Love Tanzania Festival yazidi kukamilika baada ya Mwinjilisti Andrew Palau Kuwasili Nchini

Mwinjilisti na Mwandaaji wa Love Tanzania Festival Andrew Palau  amewasili nchini tayari kwa ajili ya tamasha linalotegemewa kuwa kubwa ambalo halijawahi kutokea Nchini Tanzania hapo mwanzo.

Jana siku ya Jumapili Andrew Palau alihubiri  katika kanisa la City Christian Center (CCC) Upanga pia ibada hiyo ilirushwa live kupitia kituo cha Radio cha Clouds FM ambayo ilikuwa inasikika Duniani Kote.

Mwinjilisti Andrew Palau amewasili na timu yake kwa ajili ya Tamasha hilo kubwa la Love Tanzania Festival litakalofanyika katika Viwanja vya Jangwani siku ya tarehe 11/12 August, 2012.

Pia kuanzia tarehe 11hadi12 Andrew Palau na waimbaji wengine wa Kimataifa kama Lubben, Don Moen and Nicolle watakuwa wakihudumu pamoja,Waimbaji wa Tanzania watakao hudumu ni Christina shusho, Masanja, The Voice na Upendo Kilahiro.atakuwa katika viwanja vya Jangwani akihudumu.

Mwainjilisti Andrew Palau akihubiri katika Ibada ya Jana siku ya Jumapili  CCC Upanga

Bishop Mwenisongole wa Kanisa la CCC  akiongoza maombi na Mwainjilisti Andrew Palau katika Ibada siku ya jana.
Lubben akihudumu  katika kanisa la CCC Upanga akishirikiana na Praise Team

No comments:

Post a Comment