Nabii Flora Peter ataka amani idumishwe nchini


Kiongozi wa Kanisa la Huduma ya Maombezi, Nabii Flora Peter
Watanzania wametakiwa kudumisha na kuithamini amani ya nchi iliyopo badala ya kuiharibu kwani kuirudisha kwake ikitoweka itachukua muda.

 Wito huo ulitolewa na Kiongozi wa Kanisa la Huduma ya Maombezi, Nabii Flora Peter alipokuwa akihubiri katika siku chache zimepita katika ibada ya Krismasi katika Kanisa hilo lililoko Mbezi SalaSala Dar es salaam juzi.

“Kuwa na amani ni jambo jema kwa wananchi wote na dini zote lakini kuharibu amani ni jambo ambalo halimpendezi mungu” alisema Nabii Flora

Alisema Tanzania inajivunia amani iliyopo ambayo imedumishwa na wanzania wenyewe hivyo kila mmoja mwananchi ana wajibu wa kuitunza.

Alisema mahali palipo kosekana amani hakuna jambo lolote linaloweza kufanyika ikiwa pamoja na kuabudu kwani mifano halisi inaonekana katika nchi zenye machafuko kama vile somaria, Siria na nyinginezo.

“Katika nchi hizo watu wanahitaji kuabudu kama tulivyo sisi lakini wanashindwa kwa sababu hakuna amani hivyo tuidumishe amani tuliyo nayo” aliongeza Nabii Flora.

Alisema amani ya Tanzania idumishwe ili mataifa mengine yaje kujifunza kwetu kuliko kuiacha ikapotea kwa kugombana baina ya dini moja na nyingine.

Alisema Tanzania imekuwa ni nchi ya mfano na gumzo kwa nchi nyingine kutokana na wananchi wake kuwa na upendo na utulivu wa kipee hata mtu akiwa nje ya nchi anakuwa kifua mbele kusema anatoka Tanzania hivyo ni jambo la kujivunia.

 Katika hatua nyingine  Nabii Flora amewataka waananchi wote bila kujali imani za dini zao kujitokeza kushiriki mchakato wa kujadili katiba mpya kwani ndiyo dira ya nchi yetu.

Alisema ni vizuri watu mbalimbali wakajadili kwa kina mchakatio wa katiba mpya badala ya kujadili chama kwani katiba ndiyo itakayaotuongoza kwani suala hilo ni letu sote na si la mtu au kundi fulani.

   Nabii Flora alitumia fursa hiyo kwa kumpongeza Rais Jakaya Kikwete kwa kukubali kupitisha mchakato wa katiba mpya pamoja na kuweka uhuru kwa kila mwananchi kufanya jambo lake kwa uhuru pasipo kuvunja sheria.

” Kila mtu anaona utawala wa Rais Kikwete jinsi unavyofanya kazi kwa uwazi na kasi kubwa na ndiyo maana kila idara na taasisi imepewa nafasi ya kuamua na mamuzi hayo yanaheshimiwa na kila mtu kwa maslahi ya Taifa” alisema Nabii huyo.

No comments:

Post a Comment