Viongozi wa Dini wataka mihadhara ikomeshwe

Viongozi wa Dini nchini wameiomba Serikali na taasisi zinazohusika kufuta mihadhara ya dini ili kuepusha migogoro inayoweza kujitokeza.

Wakizungumza wakati wa warsha ya kujadili nafasi ya dini katika kulinda na kudumisha amani, viongozi hao  walisema mihadhara ya dini ni moja ya sababu zinazoweza kuchangia kutokea kwa migogoro nchini.

“Ni lazima tuchukue tahadhari kabla migogoro haijatokea sababu kila jambo huanza taratibu...hata mauaji ya kimbari yalianza hivi," alisema Mkurugenzi wa Kanisa la Huduma ya Maombezi, Peter Mitimingi.

Alisema suala la dini ni kama kidonda kilichofunikwa kwa kitambaa na kikifunuliwa kitaleta madhara makubwa kwa nchi.

Kwa upande wake,  Mhadhiri wa Chuo cha Kiislamu Morogoro, Abdallah Tego,  alisema matatizo yanayojitokeza katika nchi yanatakiwa kutatuliwa haraka ili kuepusha migogoro.

“Tunaomba serikali ichukulie suala hili kwa uzito na kulitatua kwa haraka kabla hakujatokea madhara," alisema.



No comments:

Post a Comment