Night of worship@CCC Upanga.


Night of Worship ni Event iliyokuwa ya namna yake katika Usiku wa jana ndani ya Kanisa la City Christian Center  (CCC) Upanga. Tamasha hilo lilikutanisha vikundi mbalimbali na watu kutoka maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es salaam katika kulitukuza na kuliinua Jina la Yesu.

The Nextleve Praise and Worship Team ,CCC Worship Team ,VCC, Glorious Celebration, John Lisu,Pastor Safari na John Kagaruki na wengine wengi walikuwepo kuhudumu usiku huo.

Glorious Celebration walikuwa wanafanya Live Recording ya Album yao chini ya Kampuni ya Hackneel Video Production katika usiku wa jana ambapo ilikuwa ya baraka sana.

Bupeh ni mwimbaji wa Gopsel Hip Hop kutokea Nchini Kenya aliyekuwepo kuhudumu usiku wa jana alikuwa akifanya Gopsel Hip Hop iliyotokea kuwa baraka kwa idadi kubwa ya watu,pia akatoa ushuhuda wa maisha yake ambao uliweza kugusa maisha ya wengi.

Watu walipata kumpokea Yesu kama Bwana na Mwokozi wa Maisha yao. Night of worship ni Ibada itakayo kuwa katika mwendelezo wa Ijumaa usiku ya Kila mwezi ndani ya Kanisa la CCC Upanga.
VCC Praise and Worship Team kwa stage.
John Lisu

Backup Team ya John Lisu
Sarah katikati na wezenzake wakisupport John Lisu Team
Ilikuwa fullshangwe mpaka asubuhi Watu walipata mda wa kutosha kusifu na kuabudu
Glorious Celebration wakirecord Live ndani ya CCC Upanda usiku wa jana.
Paul na wenzake wa Glorious Celebration wakikamua vocal kwa stage.
Flora Mbasha na Mmewe pia walikuwepo kuwakilisha usiku wa jana.

Paul kwa stage na Umenifanya Ibada


Bupe kutoka Kenya kwa stage akifanya Gospel Hip Hop
Abella na Paula ni wadau walikuwepo katika Event hiyo usiku wa jana.
Bupe na Catheline wakifanya collabo ya Gospel Hip Hop
Video Production Crew wakifanya Live recording ya Glorious Celebration usiku wa jana
Chini ya Hackneel Video Production. 
Audio Production Crew wakiwa kazini kurecord Album ya Glorious Celebration usiku wa jana

No comments:

Post a Comment