Maaskofu TAG Kanda ya Ziwa wasimikwa.

Maaskofu waliochaguliwa katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika mkoani Dodoma miongoni mwao ni pamoja na viongozi wa kanda ya ziwa kutoka majimbo ya Kagera, Geita, Mwanza na Jimbo la Mara wamesimikwa na Askofu Mkuu wa Kanisa la TAG, Dk Barnabas Mtokambali kwenye ukumbi wa  Mkuyuni  jijini Mwanza hivi karibuni.

Maaskofu waliosimikwa ni pamoja na Askofu Charles Mkumbo Jimbo la Mwanza,  makamu Askofu wake Mchungaji valentine Mbuke, Makamu Askofu wa Jimbo la Mara, Mchungaji Godson Sharua na Mchungaji Elias Jacob  kuwa makamu askofu wa Jimbo la Geita.

 Askofu Mkuu wa Kanisa la TAG, Dk Barnabas Mtokambal
 Askofu Mkuu Dk. Barnabas Mtokambali akiongea katika sherehe hizo za usimikaji zilihudhuriwa na  Makamu Askofu Mkuu Dk. Mhiche na Katibu Mkuu wa TAG, Ron Swai, Askofu wa maimbo ya Simiyu, Geita, Mara na Moshi aliwaasa wachungaji na watumishi wengine wa Mungu kujua wameitwa kuihubiri Amani na Haki hivyo, hawapaswi kuvunja vizuizi vyote vinavyoleta kiwingu cha kupoteza amani nchini.

 Dk. Mtokambali alikumbusha kanisa la Tanzania kutambua wakati umefika wa kuivuna  nchi,  yaani mioya ya watu wote wamjue Mungu wa kweli wala si vinginevyo, kutokana na watu wengi kupoteza dira na wanatapata kutafuta msaada kwa kuamini ushirikina, uchawi na kufuata imani potofu za ushoga ambayo ni machukizo kwa Bwana.


Mtumishi wa  Mungu alikemea vitendo viovu vinavyofanywa nchini hu susan kanda ya ziwa vya kishirikina na kuamini uchawi, mauaji ya walemavu wa ngozi, na vikongwe viachwe mara moja, huku akiongeza kuwa watu hao wana haki ya kuishi.

Askofu Mkuu Dk. Mtokambali akinukuu kutoka Kitabu cha Matendo ya Mitume 17:16-24 alisema, watumishi wa Mungu kuwa na huruma na uchungu juu ya taifa letu jinsi linavyopotoshwa na mafundisho potofu ya kuabudu miungu na sanamu ambayo ni machukizo mbele za Bwana.

No comments:

Post a Comment