Love Tanzania Festival kuacha historia Tanzania

Love Tanzania Festival imeweka historia katika Nchi ya Tanzania Baada ya kumalizika kwa kufanya maajabu katika Festival hiyo katika viwanja vya Jangwani Jijini Dar es salaam.

Love Tanzania Festival ilikuwa imeandaliwa na mtumishi wa Mungu  Andrew Palau imeshilikisha wachungaji kutoka makanisa mbalimbali Nchini,Mtumishi wa Mungu Andrew Palau katika event hiyo alihubiri na idadi kubwa ya Watanzania kuokoka na kumpa Yesu Maisha yao.

Love Tanzania Festival pia ilitawaliwa na Massanja Mkandamizaji wa Original Comedy kwa kile alichofanya kwa kuushuhudia umati wa watu kuwa ameokoka na Yesu ni Bwana katika maisha yake

Pia wanamuziki wa Tanznia waliojumuika katika Love Tanzania Festival ni Christina Shusho,Upendo Kilahiro,Pastor safari na team aliyokuwa anaiongoza.

Kwa upande wa wa waimbaji wa Kimataifa alikuwepo Don Moen,Dave Lubben na Nicolle C Mullen 
ambao katika event hiyo walikuwa wakishilikiana na umati wa watu ulikuwa ukiimba pamoja nao kutokana na idadi ya kubwa ya watu kuwa wanajua nyimbo zilizokuwa zikimbwa katika tamasha hilo.
Andrew Palau Mwinjilisti wa Kimataifa na mwandaaji wa Love Tanzania Love Festival

Andrew Palau Akihubiri katika Love Tanzania Love Festival

 Dave Lubben


                                                                         Don Moen


Watu na hawakusita kutumia simu na Ipad zao kuchukua kumbukumbu za Don Moen




 
Nicole C Mullen


Christina Shusho na  Upendo Kilahilo wakiwakilisha kwa stage
Watu wa  Mataifa mbalimbali walijitokeza kumtukuza Mungu katika Love Tanzania Festival
Maelfu ya watu walimpokea Yesu kama Bwana na Mwokozi wa Maisha yao
Massanja Mkandamizaji wa Original Comedy hakusita kuushuhudia umati wa watu kuwa ameokoka na  aliyotendewa na Yesu katika maisha yake.
The Voice na Don Moen
Christina Shusho na  Upendo Kilahilo wakibadilishana mawazo na Nicole C Mullen



No comments:

Post a Comment