Wabunge 400 wapiga kura kumkataa Mungu..!

Majira ya saa moja jioni, Januari 5, mwaka  huu, jumla ya wabunge 575, walipiga kura kuamua kumpendeza Mungu au shetani,  400 miongoni mwao wakamchagua shetani na 175 tu waliosalia wakamng’ang’ania Mungu na maadili yake.

Kwa mujibu wa shirika la habari la Life Sitenews.com wale waliosalia na msimamo wa kupiga kura kuharibiwa kwa maadili ya mwanadamu na sheria za Mungu, wameapa kutokaa chini, watapambana hadi mwisho ufike.

Mbunge wa eneo la Tory, Roger Gale, aliwashutumu wale wanaounga mkono hoja hiyo akisisitiza kuwa hawana msingi wa hoja yao badala ya kushikilia dai la usawa.

“Ni vigumu sana kutafsiri dhana ya ndoa, huu ni Muungano wa mwanamume na mwanamke wenye historia ndefu sana, na kamwe serikali haiwezi kutafsiri na kuirekebisha ili kukidhi matakwa yao na tama zao,” alisema Gale.

Lakini wakati hayo yakiendelea, mbunge mwingine aliliambia  Gazeti la The Sun kuwa Waziri Comeron anashutumiwa tu kwa kutoa mdomoni mwake tamko ambalo ni mpango wa Jumuiya ya Ulaya.

“Nawaambia ukweli kuwa ifikapo katikati ya mwaka huu sheria ya kuunga mkono ndoa za mashoga itatolewa na kuwa amri kwa wanachama wote na baadaye kuenea katika ulimwengu wote,” alisema na kuongeza:

“Utaratibu wa siri uliofanywa na kamati maalumu ya Jumuiya ya Ulaya utalazimisha mataifa yote duniani kubadili sheria zao za ndoa ili ziendane na sheria ya haki za kiutu zinazokubaliana na haki za usawa kibinadamu. Kura ya kupitisha azimio hilo itapigwa Novemba mwaka huu katika Bunge la Ulaya.”

No comments:

Post a Comment