Watumishi wa Mungu 30 kuikabili Kondoa

Watumishi wa Mungu wapatao 30 toka maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam, wanameanza kazi ya kuuvamia mji wa Kondoa kiinjili ikiwa ni katika mpango wa kupeleka Neno la Mungu katika vijiji vya Dodoma, kumnyang’anya shetani mateka na kutawala.

Akizungumza hayo Jijini Dar es salaam yaliyofanyika mwanzilishi wa huduma hiyo, Gospel For All People, (GFAP), Mchungaji Tumaini Chanjarika, alisema kuwa mpango huo umekamilika.

Mchungaji huyo alisema, timu hiyo imewasili wilayani Kondoa mwishoni mwa mwezi uliopita mwaka huu, ambapo mikutano itaanza rasmi katika vijiji vinne, watakuwa na ushuhudiaji wa nyumba kwa nyumba na jioni watafanya mkutano mkubwa wa injilii, katika vijiji hivyo.

“Safari ya Kondoa kwa sasa imekamilika, tuta chukua takriban mwezi mmoja, kuwaeleza watu wa vijiji vya wilaya hiyo habari za Yesu, kutakuwa na timu itakayotangulia wiki moja kabla, kisha timu ya pili itafuata, lengo ni kuwaleta watu kwa Yesu,” alisema Mchungaji Chanjarika. 

Alisema mara baada ya kufika wilayani humo zitagawanywa timu ambapo kila moja itakuwa na kijiji chake, na itafanya kazi hiyo ya kumkanyaga shetani wilayani humo pasi mzaha.

Mbali na hilo aliongeza kuwa, mikutano itachukua wiki tatu na semina kwa waongofu wapya wiki moja, huku akiamini kuwa kwa neema ya Mungu watayaona mafanikio makubwa katika kazi hiyo ya kuwaleta watu kwa Bwana ili kuachana na dunia iliyoharibika.

“Katika huduma ya Kondoa tutaingia nyumba kwa nyumba kushuhudia, lengo letu ni kuwaleta watu kwa Yesu, waache kuteswa na ibilisi baada ya mikutano ya vijijini timu zote zitaungana na kufanya mkutano mkubwa mjini Kondoa,” alisema Mchungaji Chanjarika.

Mbali na hilo Mchungaji huyo aliweka wazi kuwa bado wanakabiliwa na changamoto kadha wa kadha kama vile; upungufu wa fedha.

Aliongeza kuwa changamoto nyingine ni upungufu wa vyombo vya injili ambapo zinahitajika seti nne, pamoja na usafiri wa vyombo, hivyo kuwataka watumishi wa Mungu kujitoa kusaidia ili kazi ya Bwana isonge mbele.

Huduma hiyo alieleza kwamba ni endelevu, ambapo mara baada ya Kondoa, wana mikakati ya kwenda maeneo mengine kumhubiri Kristo.

Mwenyekiti wa (GFAP) Paul Kashaga, akitokea wilayani Kondoa kwa ajili ya utafiti kuwa bado kuna uhitaji mkubwa wa Neno la Mungu hasa vijijini, kutokana na kuzungukwa na dini ya kiislamu.

Aliongeza kuwa bado kuna umuhimu wa wadau wa injili kuelekeza macho katika wilaya hiyo, ikiwa ni pamoja na kujitoa kuwasaidia watumishi wa Mungu walioanzisha huduma katika maeneo ya vijiji vya Kondoa.   

Dhamira ya huduma hiyo, aliizungumzia ni kumtangaza Kristo katika maeneo mbalimbali ya Tanzania, ili watu wamjue Mungu kwa lengo la   kukomesha migogoro isiyo na tija inayoibuka kila kukicha katika taifa la Tanzania.

No comments:

Post a Comment