Tamasha la Praise in the City funga kazi 2012


 Praise in the City tamasha lililoandaliwa na Kanisa al Living Water Makuti Kawe jijini Dar es salaam limefanyika kama ilivyopangwa na kuwa barika wengi waliohudhuria katika ukumbi wa Diamond jubilee ambako limefanyika tamasha hilo.

Waimbaji kama John Lisu, Glorious Celebration,R.I.O.T Dancers walipata kuhudumu katika Tamasha hilo,Living Waters ndio waandaaji wa tamasha hilo pamoja na waimbaji wengine waliweza kuwabariki wengi kwa uimbaji wao wa viwango mbele za Mungu, pia katika tamasha hilo kulifanyika live recording ya kundi la Living Waters ambao waliimba nyimbo takribani kumi na saba.

Akizungumza katika Tamasha hilo Kiongozi wa Kanisa la Living Water Center Kawe Mtume Onesmo Ndegi amesema pamoja na changamoto walizopitia katika maandalizi ya Tamasha hilo wanamshukuru Mungu kwa kufanikisha tukio hilo la aina yake,aliongeza kwa kusema kulingana na Tamasha hilo kuwa la baraka kwa watu wengi litakuwa jambo la mwendelezo. 

 Mtume Onesmo Ndegi Kiongozi wa Kanisa la Living Water Center Kawe

Waandaaji wa Tamasha hilo Living Waters kutoka Kanisa la Living Water Center Kawe

Filipo Rupia akiwa na Living Waters


John Lisu
Glorious Celebration

R.I.O.T Dancers

Ma Mc wa Tamasha hilo Papaa ze Blogger na Rose Mushi

No comments:

Post a Comment