Wanamuziki wa Injili wa Kimataifa Mbashaz watua London, Uingereza na kutembelea Ofisi za Ubalozi

Mheshimiwa Balozi, Peter Kallaghe, akipokea zawadi ya CD na DVD kutoka kwa Waimbaji wa mziki wa injili Flora Mbasha na Mumewe Bwana E. Mbasha. wakiwa nchini Uingereza, walitembelea Miji ya Glasgow, Chemsford na Reading.
Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Mheshimiwa Peter Kallaghe, akiwa kwenye picha ya pamoja na wanamuziki wa nyimbo za Injili Flora Mbasha na Mumewe Bwana E. Mbasha (Kulia), Askofu Ernest Irungu, ambaye ni Kiongozi wa nyimbo za Injili na ni Mkuu wa Chuo cha Vision College of Theology kilichopo London, Uingereza, mama Zest Irungu (mke wa Bishop Irungu) na Bibi. Mwambola, walipotembelea Ofisi za Ubalozi. Bwana na Bibi Mbasha wapo nchini Uingereza, wakitokea Amerika kujitangaza na kutangaza Injili.

 source:fullshangweblog.com

No comments:

Post a Comment