Aliyefugwa kwa kukojolea Kura’n atinga Mahakama Kuu

Rufaa ya msichana Eva Abdallah anayetumikia kifungo cha miaka miwili jela kwa kosa la kukojolea Kura’n imefikishwa Mahakama  Kuu jijini Dar es Salaam, ambapo wiki iliyopita ilitolewa amri ya kusafirishwa kutoka gereza la Bagamoyo mkoani Pwani na kuletwa jijini Dar es Salaam.

Katika rufaa hiyo namba 132, ya mwaka 2012, iliyopo mbele ya Jaji Dk. Fauz. mrufani Eva anawakilishwa na mawakili wawili chini ya usimamizi wa taasisi ya Bibilia ni Jibu.

Uchunguzi wa chanzo kimoja cha habari hii umebaini kuwa Wiki iliyopita Jaji Dk. Fauz, alitoa amri ya mrufani kusafirishwa kutoka katika gereza anakotumikia kifungo chake huko Bagamoyo  na kufikishwa Mahakama Kuu, Jumanne saa nne asubuhi tayari kwa ajili ya usikilizwaji wa rufaa hiyo.

Hata hivyo, Jumanne iliyopita mawakili wa pande zote pamoja na wanaofuatilia shauri hilo walifika mahakamani  na shauri iliaanza kusikilizwa, lakini mrufani hakufikishwa mahakamani.

Karani wa Mahakama alimweleza Jaji kuwa amri yake ilitekelezwa na uongozi wa Magereza uliahidi kumfikisha mahakamani siku hiyo. Baada ya maelezo hayo mawakili wa pande zote mbili walijaribu kumshawishi Jaji kesi isikilizwe wakati bila mrufani kwa kuwa mawakili wake wangemuwakilisha, lakini aliwaeleza kuwa angependa rufaa iendelee wakati Eva akiwepo.

Baada ya msimamo huo walikubaliana kuahirisha shauri kwa muda ili kutoa nafasi kwa mrufani kufika, hata hivyo baada ya kusubiri kwa muda mawakili waliitwa tena kwenye chumba cha mahakama ambapo mjadala wa hoja zinazojadiliwa kwenye rufaa hiyo.

Jaji aliwaambia mawakili kuwa iwapo mrufani angefika mahakamani basi shauri hilo lingesikilizwa na hata kufikia mwisho siku hiyo.
Hata hivyo Karani wa Mahakama alimjulisha Jaji kuwa uongozi wa Magereza umeahidi kumhamishia Eva kwenye gereza la Segerea ili iwe rahisi kupelekwa mahakamani.

Baada ya majadiliano Jaji aliahirisha shauri hilo hadi Januari tisa saa nne asubuhi ambapo mrufani atafikishwa mahakamani akitokea Gereza la Segerea.

Eva anatetewa na Mawakili wawili ambao ni Mark Lebba na Barnaba Luguwa, wakati upande wa Jamhuri (Mjibu rufani) unawakilishwa na Wakili wa serikali, Mwakamale.
Eva alihukumiwa kifungo cha miaka miwili jela, Agosti mwaka huu baada ya kutiwa hatiani na mahakama ya Wilaya ya  Bagamoyo.

Inadaiwa kuwa Eva ni mtoto wa imamu mmoja huko Luhangwa, lakini aliisikia Injili ya Bwana Yesu Kristo akaiamini na kuikimbia hukumu ya Mungu kwa kuokoka katika kanisa la Pentekoste Bagamoyo.
Wito umetolewa kwa Wakristo kuingia katika maombi ili kumuombea binti huyo anayeteseka gerezani.

Source Jibu la Maisha










No comments:

Post a Comment