Nabii Malisa Aliyekataliwa Coverage Kwenye Media Za Kikristo Atikisa Jiji La Dar-es-Salaam

Baada ya media za Kikristo katika Jiji la Dar-es-Salaam Kukataa kumpa Coverage ya Matangazo Nabii Malisa Kutoka Katika Jiji la Mwanza ametikisa Jiji la Dar-es-Salaam kwa Kuweza Kujaza Ukumbi wa PTA ali maarufu Karume Hall.
Nabii Malisa akimuhoji Mwanamama aliyekuwa amekuja na Mgongo Ya Kutembelea katika Semina Hiyo.

Gazeti la Nyakati pekee ndilo lililokuwa limetoa tangazo kwa ajili ya kuwaalika Watu katika Mkutano Huo Mkubwa iliofanyika katika Ukumbi wa PTA.

Nabii Malisa ambaye hana tawi lolote katika Jiji la Dar-es-Salaam lakini aliweza wakusanya Watu kuhudhuria katika Mkutano huo.
Kati ya Mambo yaliyoleta Utata katika Mkutano wa Nabii Malisa ni kitendo cha kualika watu ambao kwenda Kusafisha nyota zao zilizofifia. Blog ilimuuliza Mmoja wa viongozi wa kanisa moja kwanini hawakumpa ushirikiano Nabii Malisa alisema "Kwa watumishi wa Dar-es-Salaam tunafahamiana, huyu kijana Mwanza kwenyewe bado kuna utata wa huduma yake, kuingia kichwa kichwa kushirikiana nae pasipo kujua foundation teachings zake unaweza kuta unapoteza watu bure"
Umati Wa Watu Waliohudhuria Semina Ya Nabii Malisa Katika Ukumbi wa PTA 
Katika Siku 3 hizo wagonjwa kutoka hospitali mbalimbali katika Jiji la Dar-es-Salaama walipelekwa katika Ukumbi huo na kufunguliwa kwa uweza wa Nguvu za Mungu.
Akifundisha kuhusu nidhamu ya Pesa, Nabii Malisa alisema Watu wengi wamekuwa na nidhamu ya Pesa wakiwa hawana Pesa ama Zinapokuwa zimepungua, aliuliza watu waliohudhuria ni nani aliyewahi kuwa na nidhamu ya Pesa alipokuwa kwenye Neema, na watu walishindwa kutoa majibu. Nabii Malisa amemaliza Siku 3 za Kinabii siku ya tarehe 6 May, 2012 Katika Jiji la Dar-es-Salaam.

No comments:

Post a Comment