Jaji Warioba awaasa wakristo kupendana

Wakati Tume ya  Marekebisho ya Katiba ikiwa imeianza kukusanya maoni  katika Halmashauri ya Jiji la Mwanza,  Mwenyekiti wa tume hiyo,Jaji Joseph  Warioba, amewakumbusha Wakristo kupendana na kusaidiana na serikali kupunguza migogoro.

Mwenyekiti wa tume Tume ya Marekebisho ya Katiba, Jaji Joseph Warioba.
Alitoa wito huo wakati   akizungumza   kwenye  uzinduzi  wa sherehe  za miaka 50  tangu  kanisa la Anglican (ACT) lilipoanzisha  Dayosisi ya Victoria Nyanza (DVN), mkoani Mwanza.

“ Ni  vyema  sisi waumini wa  Kikristo, tukaonyesha  utaifa kwa kutekeleza kwa vitendo amri mbili kuu  zilizotolewa na  Yesu Kristo , ikiwemo ya kututaka tuwapende jirani zetu kama nafasi zetu. Tukifanya hivyo, tutaondokana  na hii tabia  imbayo imenza kujengeka  hapa nchini; yaani  ubinafsi” alisema  Warioba  mbaye alikuwa mgeni rasmi kwenye  uzinduzi huo.

Aliwashauri  Wakristo  wawe  mfano kwa kutii  sheria za nchi  na kwamba wasichezee amani  kwani pia ni kinyume cha maandiko matakatifu ambayo  yanasisitiza  binadamu wote  kupendana





No comments:

Post a Comment