Mwanamuziki wa Injili wa Tanzania anayeishi Nchini Sweden Rachel Sharp azindua Album yake ya kwanza siku ya jana.

Siku ya jana Mwanamuzi Injili wa Tanzania anayeishi Nchini Sweden, Rachel Sharp ameitambulisha albam yake mbele ya Wanahabari wa Kikristo. Utambulisho huo wa Albam umefanyika Nyumbani Kwake Tegeta nje kidogo ya jiji la Dar-es-Salaam.

Mwanamuziki huyo alisema albam hiyo yenye jina la "Ni Mungu Wa Ajabu" ina jumla ya nyimbo kumi zilizo katika mfumo wa CD na nyimbo 8 zilizo katika DVD.

Rachel anayeishi Malmo Sweden amewataka Wanamuziki Wa Tanzania Kutukuza asili yao na kuacha kuiga tamaduni za South Africa na Africa Magharibi na hata barani Ulaya. Akiongea na Waandishi Wa Habari siku ya leo Rachel alisema " Ipo haya ya watanzania Kuimba nyimbo zenye mahadhi ya Mdumange na Mdundiko ili kulinda radha halisi ya Kitanzania na Kuutangaza Muziki Wa Asili ya Kitanzania nje ya Mipaka Ya Tanzania".

Rachel Sharp kwa stage na dancers wake

Master Prophet C.J. Machibya akiiyombea kazi ya dvd na Audio
Rachel akiwatambulisha Baba mzazi na Mama mzazi

Upendo Kilahiro,Chavala,Uncle Jimmy na Rachel wakifanya performance siku ya jana.
Rache Sharp akisoma Press Release
Wakinadada wadau wa Muziki wa Injili na media wakiwa kazini kuhakikisha mambo event  hiyo inakwenda sawa

Wadau wa media wakiwa kazini kuhakikisha mambo yanekwenda sawa.

source:samsasali.blogspot.com

No comments:

Post a Comment