Rose Muhando ndani ya Uwanja wa Kaitaba Mjini Bukoba

Rose Muhando Mwimbaji nyota wa muziki wa injili nchini  pamoja na waimbaji wenzake waliweza kulipendezesha tamasha kubwa la Shangwe Kagera zilizofanyika katika uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba na kukusanya mamia ya wakazi wa mji huo pamoja na viongozi wa dini na serikali.

Tamasha hilo liliandaliwa na kampuni ya Beula Communication kwa lengo la kukusanya fedha ili kuwasaidia watoto wanaoishi katika mazingira magumu mkoani Kagera.

Kati ya viongozi waliohudhuria tamasha hilo ni pamoja na mkuu wa wilaya Bukoba bibi Zippora Pangani, bwana Melkzedek Mutayabarwa ambaye ndiye kiongozi wa kampuni ya Beula iliyoandaa tamasha hilo pamoja na wauguzi kutoka kituo cha watoto cha Tumaini cha mjini humo.


Rose Muhando  pamoja na waimba wake
Rose Muhando akiimba mbele ya viongozi wa Dini na viongozi wa serikali walioudhulia katika event hiyo.



   
SOURCE: gospelkitaa.blogspot.com

No comments:

Post a Comment