Mkesha wa Kuliombea Taifa la Tanzania wafana.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Uhusiano na Uratibu, Stephen Wasira amesema kuwa amani iliyopo Tanzania inatakiwa itumike kupambana na ufisadi.

Pia amesema amani ambayo ni haki ya kila mtu na Taifa la Tanzania inatakiwa itumiwe kudumisha haki kwani amani ni tunda la haki.

Waziri Wasira alisema kuwa mwaka 2013 ni mwaka wa kuhakikisha amani ambayo pacha wake ni maendeleo vinalindwa kama mboni ya jicho.

Mkesha huo uliozihusisha taasisi za dini ya Kikristo 50 ziliongozwa na Askofu Emmanuel Malasi ambaye katika maneno yake kubwa alilokuwa akisisitiza ni kudumisha, amani, upendo na uvumilivu.

Kwenye mkesha huo wa kuuaga mwaka 2012 na kuukaribisha mwaka 2013 walihudhiria viongozi mbalimbali wa Serikali akiwemo, Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dodluck Ole Medeye na Mbunge wa Viti Maalumu Mbeya, Dk. mary Mwanjelwa.

Pia zilikuwepo nafasi za uwakilishi katika idara na mashirika mbalimbali ya kimataifa huku ubalozi wa Marekani nao ukiwakilishwa na Elizabeth Petro.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Uhusiano na Uratibu), Stephen Wasira (katikati), akipunga bendera pamoja na viongozi wengine wa Dini,Katika Mkesha huo uliofanyika uwanja wa Taifa Dar es Salaam siku ya amkesha wa mwaka mpya Wasira alimwakilisha Rais Jakaya Kikwete katika mkesha huo.

Baadhi ya viongozi wa Serikali walioudhlia mkesha huo uwanja wa Taifa ni Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Goodluck Ole Madeye (kulia), Balozi Mdogo wa Marekani nchini, Elizabeth Petro (kushoto), na Mbunge wa viti maalumu (CCM), Mbeya mjini Dk. Mary Mwanjelwa wakiwa kwenye ibada hiyo.

Waumini wa dini ya Kikristo walioudhulia mkesha huo wakishangilia na kumshukuru Mungu baada ya kuvuka mwaka mpya.

No comments:

Post a Comment