa kuwa nafanya haya yote kwa kumwamini Mungu, kwangu mimi Mungu ni wa kwanza na mengine yanafuata.”

Niko ambaye niko studio ipo Mwanyamala A. eneo la Mwijuma, katika majengo ya kanisa la Pentekoste, karibu na Ofsisi za kikundi cha TOT,  na unaweza kuwasiliana nao kwa Simu namba:
0657-334006 au 0714-678544

Kwa wale wanaohitaji magari wanaweza kuwasilina na Steven Wambura kwa simu namba 0784-252522 au 0655-252522.
KARIBU NIKO AMBAYE NIKO uhudumiwe kwa upendo wa Kristo aliyehai.

No comments:

Post a Comment