Idadi ya Watanzania kujulikana leo

Idadi  ya Watanzania itajulikana leo wakati Rais Jakaya Kikwete atakapolihutubia Taifa kwa ajli ya kuuaga mwaka 2012 na kuukaribisha mwaka 2013 kupitia vyombo vya habari.

Pamoja na mambo mengine, Rais Kikwete atatangaza idadi ya Watanzania ikiwa ni hatua ya kukamilisha zoezi la sensa ya watu na makazi iliyofanyika nchini Agosti hadi Septemba, mwaka huu.

Sensa hiyo ilianza Agosti 26 na ilitarajiwa kumamilika Septemba Mosi, lakini kutokana na changamoto zilizojitokeza, ilisogezwa mbele kwa siku saba na hivyo, kukamilika Septemba 8.

Miongoni mwa changamoto zilizolikabili zoezi hilo ni baadhi ya vikundi vya dini kuwahamasisha wafuasi wao wasihesabiwe, makarani kugoma kutokana na kucheleweshewa au kukatwa posho, vifaa kuchelewa kufikishwa katika maeneo pamoja na maeneo mengine kupokea vifaa vichache.

Kwa mara ya mwisho, Tanzania ilifanya sensa ya watu na makazi mwaka 2002, ambayo ilibainisha kuwa nchi ilikuwa na watu milioni 35.

Hivi sasa Tanzania inakadiriwa kuwa na watu wapatao milioni 40.

Changamoto, ambazo serikali ilikumbana nazo, mafanikio yaliyopatikana na matarajio kwa mwaka ujao wa 2013.

No comments:

Post a Comment