Mh.Dr Harisoni Mwakyembe amelitaka Kanisa kuhubiri Amani Nchini, ndani ya Living Water Center Ministy


Mh.Dr Harisoni Mwakyembe asema Amani izidi kuhubiriwa makanisani na kudumishwa Nchini,Maana inaisaidia Serikali katika kuhamasisha Amani na Upendo,nakuongeza kuwa Serikali inatambua na kuheshimu mchango wa Kanisa katika kutetea Amani na Upendo Nchi.

Hayo yamesemwa katika Kanisa la Living Water Center Ministry Kawe chini ya mtumishi wa Mungu Apostle Onesmo Ndegi lililopo Kawe siku ya jana alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kanisani hapo katika Ibada ya asubuhi ambapo alikuwa amearikwa kama mgeni rasmi katika shughuli ya kuchangia ujenzi wa Kanisa hilo la Living Water Center ambapo hakuja peke yake aliweza kuambatana na mke wake pia na Mbunge mwenzake Mh.Victor Mwamalaswa katika harambee hiyo.

Apostle Onesmo Ndegi ambaye ndiye kiongozi wa Kanisa hilo,akisisitiza suala la Amani na Upendo na kuitaka Serikali kutambua mchango wa Kanisa katika Suala zima la Amani na Upendo Nchini.
Pia aliongeza kwa kusema Watanzania sote ni wamoja tunapaswa kuachana na itikadi za Udini,Ukabira na Uchama baadala yake Kuangalia suala la Amani na Upendo kutufanya kuwa kitu kimoja.

Akaulizwa na waandishi wa habari anazungumziaje suala la vurugu za Zanzibar akasema anaitaka Serikali kuwa makini katika ufuatiliaji wa jambo hilo na wahusika wote watiwe chini ya vyombo vya sheria,hata kama inasemekana kuwa ni wahuni wanaofanya hiyo kama inavyodaiwa basi wakamatwe na kufikishwa mahakamani, akamalizia kwa kusema yote yanayo fanyika kisasi ni juu ya Bwana.

Akamalizia kwa kusema katika Serikali kuna ulegevu katika usimamiaji wa kanuni na sheria za Nchi kwa mujibu wa Katiba ya Nchi,hivyo ameitaka Serikali kuwa makini katika hilo.


Mh.Dr Harisoni Mwakyembe amelitaka Kanisa kuhubiri Amani Nchini, ndani ya Living Water Center Ministy
Mh.Dr Harisoni Mwakyembe asema Amani izidi kuhubiriwa makanisani na kudumishwa Nchini,Maana inaisaidia Serikali katika kuhamasisha Amani na Upendo,nakuongeza kuwa Serikali inatambua na kuheshimu mchango wa Kanisa katika kutetea Amani na Upendo Nchi.

Hayo yamesemwa katika Kanisa la Living Water Center Ministry Kawe chini ya mtumishi wa Mungu Apostle Onesmo Ndegi lililopo Kawe siku ya jana alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kanisani hapo katika Ibada ya asubuhi ambapo alikuwa amearikwa kama mgeni rasmi katika shughuli ya kuchangia ujenzi wa Kanisa hilo la Living Water Center ambapo hakuja peke yake aliweza kuambatana na mke wake pia na Mbunge mwenzake Mh.Mbunge Victor Mwamalaswa katika harambee hiyo.

Apostle Onesmo Ndegi ambaye ndiye kiongozi wa Kanisa hilo,akisisitiza suala la Amani na Upendo na kuitaka Serikali kutambua mchango wa Kanisa katika Suala zima la Amani na Upendo Nchini.Pia aliongeza kwa kusema Watanzania sote ni wamoja tunapaswa kuachana na itikadi za Udini,Ukabira na Uchama baadala yake Kuangalia suala la Amani na Upendo kutufanya kuwa kitu kimoja.

Akaulizwa na waandishi wa habari anazungumziaje suala la vurugu za Zanzibar akasema anaitaka Serikali kuwa makini katika ufuatiliaji wa jambo hilo na wahusika wote watiwe chini ya vyombo vya sheria,hata kama inasemekana kuwa ni wahuni wanaofanya hiyo kama inavyodaiwa basi wakamatwe na kufikishwa mahakamani, akamalizia kwa kusema yote yanayo fanyika kisasi ni juu ya Bwana.Akamalizia kwa kusema katika Serikali kuna ulegevu katika usimamiaji wa kanuni na sheria za Nchi kwa mujibu wa Katiba ya Nchi,hivyo ameitaka Serikali kuwa makini katika hilo.

Mwisho kabisha wa Ibada yalifanyika maombi yakiongozwa na Kiongozi wa Kanisa hilo Apostle Onesmo Ndegi kwa ndugu hao Mh.Dr.Harison Mwakyembe,Mke wake na Mh.Mbunge Victor Mwambalaswa ili Mungu aambatane nao katika kazi zao,kufanya kwa ujasili pia kuwa na hofu ya Mungu katika kutumika Serikalini.

Waziri wa Uchukuzi Mh.Dr Harisoni Mwakyembe  akizungumza katika Ibada kanisani hapo.
Apostle Onesmo Ndegi ambaye ndiye kiongozi wa Kanisa hilo akihubiri katika Ibada.

Mh.Dr.Harison Mwakyembe na Mh.Mbunge Victor Mwambalaswa
Mwenyekiti wa Kamati ya ujenzi kanisani hapo Mzee Tarimo,Mh.Dr.Harison Mwakyembe,Mke wake,Mh.Mbunge Victor Mwambalaswa na
Apostle Onesmo Ndegi ambaye ndiye kiongozi wa Kanisa hilo katika Ibada.
Baadhi ya watu kama Alex Msama,Mh.Diwani Janeth na wengine walihudhulia katika ibada hiyo na kutoa mchango wao katika ujenzi wa Kanisa
Mh.Dr Harisoni Mwakyembe akizungumza na waandishi wa habari waliofika  Kanisani hapo.




Apostle Onesmo Ndegi ambaye ndiye kiongozi wa Kanisa hilo akizungumza na waandishi wa habari waliofika  Kanisani hapo

Kiongozi wa Kanisa hilo Apostle Onesmo Ndegi na akiwaongoza wachungaji wengine kufanya maombi kwa  Mh.Dr.Harison Mwakyembe,Mke wake na Mh.Mbunge Victor Mwambalaswa ili Mungu aambatane nao katika kazi zao,kufanya kwa ujasili pia kuwa na hofu ya Mungu katika kutumika Serikalini.

No comments:

Post a Comment