WAKATI UMEFIKA SASA KUPENDEKEZA WASHIRIKI WA AFRICA GOSPEL MUSIC AWARDS.

 


Kwa muda sasa watanzania wamekuwa hawajui lolote kuhusu namna ya kushiriki katika TUZO ZA MUZIKI WA INJILI BARANI AFRIKA(Africa Gospel Music Awards) ingawa wanapenda. Toka tuzo za Muziki wa injili Barani Afrika zilipoanza, mwamko kwa watanzania kushiriki umekuwa mdogo, na hii ni kutokana na sintofahamu kwa wadau wa muziki huo kuanzia kwa

1.Wanamuziki wenyewe
2.Mameneja wa wanamuziki hao
3.Waandishi wa habari na Kanisa kwa ujumla.
Hivyo basi Kuanzia tarehe 21st April 2012 mpaka 21May 201 ni muda wa kupendekeza washiriki na tumebakiwa na takribani wiki moja tu ya kupendekeza. Ili kupendekeza unatakiwa;

a)Uandike kategori ambayo unataka mwanamuziki wa injili kutoka Tanzania aingie
b)Jina la mwanamuziki mwenyewe kisha utume jina hilo na
c)kazi yake aliyofanya kwa mwaka 2011 April – 2012April na
d)sababu ya kumchagua kwenda kwenye email;
nominations@africagospelawards.com
Mfano

Category: BEST ARTISTE OF THE YEAR EAST AFRICA
I do nominate : Christina shusho from Tanzania
Song:Thamani ya wokovu wangu
Reason:Her songs has restores many souls to the Kingdom of GOD
Kisha unatuma kupitia email tajwa hapo juu
Vipengele(categories) ambavyo unatakiwa kuchagua mtanzania wa kutuwakilisha ni pamoja na;

1. GROUP/CHOIR OF THE YEAR
2. MALE ARTISTE OF THE YEAR
3. FEMALE ARTISTE OF THE YEAR
4. BEST ARTISTE OF THE YEAR EAST AFRICA
5. EVENT OF THE YEAR

Kwa kufanya hivyo utakuwa umemuwezesha mwanamuziki wa injili kutoka nchini kuingia kwenye Nomination pull ya Tuzo hizo. Tuzo hizo zinatarajiwa kufanyika tarehe 7th July 2012 jijini London nchini Uingereza, wakati zoezi la kupiga kura baada ya nomination list kutoka, litaanza tarehe 1May-30june 2012.

Watanzania, tuamke na Kuwapendekeza washiriki wa Tuzo hizi toka Nchini Tanzania ili tuweze kuinua Muziki wetu wa Injili. Kwa Pamoja tutafanikisha hili. Kwa kupata undani wa tuzo hizo unaweza Tembelea: http://africagospelawards.com/

No comments:

Post a Comment