Vurugu zasababisha Kanisa kuchomwa Moto Zanzibar


Kwa kile kilichoonekana kuwa ni uvunjikaji wa Amani katika Visiwa Vya Zanzibar hasa kwa Jamii ya Wakristo inazidi kuwa tete baada ya Kanisa la TAG eneo la Kariakoo Visiwani Zanzibar linaloongozwa na Bishop Dickson Kaganga Visiwani humo kulipuliwa kwa kitu kinachosadikika kuwa ni bomu na kuteketeza sehemu kubwa ya madhabahuni mwa kanisa hilo na sehemu za Milango ya Kanisa hilo.

Kanisa hilo lililokuwa na uwezo wa kuchukua Waumini zaidi ya 1000 limechomwa moto ikiwa ni mara ya pili baada ya mara ya kwanza kitu kinachosadikika kuwa ni bomu kutupwa ndani ya kanisa hilo mwanzoni mwa mwaka huu na bomu hilo kushindwa kulipuka wakati wa Ibada.
 

                                                Gari iliyokuwa ikitumiwa na Pastor Dick

Baada ya Uchunguzi wa Polisi katika tukio la kwanza Polisi walisema bomu hilo lilokuwa na uwezo wa kuteketeza kila kitu kilichomo ndani ya Kanisa hilo lakini ajabu halikuweza kulipuka wakati lilikuwa tayari kwa kulipuka.

Kumekuwa na hali ya Sinto fahamu kwa Wakristo wengi wanaoabudu katika Makanisa Visiwani Zanzibar na kasi ya Serikali katika Kushughulikia masuala haya imekuwa si ya kuridhisha.

                                                      Pastor Dick alipokuwa akihojiwa leo na

No comments:

Post a Comment