Masanja,Bukuku,Mbasha Kutinga Tamasha la Kufunga Mwaka EAGT City Centre


Mwaka 2013 untaraajia kuupisha kiti mwaka mpya wa 2014 kwa kishindo cha tamasha maalumu lilpewa jina la anza mwaka na Bwana, litakalopambwa na waimbaji maarufu wa muziki wa injili nchini.

Kwa mujibu wa mchungaji Floriani Kantuzi wa kanisa la Evangestic Assembleis of God (EAGT – CITY) waimbaji watakaopamba tamashahilo ni pamoja na Emanueli Mgaya (a.k.a Masanja mkandamizaji), Bahati bukuku Florah Mbasha, Bon Mwaitege, Christian Matai, Neema Mwaipopo na jane Misso wengine ni Jenifer Mgendi, Kabula George, Martha Mwaipaja na Neema Gaspar na wengineo. Kwaya zinazotajwa kushiriki ni pamoja na Chang’ombe, Bethel na Majestic.

Mchungaji Floriani Kantuzi wa Kanisa la Evangestic Assembleis of God(EAGTCITY CENTRE)

Mchungaji Katunzi aliliambia gazeti hili mwishoni mwa wiki kwamba tamasha hilo limekusudiwa kuwapa watu fursa ya kumshuru mungu kwa ulinzi wa mwaka unaomalizika na kuwapa kibali cha kuuona mwaka mpya.

Kwa mujibu wa Mchumgaji Kantunzi kiingilio katika tamasha hilo pia kitahesabiwa kuwa mchango maalumu wa ujenzi wa jingo la kuabudia kwa ajili ya kanisa la EAGT- CITY CENTRE, Hivyo watakuwa wamepiga ndege  wawili kwa jiwe moja, ibada ya shukrani ya utoaji.

Viingilo katika tamasha hilo vinaanzia  na kiwango cha shilingi 5,000/= kwa watoto na wakubwa shilingi 10,000/=, viti maalumu shilingi 20,000/= na VIP 50,000/=. Kanisa la

EAGT- CITY CENTRE, lilianzishwa mwaka 2007 katika jiji la Dar es salaam, na tangu wakati huo limekuwa likisali katika kumbi mbalimbali ikiwemo viwanja vya Nyerere  (SABASABA) vilivyoko katika barabara ya kilwa ambako kwa zaidi ya miaka mitano sasa.

Mchungaji Katunzi alisema tayari kanisa lake limefanikiwa kupata uwanja wenye ukubwa wa eka saba na nusu kwa ajili ya ujenzi wa jingo la kuabudia na kwamba malipo yote pamoja na maandalizi mbali mbali vimegharimu karibu shilingi milioni thelathini.

 Watakao viingilio na kuhudhuria tamasha hilo la kufunga mwaka watakuwa wameanzisha safari ya ujenzi wa jingo lilokusudiwa kuingia watu wapatao 20,000/=.

Bahati Bukuku

Emanueli Mgaya (a.k.a Masanja mkandamizaji)



No comments:

Post a Comment