Sara Mvungi Mwamziki wa nyimbo za Injili azindua Album yake ya Kwanza.


Sara mvungi maarufu kama "Honey" katika tasnia ya filamu pia ni  mwimbaji wa nyimbo za injili siku ya Jumapili alizindua album yake ya kwanza ya nyimbo za Injili iitwayo "NIACHENI NIMFUATE YESU",Uzinduzi huo ulifanyka katika Kanisa la Akuzamu Ministry Posta katika Jego la IPS.


Katika Tamasha hilo Mgeni Rasmi alikuwa Mkurugenzi wa Mariedo Boutique Rose Mary Edward ambaye ni mke wa Mchungaji Kiongozi wa Huduma Akuzamu Ministry.
Uzinduzi huo ulisindikizwa pamojana na wanamuziki mbalimbali kama Enock Jonas, Afande Bupeh, Msasani kwaya, Amani kwaya toka Yombo, Madam Ruth na wengine wengi

 Pia uliudhuliwa na wasanii wa Bongo Movie kama Irene Uwoya,Dotinata,Tino Kutoka Star tv mtangazaji wa Kipindi cha Bongo Beat Sauda Mwilima, ITV alikuwepo mtangazaji wa Kipindi cha Hawavumi lakini wamo pia alikuwepo kuwakilisha bila kumsahau Maimatha wa Jesse.

Uzinduzi huo wa Album uliambatanna na uchangishaji wa fedha ambazo asilimia flani zitakazo kwenda kusaidia watoto wanaoishi kwenye mazingira .


Nikizungumza na Sara Mvungi  kwa njia ya simu kanieleza  kuwa Album yake ina nyimbo 9,akiwa amewashirikisha waimbji wengine kama Enock  Jonas,Stela Swain a Mtoto wake aitwae Neema katika album hiyo

Mgeni Rasmi alikuwa Mkurugenzi wa Mariedo Boutique Rose Mary Edward akiwa na Mme wake Mchungaji Kiongozi wa Huduma ya Akuzamu Ministry.

Watumishi wa Mungu mbalimbali walioudhulia uzinduzi huo.
Maimatha  Jesse
Kutoka Star tv mtangazaji wa Kipindi cha Bongo Beat Sauda Mwilima
Kutoka ITV alikuwepo mtangazaji wa Kipindi cha Hawavumi lakini wamo aliye changia kwa kiasi kikubwa katika huduma ya Sara Mvungi

Mwimbaji wa Nyimbo za Injili Afande Bupe
Mtumishi wa Mungu Dotinata
Irene Uwoya
Vikundi mbalimbali vilialikwa kuhudumu katika uzinduzi huo
Kwaya mbalimbali zilialikwa kuhudumu katika uzinduzi wa Sara Mvungi
Wadau wengi walijitokeza kuhudhulia uzinduziwa huo


Akabebwa na washabiki wake juu juu...!

No comments:

Post a Comment