Ambassadors of Christ ndani ya Tamasha la Pasaka 2013

Katika Kuelekea Tamasha la Pasaka mwaka 2013 watakaokuja kuhudumu kwenye tamasha hilo imezidi kuongezeka na sasa Ambassadors of Christ wamethibitisha kuwepokatika Tamasha hilo

Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya tamasha hilo, Alex Msama amesema kuwa kwaya ya Ambassadors of Christ ya Kigali Rwanda inayotamba na albamu ya Mtegemee Yesu imethibitisha kushiriki tamasha hilo litakalofanyika Machi 31 mwaka huu jijini Dar es Salaam.

 “Watakuja kung’arisha tamasha la mwaka huu na wamejipanga vya kutosha kuhakikisha mashabiki wanapata burudani ya nguvu, nia yetu ni kuwa na wasanii wakubwa Afrika na hilo ndilo tutakalolifanya mwaka huu.


 “Kabla ya Jumatano tutatangaza msanii mkubwa mwingine ambaye bado tunaendelea na mazungumzo naye kuhakikisha mambo yanakuwa safi, ili aje kutumbuiza kwenye tamasha letu,” alisema Msama.

 Alieleza kuwa katika albamu yao hiyo ina nyimbo nane ambazo ni JY’ Ushima Uwite, Mtegee Yesu, Ndifuza Kugerayo, Iyana Iby’ Isi, Yesu Niwe Mungeri, Parapanda, Abasaruzi na Nenda.


 Wasanii wengine wa nje ya Tanzania ambao tayari wamethibitisha kushiriki tamasha hili ni , Ephraim Sekeleti wa Zambia na Solomon Mukubwa raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) anayeishi Kenya. Wasanii wa Tanzania ni Rose Muhando, Upendo Nkone na John Lissu.

 Tamasha la Pasaka litafanyika Dar es Salaam Machi 31 na  litaendelea Aprili mosi kwenye Uwanja wa Sokoine Mbeya, wakati Aprili 3 ni Uwanja wa Samora Iringa na Aprili 6 Uwanja wa Jamhuri, Dodoma na siku inayofuata itakuwa Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza

No comments:

Post a Comment