Dk. Barnabas Mtokambali aibuka mshindi katika uchaguzi Mkuu wa Kanisa la TAG uliofanyika Dodoma.

Katika kile kilicho kuwa kinasubiliwa kwa mda katika swala Uchaguzi Mkuu wa Kanisa la TAG kumchagua Askofu mkuu wa Kanisa la Tanzania Assemblies of God(TAG), ambao unafanyika kila baada ya miaka minne unaoambatana na uchaguzi wa viongozi wa ngazi mbalimbali uliofanyika mkoani Dodoma.Hivi sasa matokeo yaliopatikana kwa masaa machache yaliyo pita ni kwamba Dk. Barnabas Mtokambali  aliyekuwa ameshika kiti hiko kwa muda wa miaka minne aibuka tena kidedea kwa asilimia 93 baada ya kuwa ameamua kukitetea kiti hicho kwa mara nyingine tena,Hivyo atakuwa Askofu mkuu wa Kanisa la Tanzania Assemblies of God (TAG) kwa miaka minne tena.

Dk. Barnabas Mtokambali
 

Ushindi huo ambao ameupata mara baada ya wachungaji 20119 kuandika majina ya kumpendekeza atakayegombea nafasi hiyo ili aweze kupigigiwa kura ambapo kabla haijafika katika mchakato huo wa kura hatimaye aliibuka kidedea kutokana na jina lake kurudia mara 1969 ambapo ni sawa na asilimia 93 kwa mujibu wa kanuni za uchaguzi wa Viongozi katika Kanisa hilo.

Awali kabla ya mchakato huo kuanza Askofu Dk. Mtokambali alitoa hotuba kali ya wachungaji kuacha kuenenda ki binadamu na kwamba waache kupiga kampeni na kutoa, kupokea Rushwa.

Pia kwa nafasi ya Makamu Askofu ndio hatua iliyofuata baada ya kumpata Askofu Mkuu ambayo ilikuwa ikigombewa na wachungaji kadhaa lakini hatua zilivyozidi kusonga walikuwa wakijitoa hadi mwisho kubaki wawili.Waliowania nafasi hiyo ambapo Magnus Muhiche na Raulent Kameta ndio walio wania kiti hicho,Magnus Muhiche kuibuka Mshindi kwa kura 1398 na Raulent Kameta kupata kura 618 hadi anapatikana mshindi inasemekana imerudiwa mara nne (4),walikuwa hawafikii asilimia zilizokuwa zinamfanya mtu kuwa mshindi,
Ron Swai ndiye aliyeibuka mshindi katika nafasi ya Katibu Mkuu wa Kanisa.Chanzo cha habari kikizungumza na blog hii katika kubainisha hayo!

No comments:

Post a Comment