Mkesha wa Kusifu na Kuabudu pia Maombi katika Chuo Cha Mzumbe Morogoro.

Katika kuelekea kumaliza muhula katika Chuo cha Mzumbe Morogoro huwa wanaandaa usiku wa Kumsifu na Kumtukuza na Mungu pia kupata nafasi ya kujifunza Neno la Mungu na Maombi kutoka kwa mtumishi anayealikuwa katika usiku huo.

Mkesha huo wa Kusifu na Kuabudu ,Chuoni Mzumbe Morogoro.Ulindaliwa na Umoja wana CASFETA chuoni hapo,Wanachuo walipata kuombewa na vijana wengi walipata kuokoka na kumpa Bwana Yesu Maisha yao.

Apostle Ndegi kutoka huduma ya Living Water Centre Ministry ndiye alihudumu katika upande wa Neno katika Usiku huo,Pia kwa Upande wa Waimbaji walikuwepo Upendo Nkone,Filipo Rupia na
CASFETA Mass Choir

Apostle Ndegi kutoka huduma ya Living Water Centre Ministry


Apostle Ndegi akiwaogoza sala ya toba baadhi ya wanafunzi waliosikia Neno la Mungu katika Usiku huo na kuamua Kuokoka na kumpa Bwana Yesu Maisha yao pia walipata kuombewa
Mwenyekiti CASFETA Chuo cha Morogoro akizungumza katika usiku huo

Rais wa Serikali ya Wanafunzi wa Chuo cha Mzumbe akizumgumza kuwa stage hiyo hiyo siku si nyingi aliitumia katika kuomba kula ila usiku huo ilikuwa ikitumika katika Kumtukuza Mungu.
Mwimbaji Philip Rupia akiwa na backup ya CASFETA Mass Choir kwa stage
Upendo Nkone

No comments:

Post a Comment