MKUTANO WA CHRISTIAN BLOGGERS

Jumamosi tarehe 21 April, 2012 tumeona tukutane uso kwa uso pale karibu na Mlimani City Survey kuanzia saa 3 mpaka saa 5 asubuhi.

Madhumuni ya Kukutana ni kwanza kufahamiana sisi kwa sisi, lakini pia kujifunza kwa pamoja namna ya kuanzisha (kwa wale wanaoanza), Kuboresha muonekano wa blog zetu "Technical Part" Steve Jobs aliwahi sema "designing is not just what it looks like but how it works " .

Ninafahamu tunao Bloggers walio ughaibuni kwa sasa,kuna wengine wako nje ya Dar.. lakini ninaamini kuanzia hapa tutapiga hatua ya kupashana habari.

Ninatamani Jumamosi wale wenye nafasi tujitokeze, na kama kuna watu wa magazeti haya ya Kikristo una connection tafadhari tuwasiane kwa ajili ya kazi tunayotaka kufanya nao.

Pamoja na hayo kwa wadau wote wanaotembelea blogs za Gospel nchini wanaalikwa kwa ajili ya kutoa mchango wao ili kuboresha blogs za Injili nchini.Kumbuka, Blog Kama MADHABAHU inaweza KUUJENGA ufalme wa Mungu na pia inaweza kuuharibu.

Usikose mtumishi. 


No comments:

Post a Comment