Debora Ntepa, Tunu Pinda kuteta na wanawake, Mabinti Diamond Jubilee


Mchungaji Deborah Ntepa wa Huduma ya The Palm of Deborah kwa kushirikiana na huduma ya Oasis of Healing Ministry, ya Ubungo jijini Dar es Salaam, anatarajia kuwa na kongamano la aina yake la wanawake na mabinti katika ukumbi wa VIP wa Diamond Jubilee kwa siku mbili.

Kongamano hilo ambalo mgeni ramsi atakuwa ni mke wa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Bi. Tunu Pinda na Mhe. Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Sophia Simba; litakuwa ni la kinabii juu ya maendeleo ya wanawake na mabinti wa kitanzania.

Wanenaji watakaokuwa katika kongamano hilo kubwa ni kutoka nchi mbalimbali wakishirikiana na Mchungaji Deborah Ntepa.

Vitabu mbalimbali vya Mchungaji Deborah Ntepa, vilivyoandikwa kwa umahili mkubwa kupitia uvuvio wa Roho Mtakatifu vitauzwa katika kongamano hilo.

Chakula cha mchana kitatolewa siku ya Jumamosi bure

Kongamano hilo la siku mbili litafanyika  Septemba 8-9, 2012.

Mchungaji Deborah Ntepa
Bi. Tunu Pinda

Mhe. Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Sophia Simba
KWA MAWASILIANO ZAIDI:

Email:
ancientntepa@hotmail.com
deborahpros@hotmail.com

                   SIMU:  
0713 - 212 440; 0715 - 029 602
0755 - 029 602.

No comments:

Post a Comment